Nikaragua (pia Nikaragwa) ni nchi ya Amerika ya Kati yenye wakazi 6,071,045 (2012). Imepakana na Honduras na Kosta Rika; upande wa magharibi ni pwani ya Pasifiki na upande wa mashariki kuna pwani ya Bahari ya Karibi.

Nikaragua
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
12°9′ N 86°16′ W
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY
Ramani ya Nikaragua

Jina la nchi linasemekana kuwa mchanganyiko wa jina la wakazi asilia walioitwa "Nikarao" na neno la Kihispania la "agua" (=maji) kutokana na maziwa makubwa mawili nchini yanayoitwa Lago Managua na Lago Nicaragua. Maelezo mengine yanamtaja chifu wa wazalendo wakati wa kufika kwa Wahispania aliyeitwa "Nikarao".

Jiografia hariri

Nikaragua ina volkeno nyingi; nyororo ya milima ya kivolkeno hufuata mstari wa pwani ya Pasifiki.

Sehemu ya juu ni mlima Mogoton wenye kimo cha mita 2,438 juu ya UB.

Maziwa makubwa mawili ya maji matamu ni Lago Managua na Lago Nicaragua.

Eneo upande wa Karibi lina wakazi wachache sana: ni hasa eneo la misitu minene.

Historia hariri

Nchi ilikuwa koloni la Hispania tangu mwaka 1524.

Mwaka 1821 iliachana na utawala wa Hispania pamoja na nchi jirani na kuingia katika Shirikisho la Amerika ya Kati.

Tangu mwaka 1854 imekuwa nchi ya kujitegemea kabisa.

Wakazi hariri

Wakazi walio wengi sana hukalia maeneo ya mji mkuu Managua na pwani ya Pasifiki.

Sehemu kubwa (69 %) ni machotara kati ya wakazi asilia na Wazungu. 7% ni Wazungu. 9% wana asili ya Afrika, wakikaa hasa kwenye pwani Ya Bahari ya Karibi. Waindio ni asilimia 5.

Lugha rasmi na kubwa zaidi ni Kihispania, lakini si lugha pekee.

Upande wa dini, walio wengi ni Wakatoliki (61.5% kadiri ya sensa ya mwaka 2005) na Waprotestanti (30.6%). 15.1% hawana dini yoyote.

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Taarifa za jumla
Sanaa na utamaduni
Mengineyo
  Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika ya Kati bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Nikaragua kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Coordinates: 13°N 85°W / 13°N 85°W / 13; -85