Bonifasia Rodriguez

Bonifasia Rodriguez (jina kamili kwa Kihispaniaː Bonifacia Rodríguez y Castro; Salamanca, Hispania, 3 Juni 1837 - Zamora, Hispania, 8 Agosti 1905) alikuwa bikira mwanzilishi mwenza wa shirika la kitawa la Watumishi wa Mt. Yosefu ambalo ndani ya Kanisa Katoliki linahudumia wanawake fukara na wasio na ajira[1] wapate maendeleo ya kiroho na ya kijamii kwa njia ya sala na kazi[2].

Picha yake halisi.

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 9 Novemba 2003, halafu Papa Benedikto XVI akatangaza mtakatifu tarehe 23 Oktoba 2011[3][4].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[5].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Ellsberg, Robert (2016). Blessed Among Us: Day by Day with Saintly Witnesses (kwa Kiingereza). Liturgical Press. uk. 453. ISBN 978-0-8146-4745-5. 
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/91832
  3. "The Church has three new saints". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-05-22. Iliwekwa mnamo 2021-08-01. 
  4. "Bonifacia Rodríguez Castro (1837-1905)". Iliwekwa mnamo 2011-12-15. 
  5. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

  • Servants of St. Joseph (Kihispania) [1]
  • Vatican News "Bonifacia Rodriguez Castro" [2]
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.