Metodi I wa Konstantinopoli
Metodi I wa Konstantinopoli (Siracusa, leo nchini Italia, 788 hivi – Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 14 Juni 847) alikuwa mmonaki na mwandishi wa Kikristo wa Dola la Bizanti.
Alifungwa gerezani kwa sababu ya kutetea matumizi ya picha takatifu[1], lakini hatimaye akawa Patriarki wa Konstantinopoli tangu 4 Machi 843 hadi kifo chake.
Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.
Tazama piaEdit
TanbihiEdit
MarejeoEdit
- The Oxford Dictionary of Byzantium, Oxford University Press, 1991.
Viungo vya njeEdit
- Methodius I article in the Catholic Encyclopedia (1910)
- St Methodius the Patriarch of Constantinople Orthodox Icon and Synaxarion
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |