Kontardo wa Este (Ferrara, Italia, 1216 - Broni, Pavia, Italia, 16 Aprili 1249) alikuwa mwana wa mtemi wa Ferrara. Dada yake, Beatrice, alikuwa malkia wa Hungaria. Hata hivyo Kontardo alijinyima cheo na mali akaishi miaka mingi kwa ufukara mkubwa bila makao maalumu akatembelea patakatifu pa Yerusalemu, Palestina[1].

Baadaye, akielekea patakatifu pa Santiago de Compostela, Hispania, aliugua njiani na kufariki amelala juu ya nyasi nyumbani mwa mkulima akatambuliwa baadaye tu, kutokana na miujiza kadhaa iliyotokea [2].

Tangu kale anaheshimiwa kama watakatifu. Papa Paulo V alithibitisha heshima hiyo tarehe 27 Septemba 1628.

Sikukuu yake ni tarehe 16 Aprili[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Gianna Vancini, Contardo d'Este: pellegrino da Ferrara a Broni, Ferrara, Este Edition, 2015, ISBN 9788867041626, OCLC 971545562.
  • Gianna Vancini, Contardo, il santo estense, Ferrara, Este Edition, 2003, OCLC 955375370.
  • Gianna Vancini, Inedita et rara: Contardo d'Este, santo pellegrino, patrono di Broni, Ferrara, Centro stampa Comune di Ferrara, 2001, OCLC 955374333.
  • Gianna Vancini e Giuseppe Sarina, Vita, miracoli, morte e gloria di S. Contardo protettore di Broni: spettacolo diviso in 5 atti, Azzano San Paolo, Junior, 2007, OCLC 955972521.
  • Luigi Ughi, Dizionario storico degli uomini illustri ferraresi, Ferrara, 1804.
  • Pompeo Litta, Famiglie celebri d'Italia. D'Este, Torino, 1835, ISBN non esistente.
  • Cristina Siccardi, San Contardo d'Este Palmiere protettore dell'Oltrepo, Torino 2019
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.