Kaunti ya Kirinyaga
Kaunti ya Kirinyaga ni mojawapo ya kaunti 47 za Kenya, iliyoko katika eneo la Kati mwa nchi, kwenye miteremko ya mashariki ya Mlima Kenya. Inapakana na Kaunti ya Embu mashariki na kusini, Kaunti ya Murang'a magharibi, na Kaunti ya Nyeri] kaskazini. Ina idadi ya watu takriban 610,411 kulingana na sensa ya mwaka 2019[1].. Mji wake mkubwa na makao makuu ni Kerugoya. Kirinyaga imegawanyika katika maeneo bunge 4: Mwea, Gichugu, Ndia, na Kirinyaga Central. Inajulikana kwa kilimo cha mpunga katika Bonde la Mwea, kilimo cha kahawa, na mchango wake mkubwa katika usambazaji wa chakula nchini Kenya.
Kaunti ya Kirinyaga | |
---|---|
Kaunti | |
![]() Vijana wakilima katika mradi wa umwagiliaji wa Mwea | |
![]() |
|
Kaulimbiu: "" | |
![]() Kaunti ya Kirinyaga katika Kenya | |
Nchi | ![]() |
Nambari | 20 |
Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 |
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Kati |
Mji mkuu | Kutus(Rasmi) |
Miji mingine | Kerugoya, Sagana, Wang'uru |
Serikali | |
Gavana | Anne Mumbi Waiguru |
Naibu wa Gavana | Peter Njagi Ndambiri |
Seneta | Daniel Karaba Dickson |
Mwakilishi wa wanawake | Purity Wangui Ngirici |
Bunge | Bunge la Kaunti ya Kirinyaga |
Wawakilishi Wadi | 20 |
Maeneo bunge | 4 |
Eneo | |
Jumla | km2 1 478.3 (sq mi 570.8) |
Idadi ya Watu | |
Jumla | 610,411 |
Msongamano | 413 /km² |
Majira ya Saa | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) |
Tovuti kirinyaga.go.ke |
Jiografia
haririKaunti ya Kirinyaga imepakana na Nyeri (magharibi), Murang'a (kusini magharibi) na Embu (mashariki).
Mlima kenya na msitu unaouzunguka uko kaskazini mwa kaunti. Theluji ambayo huyeyuka kutoka Mlima Kenya hutengeneza mito, k.v. Mto Thiba na Mto Kiganjo. Mito mingine iliyo katika kaunti hii ni Mto Sagana, Mto Nyamindi, Mto Rupingazi, Mto Thiba, Mto Rwamuthambi and Mto Ragati[2].
Kirinyaga huwa na tabianchi tropiki na hupata misimu miwili ya mvua.
Utawala
haririKaunti ya Kirinyaga imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo[3]:
Eneo Bunge | Kata |
---|---|
Mwea | Mutithi, Kangai, Wamumu, Nyangati, Murindiko, Gathigiriri, Teberer |
Gichugu | Kabare, Baragwi, Njukiini, Ngariama, Karumandi |
Ndia | Mukure, Kiine, Kariti |
Kirinyaga Central | Mutira, Kanyekini, Kerugoya, Inoi |
- Kirinyaga Central 122,740
- Kirinyaga East 135,559
- Kirinyaga West 114,660
- Mwea East 132,554
- Mwea West 104,828
- Mt. Kenya Forest 70
Tazama pia
haririMarejeo
hariri- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
- ↑ "Kirinyaga County Government". Iliwekwa mnamo 2018-04-30.
{{cite web}}
: Text "About Us" ignored (help) - ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-09-04. Iliwekwa mnamo 2021-09-04.
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Kirinyaga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |