Ndjamena ni mji mkuu pia mji mkubwa kabisa nchini Chad ikiwa na wakazi 1,093,492 mnamo mwaka 2013.[1]

Jiji la N'Djamena
Nchi Chad
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 1,093,492

Ndani ya manisipaa kuna hara au mitaa kumi.

Mtaa wa N'Djamena

Jina hariri

Zamani mji ulijulikana kwa jina la "Fort Lamy". Tangu mwaka 1973 jina limekuwa Ndjamena, N'Djaména, N'Djamena au Ndjaména.

Jiografia hariri

Mji wa Ndjamena uko mahali ambako mito ya Chari na Logone inaungana. Ng'ambo ya mto uko mji wa Kousseri nchini Kamerun.

Historia hariri

Ndjamena ilianzishwa na Mfaransa Émile Gentil tarehe 29 Mei 1900 kama kambi ya kijeshi ikiitwa Fort-Lamy kama kumbukumbu ya kamanda Amédée-François Lamy aliyeuawa vitani kwenye mapigano ya Kousseri siku chache kabla ya kuanzishwa kwa Fort Lamy[2][3] .

Jina lilibadilishwa na rais François Tombalbaye kuwa Ndjamena mwaka 1973. Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Chad 1979 / 1980 mji uliharibika na wakazi wengi waliondoka mjini lakini katika miaka ya baadaye wengine wengi waliingia.[4]

Wakazi hariri

Mji ulikua sana na haraka. Huduma za maji, umeme na makao havitoshi tena.

Mwaka * Idadi ya Wakazi

Makabila na vikundi mjini mwaka 1993:

  • Waarabu wa Chad : 11,08 %
  • Ngambay : 16,41 %
  • Hadjeray : 9,15 %
  • Daza : 6,97 %
  • Bilala : 5,83 %
  • Kanembou : 5,80 %
  • Maba : 4,84 %
  • Kanouri : 4,39 %
  • Gor : 3,32 %
  • Kouka : 3,20 %
  • Sar : 2,24 %
  • Barma : 2,10 %

Uchumi hariri

Ndjamena ni kitovu cha uchumi wa Chad.

Elimu hariri

Ndjamena ina vyuo na shule mbalimbali kama vile.

Shule za Sekondari (Lycée) :

  • Lycée Félix Éboué (ya serikali)
  • Lycée technique commercial (ya seriali)
  • Lycée du Sacré-Cœur (binafsi - kikatoliki)
  • Lycée-Collège évangélique (binafsi kiprotestant)
  • Lycée Ibnou - Cinna (Kifaransa - Kiarabu)
  • Lycée Roi Faycal (Kiarabu)
  • Lycée Koweitien (Kiarabu)
  • Lycée d'Amérigue (ya serikali)
  • Lycée de Farcha (ya serikali)
  • Lycée Technique Industrielle
  • Lycée du Pont de Chagoua
  • Lycée de Waliya
  • Lycée de La Liberté
  • Lycée de la Gendarmerie, etc.

Vyuo Vikuu (Université) :

créée en 1970
  • Université Roi Fayçal (binafsi - kiislamu)

Taasisi za elimu ya juu (École Supérieure) :

  • ISSED - Institut Supérieur des Sciences de l'Éducation
  • ENAM - École Nationale d'Administration et de Magistrature
  • EIE - École Supérieure d'Électronique et d'Informatique
  • ENASS - École Nationale des Sciences Infirmières et Sociales
  • INJS - Institut Supérieur de la Jeunesse et des Sports
  • ENS - École Normale Supérieure
  • ENTP - École Nationale des Travaux Publics
  • ISTAP - Institut Supérieur des Techniques Appliquées

Marejeo hariri

  1. Cahiers de l'Afrique de l'Ouest Dynamiques de l'Urbanisation Africaine 2020: Africapolis, Une Nouvelle Géographie Urbaine. OECD. 20 fevereiro 2020
  2. Roman Adrian Cybriwsky, Capital Cities around the World: An Encyclopedia of Geography, History, and Culture, ABC-CLIO, USA, 2013, p. 208
  3. Zurocha-Walske, Christine (2009). Chad in Pictures. Twenty-First Century Books. uk. 17. ISBN 978-1-57505-956-3. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-04-30. Iliwekwa mnamo 2015-11-15.  Unknown parameter |url-status= ignored (help)
  4. Samuel Decalo, Historical Dictionary of Chad, Scarecrow, 1987, pp. 229–230

Viungo vya Nje hariri