Goma

mji katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo


Goma ni mji mkuu wa Mkoa wa Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Uko katika pwani ya Kaskazini ya Ziwa Kivu na ni mpaka na mji wa Gisenyi katika nchi ya Rwanda.

Goma
Goma is located in Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Goma
Goma

Mahali pa mji wa Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Majiranukta: 1°41′0″S 29°14′0″E / 1.68333°S 29.23333°E / -1.68333; 29.23333
Nchi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mkoa Kivu Kaskazini
Wilaya Goma
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 670,000[1]
Muonekano wa Mji wa Goma na Mlima Nyiragongo mnamo mwaka 2015

Idadi ya wakazi wake ni takriban 670,000[1].

Hali ya hewa hariri

Mji wa Goma una hali ya hewa ya kitropiki ya savanna kulingana na Mfumo wa hali ya hewa wa Köppen-Geiger. Majira ya mvua ya masika huanza mwezi Machi hadi mwezi Juni. Na viwango vya joto huwa ishirini na tano Celsius mwaka mzima.

Historia hariri

Goma iliathiriwa sana na Mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka wa 1994. Watu wa kabila la Watutsi na Wahutu hata wapiganaji wa Kihutu walihama kwenye miji ambayo iko karibu na Ziwa Kivu. Kulikuwa na takriban wakimbizi laki nane katika mji wa Goma baada ya mauaji hayo[2]. Watu wengi waliumwa na kufa kwa sababu ya kuharisha, kipindupindu na malaria. Ukosefu wa chakula, maji na mahitaji ya maisha ulisababisha ugonjwa na mapambano katika makambi ya wakimbizi.

Vita vya kwanza vya Kongo vilitokea mwaka wa 1997 kati ya jeshi la Rwanda na wapiganaji wa Kihutu katika mji wa Goma. Baadaye, vita vya pili vya Kongo vilitokea baina ya nchi nyingi za kandokando ya Kongo.

Mji wa Goma uliharibiwa sana kwa sababu ya vita hivyo viwili.

Uchumi hariri

Uchumi wa mji wa Goma umepanda tangu M23, ambayo ni kikundi cha waasi, ilipoondoka mji huo. Wafanyabiashara, kama Ahraham Kazadi na Vanessa Jados, wameleta madadiliko makubwa kwa watu wa Goma[3]. Amani ni muhimu kwa maendeleo ya uchumi kila mahali. Goma ina migodi mingi na iko karibu na Ziwa Kivu, hivyo, bila shaka, itakuwa na maendeleo kama itakuwa na amani.

Usafiri hariri

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Goma hutoa ndege za ndani na, tangu mwaka 2016, ulianza kutoa huduma za Kimataifa.

Barabara ndani ya Goma zilikuwa mbaya kwa sababu ya mlipuko wa volkano mwaka wa 2002. Baadaye, njia nyingi zimejengwa upya tangu mwaka 2011, hasa kwa kutumia wakandarasi wa China na mji huu unarekebishwa aidha na wakandarasi wa umma au binafsi[4].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu maeneo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Goma kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.