Sanamu ya Askari au Askari Monument ni sanamu iliyopo penye kitovu cha jiji la Dar es Salaam mahali ambapo mitaa ya Samora na Azikiwe (zamani: Maktaba) zinakutana.

Sanamu ya askari, Dar es Salaam.
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Sanamu inamwonyesha askari Mwafrika katika sare ya kijeshi ya King's African Rifles wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914-1918) akishika bunduki yenye kisu cha kando na kutazama upande wa bahari.

Sanamu hiyo ni moja kati ya tatu zilizochongwa huko London na mchongaji James Alexander Stevenson kama kumbukumbu ya askari na wapagazi Waafrika waliopiga vita hivyo katika Afrika ya Mashariki hasa kati ya Uingereza na Ujerumani ambao wengi wao walikufa. Zilipelekwa Nairobi, Mombasa na Dar es Salaam[1].

Sanamu ya Dar es Salaam ilisimamishwa kwenye mwaka 1927. Chini yake pana maandishi ya kumbukumbu kwa Kiingereza na Kiswahili kilichoandikwa kwa herufi za Kiarabu na pia kwa herufi za Kilatini. Ni kati ya mifano michache ambako mwandiko wa Kiswahili kwa herufi za Kiarabu unaonekana hadharani.

Maneno yake kwa Kiswahili (kwa herufi za Kiarabu na Kilatini) ni kama yafuatayo:

"Huu ni ukumbusho wa askari Waafrika wenyeji waliopigana katika Vita Kuu na ni ukumbusho pia kwa wapagazi ambao walikuwa miguu na mikono ya majeshi. Ni ukumbusho pia kwa watu wote waliotumika wakafa kwa ajili ya mfalme na nchi yao katika Afrika ya Mashariki kwenye Vita Kuu toka mwaka 1914 mpaka 1918 . Ukipigania nchi yako ujapo umekufa watoto wako watalikumbuka jina lako."

Sanamu ya Askari ilichukua nafasi ya sanamu ya Wissmann iliyosimamishwa hapohapo mwaka 1909 kwa kumbukumbu ya meja Hermann von Wissmann, gavana wa pili wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani; sanamu hiyo ilibomolewa na Waingereza walipoteka mji katika mwaka 1916.

Picha hariri

Marejeo hariri

  1. Where are the Africans, the missing ˜"feet and hands" of the army of the First World War?, taarifa ya gazeti Standard, Nairobi ya 02.12.2018, iliangaliwa Aprili 2020