Saksonia (pia Saxony. Kijerumani Sachsen, Kisorbia Sakska; jina rasmi Freistaat Sachsen ("Dola Huru la Saksonia") ni moja ya majimbo 16 ya kujitawala ya Ujerumani lenye wakazi 4,173,000 kwenye eneo la 18 415 km². Mji mkuu ni Dresden, mji mkubwa Leipzig. Waziri mkuu ni Michael Kretschmer (CDU). Jimbo liko katika mashariki ya nchi likipakana na Ucheki na Poland. Saksonia ni dola la kale ndani ya Ujerumani, wakati wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani ilifutwa kati ya 1952 hadi 1990 na kugawiwa kwa mikoa mbalimbali.

Uwanja wa timu ya Leipzig ulioko Saksonia
Mahali pa Saksonia katika Ujerumani
bendera ya Saksonia

Jiografia hariri

Saxonia iko mpakani wa Ujerumani na Poland upande wa mashariki na Ucheki upande wa kusini. Majimbo jirani ndani ya Ujerumani ni Brandenburg upande wa kaskazini, Saksonia-Anhalt, Thuringia na Bavaria upanda wa magharibi. Sehemu kubwa ya mpaka wa kusini inapita kwenye safu ya milima ya Erzgebirge.

Maeneo ya kaskazini ni tambarare hasa beseni ya Leipzig. Kusini kuna kanda ya milima inayofikia mita 1215 juu ya UB kwenye Fichtelberg katika Erzgebirge (milima ya madini).

Mto mkubwa ni Elbe unaopita jimbo lote likipitika kwa meli za mtoni.

Miji hariri

Mji Wilaya Wakazi
31 Desemba 2000
Wakazi
31 Desemba 2006
Wakazi
30 Juni 2008
Leipzig Leipzig (jiji) 493,208 506,260 511,676
Dresden Dresden (jiji) 477,807 504,635 508,398
Chemnitz Chemnitz (jiji) 259,246 245,739 244,310
Zwickau Zwickau (wilaya) 103,008 96,878 95,322
Plauen Vogtlandkreis (wilaya) 71,543 68,317 67,309
Görlitz Görlitz (wilaya) 61,599 57,201 56,608
Hoyerswerda Bautzen (wilaya) 50,203 41,515 39,835
Freiberg Mittelsachsen (wilaya) 45,428 42,772 42,120
Bautzen Bautzen (wilaya) 43,353 41,766 41,354
Pirna Sächsische Schweiz-Osterzgebirge (wilaya) 42,108 39,748 39,291
Freital Sächsische Schweiz-Osterzgebirge (wilaya) 40,129 39,059 39,139
Riesa Riesa-Großenhain (wilaya) 39,367 36,145 35,139
Radebeul Meißen (wilaya) 32,246 33,205 33,284
Meißen Meißen (wilaya) 29,398 28,091 27,846
Limbach-Oberfrohna Zwickau (wilaya) 27,552 26,591 26,113
Zittau Görlitz (wilaya) 27,454 24,892 29,093
Glauchau Zwickau (wilaya) 27,285 25,744 25,159
Delitzsch¹ Nordsachsen (wilaya) 26,331 27,448 27,111
Weißwasser/O.L. Görlitz (wilaya) 26,107 21,797 20,298
Werdau Zwickau (wilaya) 26,077 23,976 23,565
Annaberg-Buchholz Erzgebirgskreis (wilaya) 24,495 22,817 22,514
Coswig Meißen (wilaya) 24,035 22,365 22,514
Reichenbach im Vogtland Vogtlandkreis (wilaya) 23,469 22,164 21,210
Crimmitschau Zwickau (wilaya) 23,305 22,330 21,684
Markkleeberg Leipzig (wilaya) 23,157 23,718 23,962
Döbeln Mittelsachsen (wilaya) 23,128 21,356 20,726
Schwarzenberg/Erzgeb. Erzgebirgskreis (wilaya) 20,201 18,517 19,187
Auerbach Vogtlandkreis (wilaya) 20,042 21,246 20,620
Borna Leipzig (wilaya) 20,010 22,657 21,539

Utawala hariri

Saksonia ina mikoa 3 (Chemnitz, Dresden na Leipzig) zenye wilaya 10:

(Alama za magari kwa kila wilaya katika mabano)

  1. Bautzen (BZ)
  2. Erzgebirgskreis (ERZ)
  3. Leipzig (L)
  4. Meißen (MEI)
  5. Mittelsachsen (FG)
  6. Görlitz (GR)
  7. Nordsachsen (TDO)
  8. Sächsische Schweiz-Osterzgebirge (PIR)
  9. Vogtlandkreis (V)
  10. Zwickau (Z)
 
Districts of Saxony

Majiji hariri

Saksonia ina majiji matatu (katika Ujerumani ila mji mwenye wakazi zaidi ya 100,000 inahesabiwa kma jiji) yenye cheo cha wilaya:

Historia hariri

Leo hii "Saksonia" ni jina la maeneo kwenye pande zote mbili za mto Elbe unapopita kwenye milima ya Erzgebirge mpakani wa Ucheki. Kiasili jina la "Saksonia" ilitaja maeneo ya kaskazini ya Ujerumani walipoishi Wasaksonia ambayo leo hii huitwa "Saksonia ya chini" (Niedersachsen). Cheo cha watemi wa Saksonia kilirithiwa na watawala wa Meißen katika karne ya 15 na tangu wakati ule nchi yao ilianza kuitwa "Sachsen"; kwa uda mrefu Wajerumani walitofautisha kati ya "Saksonia ya Juu" (= Saksonia ya leo) na "Saksonia ya Chini".

Maeneo ya Saksonia ya leo yalikaliwa na makabila ya Kijerumani upande wa magharibi na makabila ya Kislavoni walioitwa "Wasorbi" upande wa mashariki. Polepole Waslavoni wengi walianza kutumia lugha ya Kijerumani lakini hadi leo kuna vijiji kadhaa vyenye wasemaji wengi wa Kisorbi kwa jumla hawazidi watu 20,000.

Saksonia iliweza kutetea cheo chake kama dola la kujitegemea katika historia ya Ujerumani iliyoona harakati ya maeneo madogo kumezwa na madola makubwa zaidi. Wakati wa matengenezo ya kiprotestanti Saksonia ilichagua dhehebu la kilutheri kama dini rasmi.

Mtemi Friedrich August I wa Saksonia ((1670 - 1733) alichaguliwa kuwa pia mfalme wa Poland kwa jina la August II. Alipamba mji mkuu wa Dresden kwa majengo mazuri yaliyounda sifa ya mji kuwa "Firenze kwenye mto Elbe" (Kijerumani: Elbflorenz). Hata mwana wake aliweza kutawala kama mtemi wa Saksonia na mfalme wa Poland lakini baadaye dola likashuka tena cheo kuwa moja ya madola ya Kijerumani ya wastani yaliyojaribu kuhifadhi uhuru wao kati ya madola makubwa Austria na Prussia.

Wakati wa vita za Napoleoni Saksonia ilipambana dhidi ya Mfaransa pamoja na Prussia lakini baada ya kushindwa ikahamia upande wa Naoleoni ikapewa naye cheo cha ufalme. Cheo hiki kilithebitishwa kwenye mkutano wa Vienna mwaka 1815. Hadi 1870 Saksonia ilikuwa ufalme ndani ya Shirikisho la Ujerumani, baadaye ndani ya Dola la Ujerumani.

Mwaka 1918 Saksonia liona mapinduzi sawa na sehemu nyingine za Ujerumani, mfalme wa mwisho akapinduliwa na jamhuri ya "Dola Huru la Saksonia" ikatangzwa kama jimbo ndani ya Jamhuri ya Dola la Ujerumani. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia Ujerumani uliawiwa kati ya nchi washindi na Saksonia ilikuwa sehemu ya kanda la Kisovyeti na tangu 1949 sehemu ya Jamhuri ya ya Kidemokrasia ya Kijerumani (Ujerumani ya Mashariki) chini ya utawala wa kikomunisti. 1952 serikali ilifuta muundo wa majimbo Saksonia ikagawiwa kwa mikoa mbalimbali. Wakati wa kuporomoka kwa utawala wa kikomunisti majibo ya awali yaliundwa upya mwaka 1990 na mwaka uleule Saksonia pamoja na majimbo megine ya mashariki ikajiunga na Jamhuri la Shirikisho la Ujerumani katika maungano ya Ujerumani.

Demografia hariri

Mabadiliko ya idadi ya wakazi katika Saksonia tangu 1905:

Mwaka Wakazi
1905 4,508,601
1946 5,558,566
1950 5,682,802
1964 5,463,571
1970 5,419,187
1981 5,152,857
1990 4,764,301
1995 4,566,603
Mwaka Wakazi
2000 4,425,581
2001 4,384,192
2002 4,349,659
2003 4,321,437
2004 4,296,284
2005 4,273,754
2006 4,249,774
2007 4,220,200
2008 4,192,700

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:



 
Majimbo ya Ujerumani
 
Baden-WürttembergBavaria (Bayern)BerlinBrandenburgBremenHamburgHesse (Hessen)Mecklenburg-Pomerini Magharibi (Mecklenburg-Vorpommern)Saksonia Chini (Niedersachsen)Rhine Kaskazini-Westfalia (Nordrhein-Westfalen)Rhine-Palatino (Rheinland-Pfalz)Saar (Saarland)Saksonia (Sachsen)Saksonia-Anhalt (Sachsen-Anhalt)Schleswig-HolsteinThuringia (Thüringen)