Saint Vincent na Grenadini

(Elekezwa kutoka Saint Vincent na Grenadines)

Saint Vincent na Grenadini ni nchi ya visiwani ya Antili Ndogo katika bahari ya Karibi. Iko kaskazini kwa Grenada na Trinidad na Tobago na kusini kwa Saint Lucia.

Saint Vincent na Grenadini
Ramani ya St. Vincent na Grenadini

Saint Vincent ndiyo kisiwa kikubwa na Grenadini ni kundi la visiwa vidogo. Kwa jumla eneo la nchi kavu ni kilometa mraba 389.

Mji mkuu wa Kingstown, huko St. Vincent.

Watu hariri

Wakazi wengi wana asili ya Afrika (66%) au ni machotara (19%). 6% ni Wahindi, 4% Wazungu (hasa wenye asili ya Ureno) na 2% Waindio ambao ndio wenyeji wa Karibi.

Lugha rasmi ni Kiingereza, lakini wananchi wengi wanaongea kwa kawaida Krioli

Upande wa dini, walio wengi (88.6%) ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, kuanzia Waanglikana na Wapentekoste, halafu Wamethodisti, Waadventista Wasabato, Wabaptisti na Wakatoliki. Wahindu ni 3.4%, Warastafari 1.8%, Baha'i 1.6, Waislamu 1.5% n.k.

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Bahari ya Karibi bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Saint Vincent na Grenadini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.