Petro Favre (kwa Kifaransa Pierre Favre au Pierre Lefevre; Villaret, Savoie, leo nchini Ufaransa, 13 Aprili 1506 - Roma, Italia, 1 Agosti 1546) alikuwa padri wa kwanza na mwanzilishi mwenza wa Shirika la Yesu pamoja na Ignas wa Loyola na Fransisko Saveri.

Mt. Petro Favre alivyochorwa.

Kwa utiifu alitimiza majukumu mazito katika sehemu mbalimbali za Ulaya, akafariki akiwa anajiandaa kwenda Italia Kaskazini kushiriki mtaguso mkuu wa Trento[1].

Alitangazwa na Papa Pius IX kuwa mwenye heri tarehe 5 Septemba 1872, halafu Papa Fransisko alimtangaza mtakatifu tarehe 17 Desemba 2013[2].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/90923
  2. "It's official: Jesuit Fr. Peter Faber is a saint", National Catholic Reporter, 17 December 2013. Retrieved on 4 October 2014. Archived from the original on 2016-03-16. 
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • William V. Bangert, To the Other Towns: A Life of Blessed Peter Favre, First Companion of St. Ignatius Loyola (Ignatius Press, 2002)

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.