Justin mfiadini

(Elekezwa kutoka Yustino mfiadini)

Justin (pia Yustino Shahidi; Kiing. Justin Martyr; alizaliwa Flavia Neapolis, leo Nablus, Palestina, 103 hivi - Roma, Italia, kati ya 162 na 168) alikuwa mwanafalsafa ambaye, kisha kuongokea hekima halisi katika ukweli wa Yesu, aliishika katika mwenendo wa maisha yake, aliifundisha chuoni, akieneza na kutetea Ukristo hata kwa maandishi maarufu, na hatimaye akakamilisha ushahidi wake kwa kuuawa katika dhuluma ya kaisari Marko Aureli wa Dola la Roma.

Picha takatifu ya Kirusi ya Mt. Justin.

Ni kwamba, baada ya kumpatia kaisari huyo utetezi wa Wakristo, alitolewa kwa mtawala Rusticus akakiri imani mbele yake na kwa ajili hiyo aliuawa pamoja na wanafunzi wake sita (Karitoni, Karito, Evelpisto, Gerasi, Peoni na Liberiani) [1].

Hati za mateso yao zimetunzwa hadi leo[2].

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Walutheri na Waanglikana kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Juni[3].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

 
Iustini opera, 1636

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.