Medici ni jina la familia ya Firenze katika Italia ya Kati iliyokuwa muhimu upande wa siasa, uchumi na utamaduni, hasa wakati wa karne ya 15 na 16 BK.

Nembo la familia katika Jumba la Medici mjini Firenze
Cosimo di Medici (1389-1464)) mtawala wa Firenze

Mapapa watatu wa Kanisa Katoliki walikuwa wa ukoo huo, pamoja na watawala mbalimbali za mji wa Firenze; watoto wao walioa au kuolewa katika familia za wafalme wa Ulaya.

Walijenga utajiri katika biashara ya kitambaa wakaendelea kuunda benki kadhaa zilizokuwa aina mpoya ya biashara wakati ule. Uwezo wao wa kiuchumi waliutumia baadaye kisiasa.

Watawala na Mapapa wa ukoo wa Medici waliajiri wasanii wengi na kugharimia pia wataalamu, hivyo wakajenga kipindi cha utamaduni wa juu cha Italia kilichong'aa kote Ulaya.

Akina Medici mashuhuri hariri

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Medici kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.