Televisheni

(Elekezwa kutoka TV)

Televisheni (kifupi: TV) au runinga ni chombo (kifaa) chenye skrini (kioo) ambacho kinapokea mawasiliano kutoka kituo cha televisheni na kuyabadilisha kuwa picha na sauti.

TV ya Kijerumani ya mwaka wa 1956.

Neno "televisheni" linatokana na maneno mawili: tele (kutoka Kigiriki: kwa mbali sana) na visio (kutoka Kilatini: mwono; kwa pamoja yanaunda neno la Kiingereza television lililotoholewa katika Kiswahili televisheni.

Historia ya televisheni

 
TV Braun HF 1 ya Kijerumani ya mwaka wa 1959.

Kwa kawaida TV inaonekana kama sanduku. TV za zamani kabisa zilikuwa zina kirimba au fremu kubwa ya mbao na zilikuwa zikiwekwa chini kama fanicha. TV za kisasa ziko za namna nyingi kama zilivyo nyingi zaidi. Kuna baadhi ya TV zinaweza kuenea mkononi mwako zikawa zinaendeshwa kwa kutumia betri. TV nyingine zinaweza kuenea ukuta mzima wa nyumba, na inaweza kukaa katika sakafu, au kuna nyingine ambazo zimenyooka (flat) na zinaweza kubandikwa ukutani.

Televisheni inaweza kuonyesha picha kutoka sehemu mbalimbali. Cha kwanza unachotakiwa kufanya ni kutumia kidaka mawasiliano au antena (au aerial), hii itaonyesha yale yote yanayorushwa na kituo cha matangazo ya televisheni.

Vituo vya TV vinaweza kuwa mbali kabisa lakini bado matangazo yake yanapatikana kama antena ya kurusha mawimbi yake iko katika umbali wa kilomita 50 hadi 150. Teknolojia mpya zaidi ni kutumia vyombo vya angani kama antena ya kurusha mawimbi haya duniani. TV pia inaweza kuonyesha filamu kutoka VCD na DVD au VCR yaani tepu za kawaida. Cable TV na Satellite TV zinaweza zikatoa huduma nyingi za vipindi vya TV kwa mara moja na vilevile kuvirusha hewani. Michezo mingi ya video huunganishwa katika TV ili uweze kuona kile unachokicheza. Kuna baadhi ya tarakilishi au kompyuta ambazo unaweza kutumia TV kama kioo cha kufanyia kazi zako (skrini, au kwa jina lingine monita). TV za kisasa (TV janja, kwa Kiingereza: Smart TV) zina uwezo wa kutumia intaneti moja kwa moja.

TV zote zina skrini ambayo inaonyesha picha. Kabla ya miaka ya 1970 TV zilikuwa hazina rangi (yaani zilikuwa "black and white" tu), ambazo zilikuwa zinafanya kila kitu kionekane cha rangi ya kijivu. Lakini kwa sasa karibuni TV zote zinaonyesha na rangi. Kawaida ya viwambo vingi (kioo au vioo) huonyesha kuwa vina kona ya mzunguko, lakini kwa sasa vioo vingi hutengenzwa kwa kunyooka na zina ncha pembeni.

 
Njia ya picha katika TV

Kabla ya miaka ya 1990, TV zote zilikuwa zikitengenezwa kwa umbo moja - zilikuwa kubwa kidogo na kisha zilikuwa ndefu. Kwa mfano, kama kioo kilikuwa cha urefu wa inchi 3, basi lazima kitakuwa na upana wa inchi 4. Au kama kioo kina urefu wa cm 30, lazima kitakuwa kina upana wa cm 40.

Umbo la TV za kisasa linazidi kuwa maarufu na kupata wapenzi wengi zaidi kila siku ziendapo. TV zenye kioo cha upana mkubwa wa mstatili huonekana vizuri katika runinga kubwa (theatre screen) na pia inapendeza wengi zaidi. Hizi huziita kioo kipana (widescreen). Endapo TV ya kioo kipana ina urefu wa cm 30, basi lazima itakuwa ina upana wa cm 53. Ili ifanye kazi vizuri, uonyeshaji wa TV pia unatakiwa ujengwe kwa namna ya upana yaani 'widescreen'. Kioo kipana kinaweza kubadilishika kwa ukubwa wowote unaoutaka, lakini suala la umbo linabaki kuwa vilevile kama lilivyo (widescreen).

Televisheni Afrika

Chaneli Nchi Lugha Mwanzo Tovuti
Al Jazeera Kiarabu Live Stream http://oklivetv.com/al-jazeera-documentary-live/
RTPAFRICA Kongo Kireno 2016 http://www.rtp.pt/play/direto/rtpafrica
Africa Black Tv Eacu Kiswahili, Kiarabu, Pijini, Camfrancangle (FR), Kireno 2017

[1]

VOXAFRICA Kamerun Camfrangle 2018 http://www.africawebtv.com/vox-africa/
lc2 International Nigeria
NTV2 Benin
BeTV Burundi Kirundi, Kiswahili, Ufaransa 2017 http://www.betvburundi.com

Viungo vya nje

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: