Denis wa Paris

(Elekezwa kutoka Denis mfiadini)

Denis wa Paris alikuwa Mkristo wa karne ya 3 kutoka Roma (Italia).

Sanamu ya Mt. Denis akishika fuvu la kichwa chake, Notre Dame de Paris, Ufaransa.
Kifodini cha Mt. Denis na wenzake, Basilika la Mt. Denis.

Kadiri ya wanahistoria Wakristo[1]. chini ya kaisari Decius (250 BK), Papa Fabian alituma maaskofu 7 kutoka Roma kwenda Gallia (Ufaransa wa leo) wakahubiri Injili: Grasyano huko Tours, Trofimo huko Arles, Paulo huko Narbonne, Saturnini huko Toulouse, Denis huko Paris, Austremoni huko Clermont na Martial huko Limoges.

Akiwa askofu wa Paris (Ufaransa) aliuawa pamoja na padri Eleuteri na shemasi Rustiko kwa kukatwa kichwa kwa sababu ya imani yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 9 Oktoba[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. The Vetus Martyrologium Romanum (1961) under Die 18 Decembris: Quintodecimo Kalendas Januarii: "Turonis, in Gallia, Sancti Gatiani Episcopi, qui, a Sancto Fabiano Papa primus ejusdem civitatis Episcopus ordinatus est, et multis clarus miracolis obdormivit in Domino".
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

Marejeo mengine hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.