Shahada ni ungamo wa imani ya Kiislamu.

Sehemu ya mfululizo wa makala juu ya

Uislamu

Imani na ibada zake

Umoja wa Mungu
Manabii
Misahafu
Malaika
Uteule
Kiyama
Nguzo za Kiislamu
ShahadaSwalaSaumu
HijaZaka

Waislamu muhimu

Muhammad

Abu BakrAli
Ukoo wa Muhammad
Maswahaba wa Muhammad
Mitume na Manabii katika Uislamu

Maandiko na Sheria

Qur'anSunnahHadithi
Wasifu wa Muhammad
Sharia
Elimu ya Sheria za KiislamuKalam

Historia ya Uislamu

Historia
SunniShi'aKharijiyaRashidunUkhalifaMaimamu

Tamaduni za Kiislamu

ShuleMadrasa
TauhidiFalsafaMaadili
Sayansi
SanaaUjenziMiji
KalendaSikukuu
Wanawake
ViongoziSiasa
Uchumi
UmmaItikadi mpyaSufii

Tazama pia

Uislamu na dini nyingine
Hofu ya Uislamu

Shahada kama mapambo kwenye ukuta wa msikiti wa Wazir Khan mjini Lahore (Pakistan)
Shahada kwenye bendera ya Uarabuni wa Saudia

Tamko hili lina maneno yafuatayo: لا إله إلا الله محمد رسول الله (Lā ilāhā illā-llāhu; muhammadun rasūlu-llāhi). Maana yake ni: "Hakuna mungu ila Allah; Muhammad ni mtume wa Allah". Katika sala maneno haya huanzishwa kwa "أشهد أن‎" (ash-hadu an yaani: Nakiri kwamba...).

Kwa maneno haya Mwislamu hutamka kuwa

  • Mungu (Allah) ni mmoja tu hakuna mwingine
  • Muhammad ni mtume na rasul wake wa mwisho.

Shahada ni moja ya nguzo tano za Uislamu. Hurudiwa kila siku na Mwislamu akifuata wajibu wake wa sala.

Kuna Washia kadhaa wanaoongeza maneno "Alīyun wali Allah" (علي ولي الله - "Ali rafiki yake Mungu") wakitaka kukiri ya kwamba katika imani yao Ali ni kiongozi teule wa Waislamu.

Kutamka shahada kwa imani ni tendo la kujiunga na Uislamu na kuwa Mwislamu.

Historia

Mfano wa kale wa shahada uko kwenye maandiko yaliyopo kwenye ukuta wa nje wa msikiti wa Kubba ya Mwamba mjini Yerusalemu uliojengwa kwa amri ya khalifa Abd al-Malik ibn Marwan mnamo mwaka 691. Hapa ina umbo lifuatalo: لا اله إلا الله وحده لا شريك له محمد رسول الله ‎ / la ilaha ila allahu wahdahu la sharika la-hu Muhammadun rasulu ʾllah(i) /„Hakuna mungu ila Allah peke, hana mwenzake, Muhammad ni mtume wa Allah". Sehemu yenye maneno yasiyotazamiwa leo kuwa sehemu ya shahada "lā šarīka la-hu" ni kutoka Kurani sura 6, 163.

Umbo jinsi nilivyo leo ni mapatano kati ya madhehebu ya Kisunni.

 
Bendera ya Somaliland inaonyesha shahada

Matumizi ya kisiasa

Kuna bendera ya nchi kadhaa zinazoonyesha shahada: