Mtumiaji:Ad scribendum/Amani Research Institute

Taasisi ya Utafiti ya Amani ni taasisi ya utafiti iliyoko Amani, katika Wilaya ya [[Muheza]], kwenye Milima ya Usambara Magharibi ya mkoa wa kaskazini mashariki mwa Tanzania ya leo. Milima hiyo ni sehemu ya Milima ambayo huanzia Kenya kupitia Tanzania, na ina misitu ya mawingu ambayo imevumilia kipindi kirefu cha maangamizi ya kipekee.

Usambara Magharibi

Taasisi ya Kilimo na Biolojia ya Amani, ilianzishwa mnamo 1902, katika nyakati za ukoloni, iliyokuwa wakati huo Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.

Taasisi ilianza kama kituo cha utafiti wa kibiolojia na kilimo, lakini iliongezeka haraka katika maeneo mengine ya utafiti katika miaka iliyofuata.

Mwanzo wa Taasisi ya Amani kilikuwa kituo cha upimaji kilimo huko Kwai, ambacho kilianzishwa Usambara tangu 1896.

Taasisi ya Amani ilianzishwa mnamo Septemba 1902 katika milima ya Usambara Mashariki iliyoko katikati mwa jiji la bandari ya Tanga, kwa maoni ya Franz Stuhlmann , mtaalam wa wanyama wa Ujerumani. Kazi ilianza mnamo 1903 na iliongozwa na mtaalam wa mimea, Albrecht Zimmermann. Zimmermann walifanya kazi huko Amani hadi 1920, wakati serikali ya Uingereza iliamuru wafukuzwe. Kuanzia 1905 hadi mwisho wa 1906, Franz Stuhlmann alikuwa mkurugenzi binafsi huko Amani.

Stuhlmann alianzisha upandaji wa miti ya gome ya cinchona katika Afrika Mashariki, ambayo ilitumiwa kwa utengenezaji wa kwinini dhidi ya malaria . Pia aliagiza upandaji wa mamia ya miti ya kafuri katika Usambara kutoka kwa mbegu zilizotumwa na Adolf Engler, mtaalam maarufu wa mimea huko, Berlin, na ambaye alikuwa amezipata kutoka Japani . [1] .

Stuhlmann alimleta Albrecht Zimmermann kwa Amani kwa kusudi la utafiti wa mimea. Zimmermann alikuwa anajulikana sana kama mtaalam wa kilimo cha kahawa na kwa muda mfupi aliiletea taasisi hiyo kutambuliwa kimataifa. Hapa, utafiti wa mbolea ulifanywa katika maeneo mbali mbali. Fiziolojia ya mimea, entomolojia, sumu ya mimea na uwezekano wa kudhibiti wadudu zote zilikuwa sehemu za uwanja wa kazi wa Taasisi, kama ilivyokuwa utafiti wa njia za kilimo na tiba ya mimea.

Amani ikawa arboretum (bustani ya mimea na miti) ya muhimu sana duniani. Aina zililetwa kutoka sehemu nyingi za ulimwengu kwa majaribio ya kilimo na masilahi kadhaa ya kiuchumi, kama mimea ya dawa matunda na viungo, miti yenye thamani, vipodozi, mpira, nyuzi, mafuta na mimea ya mapambo[2] .

Mwaka wa 1914 maktaba ya Amani ilikuwa na vitabu karibu 4,000 na majarida 300. Machapisho mengi na vielelezo vingi vilivyofanyika Amani vililetwa Berlin mwaka wa 1918, lakini mnamo 1943, herbarium ya Berlin ilipigwa na bomu na vyote viliangamizwa. [3]

Mmoja wa wageni waliotembelea Amani alikuwa Robert Koch, daktari maalum na mtaalam wa magonjwai, Profesa katika Chuo Kikuu cha Berlin, na Mkurugenzi wa Taasisi mpya ya Usafi na ya Magonjwa ya Kuambukiza[4] Alishiriki katika utafiti ulioendelea kufanywa katika Taasisi hiyo, na akaonyesha kuwa matukio ya msimu wa malaria yaliongezeka wakati wa masika, wakati maji katika mwezi mzima yalienea juu ya ardhi, kama husemekana katika Kiswahili 'Hakuna masika bila mbu' . Alionesha pia kipindi cha incubation kilikuwa cha siku 12 kwa ugonjwa huo. Mnamo Desemba, 1904, Koch alitumwa Afrika Mashariki ya Ujerumani kusoma homa ya ng'ombe katika Pwani ya Mashariki. Mwaka wa 1905, alishinda Tuzo ya Nobel ya Fiziolojia au Tiba "kwa uchunguzi na ugunduzi wake kuhusiana na ugonjwa wa kifua kikuu" [5]

Katika 1906 Robert Koch na timu yake walifika tena Amani, na baadaye walifanya safari kwenda Uganda, sehemu ya utafiti wao juu ya ugonjwa wa malale. Eneo la magharibi la Tanganyika, haswa karibu na maziwa, lilibahatisha ' janga ' la ugonjwa wa malale, ugonjwa ambao pia uliingia jirani, nchini Uganda. Mlipuko mkubwa wa ugonjwa huu ulikuwa umetokea Afrika Mashariki mwanzoni mwa karne (1896 -1910), na wengi walidhani ugonjwa huu ulitoka nchi za nje kama Afrika Magharibi au Kongo. Maelezo ya kwanza ya ugonjwa yalichapishwa huko Uganda, katika Hospitali ya Kanisa la Wamisionari wa Kanisa (CMS) mwaka wa 1901.


Koch alirudi tena mwaka wa 1906-7, kujaribu dawa ya atoxyl . Ilionekana siku zile kwamba ilikuwa bora kuliko dawa ya arseniki na mithali ya "risasi ya uchawi " ya mwanakimia Mjerumani Paul Ehrlich. Leo, njia za Koch kuendesha majaribio haya ya atoxyl, kuwa dawa ilikuwa na hatari na athari mbaya, hata upofu, imeleta maswali ya kimaadili [6] .

Ingawa Taasisi ya Utafiti ya Amani ilijulikana sana ulimwenguni wakati wa utawala wa kikoloni wa Ujerumani kama kituo cha utafiti wa kisayansi, [7] sifa yake ilendelea baada ya Waingereza walishika utawala wa nchi. [8]

Taasisi ya Baiolojia huko Amani, Afrika Mashariki ya Ujerumani.

Wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, Taasisi ya Utafiti ya Amani ilizidisha sifa yake ya kimataifa katika utafiti na wanasayansi katika kituo hicho walitengeneza bidhaa nyingi, pamoja na dawa na bidhaa za kemikali. [[Kwinine]] ilitengenezwa, na rangi kutolewa kwenye magome ya miti, vyakula na vileo, manukato, dawa, mpira, sabuni, mafuta na mishumaa, vifaa vyakushughulika na mashua, na nyingineo. [9] [10]

Waingereza walichukua utawala wa Tanganyika baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza.na waliendelea kazi za taasisi.

Taasisi ilisifika kwa sababu ya utafiti wake juu ya malaria wakati wa utawala wa kikoloni wa Briteni na jina lilibadilishwa mwaka wa 1949 kuwa Kitengo cha Malaria cha Afrika Mashariki. Kituo cha utafiti hakilihudumia Tanganyika tu bali pia Kenya, Uganda, Zanzibar na Somalia ya Uingereza katika kazi ya kuzuia malaria na magonjwa mengine yanayoambukizwa na wadudu.

Baada ya utawala wa kikoloni wa Uingereza, taasisi hiyo iliendelea kuchukua jukumu muhimu kama kituo cha utafiti nchini Tanzania.

Bustani ya Botani ya Amani sasa ina eneo rasmi la hekta 244. Kiasi zaidi imechukuliwa na Taasisi ya Kitaifa ya Utafiti wa Tiba (NIMR). Bustani ya mimea imeshughulikwa na kibinadamu, haswa karibu na kijiji cha Amani, ambapo iko sehemu ya NIMR. Kwa hivyo Bustani ya Botani ya Amani ina vyombo kadhaa vinavyohusika na usimamizi wake - Wizara ya Kilimo, Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) na NIMR. Maktaba yake iko katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na taasisi hushirikiana na chuo hicho kwa karibu. Siku hizi kusema kweli hakuna kilichobaki kwenye shamba la zamani la miti ya cinchona, ambalo lilikuwa karibu limeharibiwa kabisa katikati ya miaka ya 1960.

Karibu spishi 3000 zilikuwa bado zakupatikana karibu na Amani mnamo 2007. Leo viwanja hivi vya mimea vyingi vimeondolewa na vinaonekana vimerudishwa na spishi za asili. Aina za mimea kigeni zilizoletwa hapo bustanini ni suala muhimu ya kuhifadhisha katika wakati ujao.

Marejeo hariri

 

  1. "History of the BGBM Library". BGBM (kwa Kiingereza). 2013-01-14. Iliwekwa mnamo 2021-06-03. 
  2. Tropical Biology Association: Amani Nature Reserve - an introduction . Cambridge 2007 (PDF file; 381 kB), online at www.tropical-biology.org http://www.tropical-biology.org/wp-content/uploads/2015/01/AmaniNR_FINAL.pdf
  3. https://www.bgbm.org/en/history-collections-botanical-museum-berlin-dahlem-b-1
  4. Ernst, H. C. (1918). "Robert Koch (1843-1910)". Proceedings of the American Academy of Arts and Sciences. 53 (10): 825–827. JSTOR 25130022.
  5. https://www.nobelprize.org/prizes/medicine/1905/koch/biographical/
  6. https://www.spiegel.de/geschichte/robert-koch-der-beruehmte-forscher-und-die-menschenexperimente-in-afrika-a-769a5772-5d02-4367-8de0-928320063b0a
  7. Ref. note #6: Conte, 2002, p. 246; Conte, 2004, p. 13.
  8. Mwakikagile, Godfrey Life in Tanganyika in The Fifties; Dar es Salaam, Tanzania: New Africa Press, 2010, p. 164: "The Amani Research Institute....was established by the German colonial rulers and became world-famous as a tropical research institute."
  9. Report of the East Africa Commission, Cmd. 2387 (1925), p. 86....Owing to the blockade, overseas trade came to an end....The long drawn-out conflict inflicted serious damage on the colony."
  10. W.O. Henderson, "The war economy of German East Africa, 1914 - 1917," Economic History Review, xiii, 1943.