Tabata
Tabata ni kata katika mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikodi namba 12103 [1]. Kata hiyo ipo jijini, katika wilaya ya Ilala, mtaa wa Mandela.

Kata ya Tabata imegawanyika katika maeneo mengi; baadhi ya hayo ni kama Tabata Bima, Tabata Kimanga, Tabata Shule, Tenge, Tabata, Segerea, Mandela na Msimbazi.
Baadae ikaja kugawanyika na kuzaliwa kata kama Kimanga, Liwiti, Segerea na Kinyerezi.
Tabata Kimanga ni eneo ambalo lina watu wengi, wakiwemo wafanyabiashara, na shule za serikali zipatazo nne ambazo ni: Kimanga, Tumaini, Kisukuru na Makoka.
Pia katika sehemu hiyo kuna kituo kikubwa kimoja (stendi ya daladala).
Marejeo hariri
Makala hii kuhusu maeneo ya Dar es Salaam bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Tabata kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |