Jumamosi kuu

(Elekezwa kutoka Jumamosi Kuu)

Jumamosi kuu ni siku ya Juma kuu inayoadhimisha hasa pumziko la mwili wa Yesu Kristo kaburini na roho yake kushukia kuzimu kabla ya kufufuka kwa utukufu usiku wa kuamkia Jumapili ya Pasaka.

Sanamu maarufu ya Pietà ya Michelangelo iliyochongwa katika marumaru kumuonyesha Bikira Maria akipakata maiti ya mwanae Yesu mara baada ya kifo chake msalabani.
Picha takatifu ya Jumamosi Kuu na Takatifu, ikimuonyesha Yesu Kushukia kuzimu.

Tarehe yake inabadilikabadilika kila mwaka na hata mwaka uleule ni tofauti katika madhehebu ya Ukristo, hasa yanayofuata mapokeo ya mashariki na yale yanayofuata mapokeo ya magharibi.

Siku hiyo Misa na sakramenti mbalimbali haziadhimishwi kwa kuwa wafuasi wa Yesu wanatulia kimya wakitafakari matukio ya Ijumaa kuu na kujiandaa washangilie ufufuko wake kuanzia kesha la Pasaka hadi Jumapili ya Pentekoste siku 50 baadaye.

Majina katika lugha mbalimbali hariri

Jumamosi kuu inaitwa kwa namna tofauti katika lugha mbalimbali. Baadhi ya mifano ni kama ifuatavyo:

Lugha Jina Tafsiri
Kicheki Bílá sobota Jumamosi nyeupe
Kifaransa Samedi saint Jumamosi takatifu
Kihispania Sábado Santo Jumamosi takatifu
Kiholanzi Stille Zaterdag Jumamosi ya kimya
Kihungaria Nagyszombat Jumamosi kuu
Kiingereza Holy Saturday Jumamosi takatifu
Kiitalia Sabato Santo Jumamosi takatifu
Kijapani 聖土曜日 (Sei Doyoobi) Jumamosi takatifu
Kijerumani Karsamstag Jumamosi ya ombolezo
Kipolandi Wielka Sobota Jumamosi kuu
Kislovakia Biela sobota Jumamosi nyeupe

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jumamosi kuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.