Ritriti

(Elekezwa kutoka Mafungo)

Ritriti (kutoka Kiingereza "Retreat") ni kipindi cha kujishughulisha na maisha ya Kiroho kwa kujitenga na kazi na mazingira ya kawaida.

Kijana mmonaki wa Kibuddha katika chumba cha ritriti, Yerpa, Tibet mwaka 1993.
Mseminari akisali peke yake kanisani, Weston, Massachusetts, Marekani.

Mara nyingi ritriti inaendana na kimya na saumu, ndiyo sababu inaitwa pia "mafungo".

Vipindi vya namna hiyo vinahimizwa katika dini mbalimbali, kama vile Uhindu, Ubuddha, Ukristo na Uislamu.

Katika Ukristo hariri

Kama nafasi ya kukutana na Mungu kwa urahisi na undani zaidi, ya kutafakari neno lake, ya kutulia pengine mbele ya tabenakulo, na hatimaye kuweka maazimio ya kuongoka na kufanya utume, ritriti inaagizwa na Kanisa Katoliki kwa mapadri na watawa, mbali ya kushauriwa kwa walei pia, walau mara kadhaa maishani, kiasi kwamba kuna rehema ya pekee kwa wanaoifanya kila mwezi.

Ritriti ikidumu muda mrefu zaidi inaweza kuitwa mazoezi ya kiroho, hasa ikifuata utaratibu maalumu wa Wajesuiti ulioanzisha na Ignas wa Loyola.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.