Yosefu (babu)
Yosefu (kwa Kiebrania יוֹסֵף, Yossef au Yôsēp̄; kwa Kiarabu, kwa mfano katika Qur'an, jina hilo linaandikwa يوسف, Yūsuf) ni jina la mtoto wa kiume wa kumi na mmoja wa Yakobo Israeli na babu wa kabila mojawapo la Israeli lililoitwa kwa jina lake mwenyewe, au kwa kawaida zaidi liligawanyika pande mbili: kabila la Manase na kabila la Efraimu kufuatana na majina ya watoto wake wawili wa kiume.

Tangu kale anaheshimiwa na baadhi ya Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 4 Septemba, lakini pia 26 Mei na 31 Julai.
Katika Kitabu cha Mwanzo Edit
Kama kawaida ya mitara, kulikuwa na upendeleo na wivu kati ya watoto wa Yakobo. Hasa Yosefu alichukiwa na kaka zake wote 10, ingawa alikuwa mnyofu hata kuwasimulia ndoto zake za ajabu (Mwa 37:2-11).
Kijicho na chuki vilifikia hatua ya kuwafanya watamani kumuua. Walipopata nafasi walifanya njama, ingawa si wote. Mwisho uamuzi ukawa kumuacha hai lakini kumuuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara walioelekea Misri (Mwa 37:12-36).
Lakini katika maovu ya binadamu Mungu akazidi kulishughulikia taifa lake teule. Hivyo Yosefu akawa mfano wa Yesu ambaye alichukiwa bure tu, akauawa msalabani kwa wokovu wa wadogo zake wakosefu.
Mwa 39 inaonyesha jinsi Yosefu alivyozidi kumtiii Mungu na kukwepa dhambi. Hivyo baada ya majaribu mbalimbali akatukuzwa kuwa liwali wa Farao kwa nchi yote, hasa kwa usimamizi wa akiba ya chakula (Mwa 41:1-49) kwa ajili ya miaka saba ya njaa aliyotabiri itafuata.
Kadiri ya mpango wa Mungu njaa hiyo ikawalazimisha kaka zake waje kumuinamia, naye hakulipa kisasi; halafu, kama vile alivyotafsiri ndoto mbalimbali, aliwafafanulia maana ya matukio ya maisha yao katika mpango wa Mungu: kwamba ndiye aliyemtuma Misri kusudi awaokoe (Mwa 45:1-15).
Mwa 46:1-7 inasimulia Yakobo na wazawa wake wote, jumla wanaume 70, walivyohamia Misri. Lakini hawakusahau nchi waliyoahidiwa na Mungu: ndiyo sababu Yakobo na Yosefu walidai waapiwe kuwa watakuja kuzikwa kwao (Mwa 49:29-50:26).
Kabla ya kufa Yakobo aliwabariki watoto wake 12, akiwemo wa mwisho wao (Benyamini), na kwa namna ya pekee Yuda ambaye atatawala moja kwa moja (Mwa 49:8-12).
Katika Kurani Edit
Yosefu ("Yusufu") anahesabiwa na Waislamu kama nabii (Qur'an, sura vi. 84, xl. 34), na kati ya manabii wote, habari za maisha yake tu zinachukua sura nzima Yusufu (sura) (sura xii.).
Tazama pia Edit
Tanbihi Edit
Marejeo Edit
- de Hoop, Raymond (1999). Genesis 49 in its literary and historical context, Oudtestamentische studiën, Oudtestamentisch Werkgezelschap in Nederland 39. BRILL. ISBN 978-90-04-10913-1.
- (2001) The Bible Unearthed: Archaeology's New Vision of Ancient Israel and the Origin of Sacred Texts. Simon and Schuster. ISBN 978-0-7432-2338-6. Retrieved on 11 September 2011.
- Goldman, Shalom (1995). The wiles of women/the wiles of men: Joseph and Potiphar's wife in ancient Near Eastern, Jewish, and Islamic folklore. SUNY Press. ISBN 978-0-7914-2683-8.
- Louden, Bruce (2011). "The Odyssey and the myth of Joseph; Autolykos and Jacob", Homer's Odyssey and the Near East. Cambridge University Press, 57–104. ISBN 978-0-521-76820-7.
- (2011) Biblical History and Israel's Past: The Changing Study of the Bible and History. Wm. B. Eerdmans Publishing. ISBN 978-0-8028-6260-0.
- Redford, Donald B. (1970). A study of the biblical story of Joseph: (Genesis 37–50), Supplements to Vetus Testamentum 20. Leiden: Brill.
- Redford, Donald B. [1992] (1993). Egypt, Canaan, and Israel in Ancient Times. Princeton University Press. ISBN 978-0-691-00086-2.
- Rivka, Ulmer (2009). Egyptian cultural icons in Midrash, Studia Judaica 52. Walter de Gruyter. ISBN 978-3-11-022392-7. Retrieved on 8 September 2011.
- Schenke, Hans-Martin (1967). "Jacobsbrunnen-Josephsgrab-Sychar. Topographische Untersuchungen und Erwägungen in der Perspektive von Joh. 4,5.6". Zeitschrift des Deutschen Palästina-Vereins 84 (2): 159–184.
- Sills, Deborah (1997). "Strange Bedfellows: Politics and Narrative in Philo", The seductiveness of Jewish myth: challenge or response?, SUNY series in Judaica. SUNY, 171–190. ISBN 978-0-7914-3602-8. Retrieved on 8 September 2011.
- Smith, Morton (1984). "Jewish religious life in the Persian period", The Cambridge History of Judaism: Introduction; The Persian period, SUNY series in Judaica. Cambridge University Press, 219–278. ISBN 978-0-521-21880-1. Retrieved on 8 September 2011.
- Sperling, S. David (2003). The Original Torah: The Political Intent of the Bible's Writers. NYU Press. ISBN 978-0-8147-9833-1. Retrieved on 8 September 2011.
- Völter, Daniel (1909). Aegypten und die Bibel: die Urgeschichte Israels im Licht der aegyptischen Mythologie, 4th, Leiden: E.J. Brill. Retrieved on 8 September 2011.
Viungo vya nje Edit
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Yosefu (babu) kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |