Msaada wa Wakristo

Msaada wa Wakristo (kwa Kilatini: Auxilium Christianorum) ni sifa mojawapo ya Bikira Maria katika Kanisa Katoliki.

Maria Msaada wa Wakristo alivyochorwa na Tommaso Lorenzone, kwa agizo la Yohane Bosco, 1867 hivi, Torino.
Patakatifu pa Maria Ausiliatrice huko Torino, palipoanzishwa na padri Yohane Bosco. Juu ya kuba kuna sanamu ya Maria Msaada wa Wakristo.

Yohane Krisostomo alikuwa wa kwanza kutumia jina hilo mwaka 345.

Baadaye, Ukristo ulipoatharishwa na uenezi wa Waislamu, waumini walimkimbilia Maria kwa jina hilo ili kupata msaada wa sala zake. Hasa mwaka 1571, Waturuki walipokaribia kuteka Ulaya, Papa Pius V aliombea jeshi la Kikristo kwa kuagiza sala ya Rozari hadi ushindi ulipopatikana katika mapigano ya Lepanto.

Yohane Bosco ndiye aliyeeneza zaidi heshima hiyo.

Mtaguso wa pili wa Vatikano, katika hati juu ya Kanisa (61, 62), ulitaja jina hilo ukieleza umama wa Maria[1].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Mei.

Katika sanaa hariri

Tanbihi hariri

  1. In an utterly singular way she co-operated by her obedience, faith, hope and burning charity in the Saviour's work of restoring supernatural life to souls. For this reason she is a mother to us in the order of grace…By her maternal charity, Mary cares for the brethren of her Son who still wander through this world in the midst of dangers and difficulties until they are led to the happiness of their heavenly home". Daniel, Michael. "Our Lady Help of Christians"

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: