Wilaya ya Siha ni mojawapo kati ya wilaya 7 za Mkoa wa Kilimanjaro yenye msimbo wa posta 25400.

Mahali pa wilaya ya Siha katika mkoa wa Kilimanjaro.

Wilaya hii ilianzishwa mwaka 2007 kutokana na maeneo ya wilaya ya Hai.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 139,019 [1]. Wilaya ya Siha inakaliwa na wakazi wa makabila mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali za nchi na nje ya nchi, wakiwemo wenyeji wa wilaya hiyo Wachagga (Wasiha).

Wasiha, kama walivyo Wachagga wengine, wakijihusisha na shughuli mbalimbali za uchumi, vikiwemo biashara, kilimo pamoja na ufugaji, ikiwa wanalima mazao makuu ya kahawa, ndizi, mahindi, maharage, viazi na mazao mengine ya biashara na chakula.

Wasiha wanasema moja kati ya lahaja nyingi za Kichagga zilizopo mkoa wa Kilimanjaro wakiwa na mchanganyiko na muingiliano mkubwa na lahaja ya Kimachame wakiwa ndio wenyeji halisi wa wilaya hiyo wakikaa na kuwekeza maisha yao kwa wingi upande wa kaskazini magharibi mwa wilaya hiyo. Lugha ya Wachagga wa Siha inalandana sana na ile ya Machame, hata hivyo hutofautiana kidogo sana kwenye matamshi na maana za maneno, ila wanaelewana kwa asilimia kubwa ukilinganisha na Wachagga wengine, hata majina wanayotumia mara kwa mara utayasikia yakilandana.

Wasiha kama walivyo Wachagga wengine pia, wana koo tawala ambazo ndizo koo zinazosikika zaidi. Koo hizo ndizo koo zilizotoa viongozi wa kitamaduni (Mangi) wa kabila hilo zikiwemo Kileo, Orio, Mmari, Mwandri, Munuo, na koo nyingine ndogondogo kama vile Mrang'u, Mosi, Maseri, Masaki. Ni nadra sana kusikia Mangi wa Siha ila kwa sasa Utawala wa Umangi unashikiliwa na ukoo wa Kileo.

Tanbihi hariri

Ramani Wilaya au manisipaa Wakazi (2022) Tarafa Kata Kijiji Eneo km²
 
Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro
Wilaya ya Hai 240,999 17 1,217
Wilaya ya Moshi Vijijini 535,803 32 1,300
Wilaya ya Moshi Mjini 331,733 21 63
Wilaya ya Mwanga 148,763 20 1,831
Wilaya ya Rombo 275,314 28 1,471
Wilaya ya Same 300,303 34 6,221
Wilaya ya Siha 139,019 17 1,217
Jumla 1,861,934 152 13,209
Wilaya ya Siha hii ilianzishwa mwaka 2007 kutokana na maeneo ya wilaya ya Hai.
Marejeo: Mkoa wa Kilimanjaro
  Kata za Wilaya ya Siha - Mkoa wa Kilimanjaro - Tanzania  

Biriri | Donyomurwak | Gararagua | Ivaeny | Karansi | Kashashi | Kirua | Livishi | Makiwaru | Miti Mirefu | Nasai | Ndumeti | Ngarenairobi | Olkolili | Ormelili | Sanya Juu | Songu

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Siha kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Isipokuwa usitaje majina ya viongozi waliopo sasa maana wanabadilika haraka mno.