Addai, kwa Kiaramu ܐܕܝ,[1] ni mtakatifu anayeheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo, hasa wa Mashariki, ingawa hakuna makubaliano ya wanahistoria kuhusu maisha yake.

Addai katika picha takatifu ya monasteri ya Mt. Katerina kwenye mlima Sinai, Misri.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Masimulizi juu yake hariri

Kadiri ya mapokeo, hasa ya kitabu Mafundisho ya Addai, alikuwa Myahudi mzaliwa wa Edessa, wakati ule sehemu ya Syria, siku hizi nchini Uturuki.

Alipokwenda kuhiji Yerusalemu, alimsikiliza Yohane Mbatizaji na kubatizwa naye katika mto Yordani, akabaki Palestina.

Baadaye akawa mfuasi wa Yesu, akachaguliwa naye kati ya wanafunzi 70 kwenda kuhubiri wawiliwawili.

Baada ya ufufuko wa Yesu na Pentekoste ya mwaka uleule, Addai alianza kuhubiri Injili huko Mesopotamia, Syria na Persia.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Agosti, pamoja na mwanafunzi wake Mari.

Hata leo inatumika anafora yenye majina yao isiyo na simulizi la Karamu ya mwisho, tofauti na nyingine zote.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Charles George Herbermann, The Catholic Encyclopedia (Universal Knowledge Foundation, 1913), p. 136.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.