Papa Anastasio I

(Elekezwa kutoka Papa Anastasius I)

Papa Anastasio I alikuwa Papa kuanzia tarehe 27 Novemba 399 hadi kifo chake tarehe 19 Desemba 401[1]. Alitokea Roma, Italia. Baba yake aliitwa Maximus.

Papa Anastasio I.

Alimfuata Papa Siricius akafuatwa na mwanae Papa Inosenti I, aliyemzaa kabla hajapadrishwa, jambo la pekee katika historia ya Kanisa[2].

Alilaani mafundisho kadhaa ya Origen na kuhimiza Wakristo wa Afrika Kaskazini wapinge Udonato.

Alikuwa rafiki wa Augustino wa Hippo, Jeromu na Paulino wa Nola. Jeromu alimsifu kama mtu mwenye utakatifu mkubwa na tajiri sana katika ufukara wake[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Desemba[4].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Sant' Innocenzo I su santiebeati.it.
  3.   Campbell, Thomas (1907). "Pope St. Anastasius I". Catholic Encyclopedia. 1. New York: Robert Appleton Company.
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Anastasio I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.