Peloponesi

(Elekezwa kutoka Peloponnese)

Peloponesi (Kigiriki Πελοπόννησος peloponesos) ni rasi ya kusini mwa Ugiriki. Imeunganika na sehemu ya bara ya nchi kwa shingo la nchi kwenye mji wa Korintho.

Peloponesi katika Ugiriki

Jina la kihistoria la rasi lilikuwa Morea (Μωριάς morias).

Eneo lote la Peloponesi ni kilomita za mraba 21,549. Kuna watu 1,155,000 walioishi huko mwaka 2011.

Peninsula imegawanywa kati ya mikoa mitatu ya kiutawala: sehemu kubwa ni ya mkoa wa Peloponesi, na sehemu ndogo ni za mkoa wa Ugiriki Magharibi na wa Attica.

Jiografia hariri

 
Shingo la nchi la Korintho, mji wa Korintho ukiwa upande wa kushoto, mstari nyoofu wa Mfereji wa Korintho katikati ya picha

Ghuba ya Korintho inatenganisha Peloponesi na Ugiriki bara.

Rasi hiyo ina milima mingi na pwani yenye hori ndefu zinazoingia ndani ya nchi. Mlima mrefu ni Taygetos unaofikia mita 2,407 juu ya UB. Rasi yote inakabiliwa na mitetemeko ya ardhi ya mara kwa mara.

Mji mkubwa zaidi ni Patras yenye wakazi 170,000.

Miji hariri

Miji mikubwa zaidi ya kisasa kwenye Peloponesi ni (sensa ya 2011):

Historia hariri

 
Lango la Simba huko Mikene (Mycenae).
 
Hekalu la Hera, Olimpia.

Rasi hii iliona vipindi na watendaji muhimu katika historia ya Ugiriki ya Kale.

Marejeo hariri

  1. Stamatoyannopoulos, George et al., Genetics of the Peloponnesian populations and the theory of extinction of the medieval Peloponnesian Greeks, European Journal of Human Genetics, 25.5 (2017), pp. 637–645
  2. Bées & Savvides (1993), p. 239
  3. Richard Clogg (20 June 2002). A Concise History of Greece. Cambridge University Press. ku. 35–42. ISBN 978-0-521-00479-4.  Check date values in: |date= (help)

 

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

  Peloponesi travel guide kutoka Wikisafiri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Ugiriki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Peloponesi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.