Miji bora duniani inatathminiwa kutokana na mazingira yake na maisha ya wakazi wake. Bila shaka vinaweza vikatumika vigezo tofauti pia.

Vienna hariri

Ni mji mkuu wa Austria; utafiti wa kimataifa umegundua kuwa ni eneo lililo bora zaidi kuishi kuliko mengine duniani kutokana na sifa mbalimbali, zikiwemo kiwango kidogo cha uhalifu na watu kuishi maisha bora na ya ustawi.

 
Vienna

Zurich hariri

Ni mji ulioshika nafasi ya pili kuishi duniani. Ni mji wa biashara wa Uswisi; unakadiriwa kuwa na wakazi 400,000. Mji huo upo kwenye kona ya ziwa Zunchi.

Auckland hariri

Ni mji unaoshika nafasi ya tatu. Upo katika fungukisiwa cha New Zealand, kusini mwa dunia. Una bandari kubwa na mpangilio mzuri wa barabara za juu na chini.


Munich hariri

Ni makao makuu ya mkoa wa Bayer nchini Ujerumani na ni mji wa tatu kwa ukubwa kwenye taifa hilo. Ujerumani umeuimarisha mji huu kuwa wa kiutamaduni na teknolojia.

Vancouver hariri

Ni mji uliopo Canada. Umeshika nafasi ya tano katika kumi bora. Ni mji wenye bandari na mandhari nzuri.

Dusseldorf hariri

Ni mji wa pili kwa ukubwa nchini Ujerumani. Umeshika nafasi ya sita duniani: ni makao makuu ya jimbo la North Rhine-Westphalia

Frankfurt hariri

Ni mji mwingine wa Ujerumani ambao umeshika nafasi ya 7. Upo mbali na wakazi wake kwa kuwa na maisha mazuri inaeleza kuwa unatoa elimu bora.

Geneva hariri

Ni mji mkuu wa Uswisi; umeshika nafasi ya 8. Ni mji ambao una benki ambazo mataifa mengi duniani yamehifadhi fedha zao na ni makao makuu ya pili ya UN ambayo inahusika na machapisho mbalimbali.

Copenhagen hariri

Ni mji mkuu wa Denmark ambao unashika nafasi ya 9. Ni mji unaosifika kwa kuwa na watu wanaoheshimu usawa wa kijinsia na mvuto wa ubunifu wa ujuzi wa majengo ya kitamaduni.

Sydney hariri

Ni mji wa Australia ulioshika nafasi ya 10; ni mji wenye vivutio vingi kama vile ufukwe, mipango mizuri ya ujenzi na bandari, daraja kubwa la kwenda angani, pia limekuwa kivutio cha utalii.