Cherero Shingo-njano

Ndege aina ya Kasuku
Cherero shingo-njano
Cherero shingo-njano katika hifadhi ya Tarangire
Cherero shingo-njano katika hifadhi ya Tarangire
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Psittaciformes (Ndege kama kasuku)
Familia: Psittaculidae (Ndege walio na mnasaba na kasuku wadogo)
Vigors, 1825
Jenasi: Agapornis
Selby, 1836
Spishi: A. personatus
Reichenow, 1887

Cherero (au kasuku-mapenzi) shingo-njano (pia cherero uso-mweusi; kisayansi Agapornis personatus) ni ndege wa kundi la kasuku katika familia Psittaculidae. Msambao wa asili ni Tanzania ya kaskazini na ya kati.

Maelezo hariri

Cherero shingo-njano ni kasuku mdogo aliye kijani hasa na kuwa na urefu wa sm 14.5. Upande wa juu ni kijani iliyoiva zaidi kuliko upande wa chini. Uso wake ni mweusi na ana domo jekundu kali na miviringo myeupe ya macho. Rangi ya manjano kwenye kidari inaendelea kwenye ukosi njano na upanuzi wa njano kwenye kisogo. Dume na jike wana muonekano wa nje unaofanana.

Ndege huyu huleta nyenzo za kiota katika domo lake kwenye shimo la mti ili kujenga kiota chao. Mayai ni meupe na kwa kawaida huwa na manne hadi matano kwenye kiota. Jike huatamia mayai kwa muda wa takriban siku 23 na makinda huondoka kwenye kiota kama siku 42 baada ya kuanguliwa.

Msambao hariri

Cherero shingo-njano ni wa asili ya Tanzania ya kaskazini na ya kati na ametambulishwa kwa Burundi na Kenya. Ingawa wameonekana katika pori huko Puerto Rico, labda ni matokeo ya ndege wa kipenzi waliotoroka, na hakuna uzazi uliorekodiwa. Pia wamezingatiwa huko Arizona. Katika Ulaya makoloni makubwa hutokea karibu na Nice, Ufaransa.

Ndege walioachiliwa nje ya msambao wa asili mara nyingi ni mvyauso kutokana na cherero uso-machungwa. Uso wao ni kijivu zaidi kuliko mweusi. Uvyausaji pia hutokea porini ambapo spishi hizo huingiliana, haswa ndani na karibu na Hifadhi ya Serengeti.

Mahusiano na watu hariri

Kama cherero wengine, cherero shingo-njano hufugwa duniani kote na watu wanaofurahi kuifanya. Ufugaji huu umesababisha rangi mpya ambazo hazitokei porini. Ndege zinazotokea nje ya msambao wao wa asili ni ama watorokaji au vizazi wao. Ndege kama hao wanaweza kupatikana katika pembe ya kaskazini mashariki mwa Tanzania na katika na karibu na Dar es Salaam, Mombasa, Nairobi na Naivasha. Kuna pia idadi ya ndege hao huko Ulaya na Amerika ya Kaskazini.

Ndege hawa wanaweza kujilisha nafaka anuwai, kama mahindi na mtama, mbegu za alizeti na matunda na wanaweza kutokea kwa makundi makubwa kiasi. Kwa hivyo wanaweza kuwa wasumbufu katika mashamba, k.m. katika maeneo ya karibu na Dodoma, Singida na Manyara, ambapo huitwa selengwa kwa lugha ya kieneo. Mnamo mwaka wa 2021 serikali ya Tanzania ilitangaza hatua za kudhibiti spishi hiyo, ingawa matumizi ya dawa za kemikali (kama inavyotumika dhidi ya kwelea domo-jekundu) ilikataliwa. Ilipendekezwa kwamba ndege hao wanapaswa kutegwa.

Picha hariri