Wilaya ya Ilala
Coordinates: 6°49′26″S 39°14′56″E / 6.824°S 39.249°E
Wilaya ya Ilala ni wilaya mojawapo ya Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikadi namba 12000[1]. Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 634,924. Eneo lake ni km² 273.

Ilala yenyewe inahesabiwa kama manispaa ya Ilala ndani ya jiji la Dar es Salaam. Inajumlisha kitovu cha kihistoria cha Dar es Salaam ambako kuna ofisi nyingi za serikali pamoja na makampuni makubwa na maduka. Nafasi ya kitovu chenyewe ni Sanamu ya Askari; mitaa mingine maarufu ni Kariakoo, Buguruni, Kivukoni na kando yake iko Pugu.
MarejeoEdit
Kata za Wilaya ya Ilala - Tanzania | ||
---|---|---|
Buguruni •Chanika • Gerezani • Gongo la Mboto • Ilala • Jangwani • Kariakoo • Kimanga • Kinyerezi • Kipawa • Kisutu • Kitunda • Kivukoni • Kiwalani • Majohe • Mchafukoge • Mchikichini • Msongola • Pugu • Segerea • Tabata • Ukonga • Upanga Magharibi • Upanga Mashariki • Vingunguti |
Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Ilala kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |