Ibaga ni kata ya Wilaya ya Mkalama katika Mkoa wa Singida, Tanzania yenye msimbo wa posta 43509[1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 11,712 waishio humo. [2]

Kata ya Ibaga
Nchi Tanzania
Mkoa Singida
Wilaya Wilaya ya Mkalama
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 10,672

Pamoja na kuwa ni moja kati ya kata zinazounda tarafa ya Kirumi, Ibaga hapo kale ilijulikana kwa jina la utani Zaire Ndogo. Wakati huo mji huu ulikuwa na watu wengi waliotoka sehemu mbalimbali za nchi kuja kustaajabu na kujionea ubize uliokuwepo hapo kwa kuwa ni kitovu cha biashara katika ukanda wa Iramba Mashariki.

Wakati huo kulikuwa na usafiri wa kutoka Ibaga kwenda Arusha hadi Mererani wilayani Simanjiro kwa ajili ya biashara na uchimbaji madini. Kwa sasa kuna usafiri wa mabasi kutoka Singida Ibaga hadi Meatu na Mwanza, Shinyanga, Maswa pamoja na usafiri wa mabasi kutoka Arusha hadi Ibaga.

Madini ya shaba, kwa mujibu wa kampuni kubwa za utafiti zilizofanya utafiti, yapo chini sana, hivyo inahitaji mtaji mkubwa sana wa kuwekezwa ili uzalishaji uwe na tija.

Tayari Ibaga ina miundombinu ya maji na umeme wa uhakika, huku ikielezwa kuwa, Serikali ipo mbioni kuanza kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Shukrani kwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dr.Samia Suluhu Hassan na waziri wa nishati kwa kuhakikisha mradi wa umeme unafikia wananchi kwa wakati. Bado vijiji vichache Sana Hadi sashisho hili likihaririwa, Juni 2023.

Ibaga kama ilivyo kwa jimbo la Mkalama imepata mbunge, Francis Mtinga, ambaye ameonesha kuwa na upendo na wananchi wa jimbo lote kwani kiu yake ya kweli ya kuwatumikia wananchi imeanza kuzaa matunda bado asubuhi.

Ibaga imerudi tena kuwa juu kutokana na uchumi kupanda kwa kasi: hii inatokana na biashara inayofanyika kati ya Mwanza, Arusha, Singida na Igunga.

Ukiutazama mji wa Ibaga kwa sasa unakimbilia kuwa mamlaka ya mji mdogo: hii ni kutokana na kuunganisha vijiji vya jirani kama Igengu, Mkiko, Kidaru, Tyegelo, Luono, Ndurumo, Mpambala, Lugongo, Nyahaa, Mkalama, Ilongo, Ilangida, Endasiku, Matongo, Isene, Nkinto, Mtamba, Kinyambuli na hata Mwangeza.

Machimbo ya madini ya shaba yaliyopo Ilangida yameuongezea mji huu mdogo umaarufu.

Baada ya ugunduzi huo maisha ya hapa yamepanda juu: chakula na malazi vipo bei ghali; nyumba unaweza ukapata kwa ajili ya kupanga kwa kuanzia shilingi elfu kumi.

Viwanja navyo vipo bei juu; kwa sasa japo nyumba nzuri za wageni, zina mandhari safi ambayo mtu kutoka mjini ataishi na kujisikia yupo bado mjini.

Kituo cha polisi pamoja na mahakama vinahakikisha amani ipo masaa 24 siku 7 za wiki, hivyo ustawi wa mji huu unakwenda kwa kasi.

Kuna mnara wa Airtel, Zantel, Halotel na Vodacom.

Sehemu za kula starehe zipo kama baa ambapo kuna vinywaji baridi aina zote kwa bei rahisi.

Soko la Ibaga linapanuka hata kulishinda soko la mji kama Ndago ambapo kuna umeme.

Kuna mnada wa kila mwezi ambao ni sikukuu ya kila tarehe moja ya mwezi, pamoja na gurio maarufu kama lukule ya diwani kila siku ya jumamosi.

Ibaga ni kituo cha ununuzi wa mazao mbalimbali ya biashara kama karanga, ufuta, choroko, alizeti, mtama, uwele, mahindi n.k.

Kuna taasisi za elimu; shule mbili za msingi yaani Kilimani na Ibaga pamoja na sekondari ya kata ya Ibaga.

Wakazi wa Ibaga kwa sasa ni wenyeji yaani Wanyisanzu, Wanyiramba na Wasukuma kwa kiasi kidogo na watu kutoka sehemu mbalimbali ambao ni mmojammoja.

Katika masuala ya kijamii na kiutawala kuanzia mwaka 2015 kumekuwa na mwamko wa vijana kusaka fursa za kiuongozi kuanzia ngazi ya kijiji, kata, jimbo hadi taifa.

Uwepo wa kikundi maarufu cha ESAMA unaipa Umaarufu wilaya ya Mkalama na Ibaga, kwani ndani ya kikundi hicho mna vijana wataalamu na wenye nia njema ya kuinyanyua wilaya.

Lakini pia uwepo wa vijana wasomi na wenye vipaji katika mji huo, ambao unakaribia kuwa 'mamlaka ya mji mdogo', ni kichocheo kingine cha maendeleo kwa siku zijazo. Wamo vijana waandishi wa habari, watunzi wa riwaya na waandishi wa vitabu; akiwemo Joseph Shaluwa akijulikana kama JOPASHA.

Shaluwa kwa kutumia kampuni yake, anasambaza vitabu vya shule za msingi, sekondari na dini.

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Singida bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ibaga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.
  Kata za Wilaya ya Mkalama - Mkoa wa Singida - Tanzania  

Gumanga | Ibaga | Iguguno | Ilunda | Kikhonda | Kinampundu | Kinyangiri | Matongo | Miganga | Mpambala | Msingi | Mwanga | Mwangeza | Nduguti | Nkalakala | Nkinto | Tumuli