Veronika Giuliani
Veronika Giuliani (Mercatello sul Metauro, Marche, Italia, 27 Desemba 1660 - Città di Castello, Umbria, Italia, 9 Julai 1727) alikuwa mmonaki wa urekebisho wa Wakapuchini wa Utawa wa Mt. Klara.

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu bikira. Ingawa aliheshimiwa hivyo mara baada ya kufa, kesi ya kumtangaza rasmi ilicheleweshwa na uchunguzi wa maandishi yake marefu.
Papa Pius VII ndiye aliyemtangaza mwenye heri mnamo Juni 1804, halafu Papa Gregori XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 26 Mei 1839.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyofariki dunia[1] au kesho yake.
Maisha Edit
Maandishi yake mwenyewe yanasimulia alivyoanza kujaliwa karama za pekee akiwa na umri wa miaka 3 tu, alipokuwa anaitwa Orsola.
Alijiunga na Waklara Wakapuchini wa monasteri ya Città di Castello mwaka 1667 ambapo akawa abesi tangu mwaka 1716 hadi kifo chake.
Kwa namna ya pekee aliambatana na Yesu msulubiwa kadiri ya karama ya Fransisko wa Asizi.
Kanisa Katoliki linakubali ukweli wa madonda matakatifu aliyosema alikuwanayo tangu tarehe 5 Aprili 1697 hadi kifo chake.
Maandishi Edit
Kwa agizo la padri aliyemuongoza kiroho, aliandika kirefu (kurasa 22,000 kwa mikono bila ya sahihisho lolote) kumbukumbu za maisha yake yote, ambazo zilitolewa baada ya kifo chake kwa jina Il Tesoro Nascosto (ni magombo 36).
Kutokana na shajara hiyo, Veronika Giuliani anahesabiwa kati ya Wakristo wanasala waliojaliwa mang'amuzi ya juu zaidi.
Tazama pia Edit
Tanbihi Edit
Viungo vya nje Edit
- St. Veronica Giuliani Archived 1 Juni 2002 at the Wayback Machine. at AmericanCatholic.org Saint of the Day
- St. Veronica Giuliani Archived 20 Desemba 2007 at the Wayback Machine. at Saints Alive
- Saint Veronica Giuliani Archived 3 Mei 2008 at the Wayback Machine. at Patron Saints Index
- Incorrupt Bodies of the Saints Archived 14 Juni 2008 at the Wayback Machine. at Catholic Apologetics Information
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |