Chelsea F.C.
Chelsea Football Club[5][6] [7][8]ni klabu ya mpira wa miguu ya nchini Uingereza iliyo na maskani yake Fulham, London. Klabu hii ilianzishwa mwaka 1905, na kwa miaka mingi sana imekuwa ikishiriki ligi kuu ya Uingereza. Uwanja wao wa nyumbani ni Stamford Bridge ambao una uwezo wa kuingiza watazamaji 41,837, wameutumia uwanja huu tangu klabu ilivyoanzishwa.
Chelsea FC.svg | |||
Jina kamili | Chelsea Football Club | ||
---|---|---|---|
Jina la utani | The Blues The Pensioners (zamani)[1] | ||
Imeanzishwa | 10 Machi 1905[2] | ||
Uwanja | Stamford Bridge (Uwezo: 40,341[3][4]) | ||
Mmiliki | Todd Boehly Clearlake Capital Hansjörg Wyss Mark Walter | ||
Mwenyekiti | Bruce Buck | ||
Kocha | Thomas Tuchel | ||
Ligi | Ligi Kuu Uingereza (EPL) | ||
2021-22 | Premier League, 3th | ||
Tovuti | tovuti ya klabu | ||
|
Chelsea, kwa mara ya kwanza ilipata mafanikio makubwa mwaka 1955, ambapo walipata ubingwa wa ligi, na walishinda mataji kadhaa katika miaka ya 1960, 1970, 1990 na 2000. Klabu hii imefurahia zaidi mafanikio katika miongo miwili ilopita, kwa kushinda mataji makubwa 15 tangu mwaka 1997.
Nyumbani, Chelsea imeshinda ubingwa wa ligi mara nne, kombe la FA mara saba, kombe la ligi mara nne, pamoja na ngao za jamii mara nne. Na kimataifa Chelsea imeshashinda UEFA Cup Winners' Cups mara mbili, UEFA Super Cup moja, UEFA Europa League moja na UEFA Champions League moja. Chelsea ndio klabu pekee kutoka London kushinda UEFA Champions League, na ni moja kati ya klabu nne kutoka Uingereza, kuchukua makombe yote makubwa matatu ya Ulaya.
Kwa kawaida Chelsea huvaa jezi ya bluu, kaptula ya bluu na soksi nyeupe. Nembo ya klabu imebadilishwa mara nyingi kulingana na wakati na kuboresha muonekano wa klabu. Nembo ya sasa inaonesha picha ya simba akiwa amebeba mkuki. Tangu Julai 2003, Chelsea imekuwa ikimilikiwa na bilionea wa Kirusi, Roman Abramovich. Tarehe 7 Mei 2022, Chelsea ilithibitisha kwamba masharti yametimiza na kikundi kipya cha umiliki, kinachoongozwa na Todd Boehly, Clearlake Capital, Mark Walter na Hansjörg Wyss, kununua klabu hiyo.[9] Mnamo tarehe 25 Mei 2022, serikali iliidhinisha kuuzwa kwa Chelsea kwa £4.25bn. Mnamo tarehe 30 Mei 2022, mauzo yalikamilika, na hivyo kumaliza umiliki wa miaka 19 wa Abramovich.[10]
Wachezaji Edit
Kikosi cha timu ya kwanza Edit
Kama ilivyokuwa tarehe 10 Agosti 2022, kulingana na vyanzo mseto katika tovuti rasmi.[11]
Note: Flags indicate national team as has been defined under FIFA eligibility rules. Players may hold more than one non-FIFA nationality.
|
|
Nje kwa mkopo Edit
Note: Flags indicate national team as has been defined under FIFA eligibility rules. Players may hold more than one non-FIFA nationality.
|
|
Wa ziada na walio chuoni Edit
Orodha ya wachezaji wa kikosi cha ziada na walio chuoni ambao wamewahi kucheza kikosi cha kwanza.
Note: Flags indicate national team as has been defined under FIFA eligibility rules. Players may hold more than one non-FIFA nationality.
|
|
Mchezaji Bora wa Mwaka Edit
Chanzo: Chelsea F.C.
Tuzo Edit
- Ligi Kuu (6) 1954-1955, 2004-2005, 2005-2006, 2009-2010, 2011-2012, 2016-2017
- FA Cup (7) 1970, 1997, 2000, 2007, 2009, 2010, 2018
- Kombe la Ligi (4) 1965, 1998, 2005, 2007;
- Ngao ya Jamii (4) 1955, 2000,2005, 2009
- UEFA Cup Winners' Cup (2) 1971, 1998
- UEFA Super Cup (1) 1998, 1999, 2003
- Full Members Cup (2) 1986, 1990
- FA Youth-cup (3) 1960, 1961, 2010
Tanbihi Edit
- ↑ Chelsea's first cup final – a century ago. Chelsea FC (23 April 2015).
- ↑ Team History – Introduction. Chelsea FC.
- ↑ General Club Information (en). | site=chelseafc.com.
- ↑ Premier League Handbook 2020/21. Premier League.
- ↑ Danyal Khan, Jake Stokes (2022-05-03). Chelsea news and transfers LIVE: Todd Boehly takeover hint, Abramovich fear (en). Football.London. Iliwekwa mnamo 2022-05-03.
- ↑ Bobby Vincent (2022-05-03). Chelsea could look to reunite Lautaro Martinez and Romelu Lukaku in the summer (en). Football.London. Iliwekwa mnamo 2022-05-03.
- ↑ Luke Thrower (2022-05-04). Glen Johnson urges Chelsea to offer Jorginho a new contract amid transfer links (en). Football.London. Iliwekwa mnamo 2022-05-04.
- ↑ Luke Thrower (2022-05-04). Chelsea bidder Lord Coe warns club to find quick takeover solution (en). Football.London. Iliwekwa mnamo 2022-05-04.
- ↑ Club statement (en-gb). www.chelseafc.com. Iliwekwa mnamo 2022-08-13.
- ↑ https://twitter.com/fabrizioromano/status/1531290432327634944 (en). Twitter. Iliwekwa mnamo 2022-08-13.
- ↑ Men: Senior. Chelsea F.C..
Men: On Loan. Chelsea F.C..