Jiografia ya Kenya

Jiografia ya Kenya inahusu nchi hiyo ya Afrika Mashariki ambayo ni ya 47 kwa ukubwa duniani ikifuata mara Madagaska km2 580 367 (sq mi 224 081) ikiwa na eneo la kilomita mraba 580,367 (maili mraba 224,081).

Mlima Kenya ni kilele cha juu kabisa nchini. Kenya imepata jina lake kutoka mlima huo.

Kutoka pwani ya Bahari ya Hindi, nyanda za chini zimeinuka hadi milima ya kati. Milima hii imetenganishwa na eneo la Bonde la Ufa; sehemu tambarare yenye rutuba upande wa mashariki. Milima ya Kenya ni kati ya zilizofaulu kwa kilimo barani Afrika.

Eneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) m 5 199 (ft 17 057) na ni eneo lenye mito ya barafu. Ng'ambo ya mpaka wa Tanzania Mlima Kilimanjaro (m 5 895 (ft 19 341)*) huweza kuonekana upande wa kusini.[1]

Kenya ni nchi yenye jua kali na nguo za majira ya joto huvaliwa mwaka mzima. Hata hivyo, huwa na baridi usiku na pia asubuhi na mapema.

Hali ya hewa ina joto na unyevu sehemu za pwani, joto kiasi sehemu za bara na ni kame katika sehemu za kaskazini na kaskazini-mashariki mwa nchi. Hata hivyo kuna mvua nyingi kati ya Machi na Aprili, na mvua ya kadiri kati ya Oktoba na Novemba. Halijoto huwa juu zaidi miezi hii yote.

Mvua ya masika hunyesha kuanzia Aprili hadi Juni. Mvua ya vuli nayo hunyesha kuanzia Oktoba hadi Desemba. Wakati mwingine mvua hii huwa nyingi na aghalabu hunyesha wakati wa alasiri na jioni. Majira ya joto jingi ni kuanzia Februari hadi Machi nayo ya baridi ni Julai hadi Agosti.

Wastani wa halijoto
Mji Mwinuko (mita) Upeo wa juu (°C) Upeo wa chini(°C)
Mombasa (Mji wa Pwani)    17 30.3 22.4
Nairobi(Mji Mkuu) 1,661 25.2 13.6
Eldoret align = "center" 3,085 23.6 9.5
Lodwar (Sehemu kame nyanda za juu) 506 34.8 23.7
Mandera (Sehemu kame nyanda za juu) 506 34.8 25.7

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Rough Guide (2006). Rough Guide Map Kenya [map], 9 edition, 1:900,000, Rough Guide Map. Cartography by World Mapping Project. ISBN 1-84353-359-6.