Mae Carol Jemison (alizaliwa tarehe 17 Oktoba 1956) ni mwanakemia, tabibu na mwanaanga wa Marekani. Pia ni Mmarekani mweusi wa kike wa kwanza aliyefika kwenye anga-nje.

Mae Jemison

Mwaka 1987 alijiunga na NASA akateuliwa kushiriki katika safari ya 50 ya mradi wa space shuttle kwenye mwaka 1992 aliposimamia majaribio ya kiganga katika hali pasipo graviti.

Mwaka 1993 aliondoka kwenye NASA akaanza kufundisha kwenye vyuo vikuu na kuwa na kampuni yake binafsi.

Maisha ya zamani

 
stempu ya Mae Jemison

Jemison alizaliwa huko Decatur, Alabama. Alihamia Chicago akiwa na umri wa miaka mitatu. Ndugu na dada yake ni Ada na Charles Jemison. Kuanzia zamani, alionyesha upendo wa sayansi. Wazazi wa Jemison walimsaidia kufuatilia shauku yake kwa sayansi na mambo ya anga. Alipokuwa mtoto, alitumia muda mwingi katika maktaba. Alisoma vitabu kuhusu anga-nje na teknolojia.

Elimu

Jemison alihitimu kutoka shule ya sekondari akiwa na umri wa miaka 16. Alisoma kwenye Chuo Kikuu cha Stanford hadi kupata Shahada ya Awali katika uhandisi wa kemia mwaka 1977. Alitimiza pia masharti ya shahada katika somo la Utamaduni wa Wamarekani Weusi. Wakati wa masomo yake, Jemison alijihusisha na shughuli nje ya madarasa. Hizi ni pamoja na ngoma, michezo ya ukumbini, na kazi ya kujitolea. Pia alikuwa kiongozi wa Umoja wa Wanafunzi Weusi.

Baada ya Stanford aliendelea kusoma tiba kwenye Chuo Kikuu cha Cornell alimomaliza na shahada ya uzamivu yaani daktari ya tiba kwenye mwaka 1982. Alifanya kazi ya tibabu kwa muda mfupi Marekani akaendelea kujitolea kama bingwa wa tiba katika Peace Corps ya Marekani. Alitumwa Sierra Leone na Liberia alipohudumia kwenye miaka 1983 hadi 1985.

Mwanaanga

Video fupi ya NASA inayomwonyesha Mae Jemison

Baada ya kurudi kwao aliona nafasi ziko kwenye mradi wa NASA ambako wanaanga walitafutwa. Alikubaliwa hatimaye mwaka 1987 akaingia katika mafunzo kwa safari kwenye anga-nje. Mwaka 1992 Jemison alirushwa katika safari ya kumi ya maabara ya angani. Alihusika katika uchunguzi wa athira ya graviti kwa mbegu wa mimea na wanayama kama samaki, chura na wadudu. Sehemu nyingine ya majaribio aliyoendesha yalihusu athira ya graviti kwa mata kama vile kioo, kauri au aloi za metali mbalimbali.

Mafanikio

Baada ya kutoka kwenye utumishi wa NASA Jemson alianzisha kampuni yake ya utafiti wa teknolojia kwa maisha ya kila siku. Aliitwa kuwa profesa kwa teknolojia ya mazingira kwenye Chuo cha Dartmouth, Hanover, New Hampshire. Hapa aliongoza taasisi ya "Jemison Institute for Advancing Technology in Developing Countries".

Jemison ameshinda tuzo nyingi tangu wakati wake katika anga-nje. Aliitwa kama mmoja wa wanawake 50 muhimu zaidina gazeti la Ebony. Yeye ni mojawapo ya watu maarufu kwenye: National Medical Association Hall of Fame, Texas Science Hall ya Fame, na National women hall of fame. Jemison pia amekuwa kwenye mipango michache ya televisheni, ikiwa ni pamoja na mpango wa PBS wa Afrika pia wa Amerika. Pia anasema kwa umma juu ya maisha yake na ushawishi wake. Shule ya Umma ya Mae C. Jemison iliitwa jina lake.

  Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mae Jemison kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.