Ubatizo wa Bwana ni sikukuu ya liturujia inayoadhimisha fumbo la Yesu kubatizwa na Yohane Mbatizaji katika mto Yordani kabla hajaanza utume wake mwenyewe.

Ubatizo wa Kristo ulivyochorwa ukutani na Giotto mwaka 1305 hivi (Cappella Scrovegni, Padua, Italia).
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Ndiyo sababu inatimiza kipindi cha Noeli kinachoadhimisha kwa muda mfupi miaka yote ya maisha yaliyofichika ya Yesu, mingi ikiwa aliitumia kama seremala kijijini Nazareti.

Kwa kuwa Yesu aliacha maisha hayo akaanza utume wake miezi tu baada ya Yohane Mbatizaji, jamaa yake, kuwatikisa Wayahudi wote akihubiri wawe tayari kwa ujio wa mtu mkubwa zaidi, akisema, “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto” (Math 3:11).

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ubatizo wa Bwana kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.