Liturujia ya Antiokia

Liturujia ya Antiokia, inayoitwa pia Liturujia ya Siria, ni jina la taratibu za ibada ya Wakristo ambayo ina asili yake katika mji wa Antiokia wa Siria (siku hizi umo katika mipaka ya Uturuki) ambao katika karne ya 1 ulikuwa kituo kikuu cha umisionari wa Kanisa, halafu ukawa na shule ya teolojia muhimu kama ile shindani ya Aleksandria (Misri).

Liturujia ya Kimungu ikiadhimishwa katika monasteri ya Mt. Marko.

Wanaotumia liturujia hiyo ni hasa Kanisa la Kiorthodoksi la Siria na madhehebu yenye uhusiano naye kihistoria (hasa matawi ya Kanisa la Kiorthodoksi la Kisiria la Malankara kutoka India), na yale yaliyotokana nalo, yakiwa pamoja na Kanisa Katoliki la Kisiria na Kanisa Katoliki la Kimalankara. Kwa kiasi kikubwa liturujia hiyo ni pia ya Kanisa la Wamaroni.

Historia hariri

 
Adhimisho la Kiorthodoksi la Kisiria katika monasteri ya Mosul, (leo nchini Iraq), mwanzoni mwa karne ya 20.

Liturujia hiyo ilitokana hasa na ile ya Kigiriki iliyotumiwa kwanza na Patriarki wa mji huo (kama Ignas wa Antiokia mwanzoni mwa karne ya 2), lakini, baada ya farakano la mwaka 451 lililofuata Mtaguso wa Kalsedonia, ilitafsiriwa katika lugha ya Kiaramu, iliyokuwa ya kawaida zaidi katika maeneo yote ya kandokando.

Matini ya Kiaramu ya zamani zaidi yaliyobaki hadi leo ni ya karne ya 5[1] Yanatunza kumbukumbu muhimu kuhusu liturujia ilivyokuwa wakati huo, nazo zinatusaidia kufuatilia mabadiliko yaliyofanyika baadaye.

Kuanzia anafora ya awali, iliyotafsiriwa kutoka ile ya Kigiriki ya Mt. Yakobo, zilitungwa nyingine nyingi, si chini ya 39.

Wakatoliki ndio waliofanya utafiti bora zaidi juu ya liturujia hiyo, wakitoa vitabu rasmi ili kupunguza fujo iliyojitokeza pengine kati ya Waorthodoksi wa Mashariki. Kati ya anafora hizo zote, wanazitumia saba tu.

Pengine masomo ya Biblia yanafanyika kwa Kiarabu, lugha ya kawaida ya waamini wengi huko Mashariki ya Kati. Lakini waamini wengi zaidi wanaishi India kusini.

Tanbihi hariri

  1. Testamentum Domini, ed. by Ephrem Rahmani, Life of Severus of Antioch, sixth century.

Marejeo hariri

 
Undani wa kanisa la Mt. Stefano huko Gütersloh, Ulaya.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Antiokia kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.