Riali ya Zanzibar ilikuwa fedha halali iliyotolewa na Usultani wa Zanzibar kuanzia mwaka 1882 (1299 AH). Amri ya kuanzisha pesa hii ilitolewa na Sultani Barghash ibn Said ibn Sultan.

Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Ilipatikana kwa sarafu za riali 5, 2 1/2, 1, nusu na robo riali. Iligawiwa katika paisa 136.

Pamoja na riali, matumizi ya rupia ya Uhindi na Dolar ya Maria Theresia yalikuwa kawaida.

Mwaka 1908 Usultani (wakati ule ulikuwa tayari nchi lindwa chini ya Uingereza) uliacha riali na kutumia fedha ya rupia sawa na majirani kwenye bara yaani Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na Afrika ya Mashariki ya Kiingereza.

Sarafu hariri

Mwaka 1882 (AH 1299) sarafu za paisa 1 na riali ¼, ½, 1, 2½ na 5 zilipelekwa nchini. Paisa ilikuwa sarafu ya shaba. Riali ndogo zilikuwa za fedha na sarafu za riali 2½ na 5 za dhahabu.

Viungo vya nje hariri