Bolivia (jina linatokana na shujaa Simon Bolivar) ni nchi isiyo na mwambao wa bahari katika Amerika Kusini.

Bolivia
Ramani ya Bolivia
Mji wa La Paz
Uyuni

Imepakana na Brazil, Paraguay, Argentina, Chile na Peru.

Jiografia hariri

Nchi inakatwa na safu mbili za milima ya Andes zenye kimo hadi mita 6500 juu ya UB.

Nyanda za juu (kwa Kihispania: "Altiplano") zinakaliwa na wakazi wengi (80%) ziko kwenye kimo cha mita 3.000 hadi 4.000. Altiplano ni takriban theluthi moja ya eneo la nchi; sehemu nyingi ni tambarare ya "llanos" ambayo ni nchi ya chini yenye joto ambayo ina sehemu mbili: savana kavu za Gran Chaco na misitu minene ya beseni ya Amazonas.

Ziwa la Titicaca liko kwenye Altiplano.

Bolivia ni kati ya nchi maskini zaidi za Amerika Kusini.

Watu hariri

Tofauti na nchi nyingine za bara hilo, wakazi asilia (Waindio) ni sehemu kubwa ya wananchi (55%), wakifuatwa na machotara (30%) na watu wenye asili ya Ulaya (15%).

Lugha rasmi ziko 37, kuanzia Kihispania na lugha nyingi asilia.

Upande wa dini, Kanisa Katoliki linaongoza (78%), likifuatwa na Uprotestanti (19%).

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

  Makala hii kuhusu maeneo ya Bolivia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bolivia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.