Mlipuko wa virusi vya corona 2019-20

(Elekezwa kutoka Covid-19)

Mlipuko wa Virusi vya Korona (kwa Kiingereza: Coronavirus) ulibainika rasmi tarehe za katikati za mwezi Desemba mwaka 2019 katika mji wa Wuhan huko China ya kati. Ulikuwa kikundi cha watu wenye nimonia bila chanzo kinachoeleweka. Ulibanika baadaye kama aina mpya ya virusi vya korona.[1][2][3][4]

Mlipuko wa Virusi vya Korona duniani.
Ukomeshaji uenezi wa viini.

Tarehe 20 Januari 2020 Waziri Mkuu wa Uchina Li Keqiang alitoa wito wa kutia juhudi katika kukomesha na kudhibiti janga la nimonia lililosababishwa na virusi vya korona.[5] Kufikia tarehe 23 Machi, 2020, kesi 337,000 zimethibitishwa,[6]

Kufikia tarehe 5 Februari 2020, vifo 493 vilitokana na virusi hivyo tangu kifo cha kwanza kilichothibitishwa Januari 9, na watu 990 waliopona. [7] Kifo cha kwanza nje ya Uchina kiliripotiwa tarehe 1 Februari nchini Ufilipino, kilikuwa ni kifo cha mwanamume wa Kichina mwenye umri wa miaka 44.

Kumekuwa na majaribio ambayo yameonyesha kesi zaidi ya 6000 zilizothibitishwa nchini Uchina, ambazo baadhi zao ni za wafanyakazi wa huduma ya afya.[8]

Katikati ya Februari 2020 maswali mengi kuhusu virusi hivi vilibaki bila jibu, lakini Shirika la Afya Duniani lilitoa tathmini kuwa[9]

  • zaidi ya asilimia 80 za wagonjwa huonekana kuwa na ugonjwa mwepesi, wanapona
  • kati ya asilimia za wagonjwa kuna maambukizi mazito yanayosababisha matatizo ya kupumua, hata nimonia, na asilimia 15 kudai walazwe hospitalini
  • takriban asilimia 5 huwa na magonjwa hatari
  • mnamo asilimia 2 hufa; hatari ya kifo inapatikana hasa kwa wazee, kuna mfano michache ya watoto. Baadaye imeonekana kwamba kiwango cha vifo si kubwa vile, labda kati ya % 0.5 hadi 1 lakini si rahisi kutaja kiwango kwa uhakika kwa sababu wengi walioambukizwa hawajulikani.
  • utafiti wa ziada bado unahitajika
  • kuna dalili kwamba virusi vya Covid-19 vinaweza kudumu hadi siku 8 kwenye uso wa kitu kilichoguswa na mgonjwa na bado kusababisha maambukizi

Kufikia tarehe 11 Julai 2020, zaidi ya watu milioni 12.5 walithibitishwa kupatwa na COVID‑19 katika nchi na maeneo 188 duniani kote. Kati yao waliofariki ni zaidi ya 560,000 na waliopona ni zaidi ya milioni 6.89.

Kufikia tarehe 15 Aprili 2022, WHO ilitangaza kuwa walitohibitishwa kuambukizwa ni 500.186.525, na kati yao 6.190.349 wamefariki, Marekani ikiwa nchi iliyoathiriwa zaidi (79.71 milioni walioambukizwa na 979.321 waliofariki, karibu 16% ya jumla ya dunia nzima), ikifuatwa na India (zaidi ya maambukizi milioni 43, na vifo 521.737) na Brazil (zaidi ya maambukizi milioni 30, na vifo 661.493).

Historia hariri

Kuna nadharia kadhaa kuhusu kesi ya kwanza ilitoka lini. Kwa mujibu ya ripoti ya serikali ya Uchina isiyochapishwa, kesi ya kwanza inaweza kufuatiliwa mnamo 17 Novemba 2019; mtu huyo alikuwa raia wa jimbo la Hubei wenye miaka 55. Kulikuwa na wanaume wanne na wanawake watano walioripotiwa kuambukizwa mwezi Novemba, lakini wao wote si kesi ya kwanza. Kuanzia mwezi Desemba, idadi ya kesi huko Hubei iliongezeka pole pole, kufikia 60 mnamo 20 Desemba na angalau 266 mnamo 31 Desemba. Kwa mujibu ya vyanzo rasmi vya Kichina, nyingi za kesi hazikuunganishwa na soko la samaki, lililouza wanyama hai. Mwezi Mei 2020, George Gao, Mkurugenzi wa kituo cha Kichina kwa ajili ya kudhibiti na kuzuia magonjwa (CDC), alisema sampuli za wanyama zilizokusanyika sokoni humo zilipima hasi kwa virusi hivyo, kuonyesha kwamba ingawa soko lilikuwa chanzo cha kesi nyingi, halikuwa chanzo cha mlipuko wa kwanza. [10] [11] [12]

Mnamo 24 Desemba, hospitali kuu ya Wuhan ilitumia maabara ya Vision sampuli. Tarehe 27 na 28 Desemba, Vision ilitoa taarifa hospitali hiyo na CDC ya kichina, ikionyesha virusi vipya. Kundi la nimonia yenye sababu isiyojulikana liliangaliwa tarehe 26 Desemba na kutibiwa na daktari Zhang Jixian katika hospitali Hubei Provincial, na aliambia Wuhan CDC tarehe 27 Desemba juu ya kundi hilo. Tarehe 30 Desemba, ripoti ya kupima iliyotumia hospitali ya Wuhan kutoka maabara CapitalBio Medlab iliripoti matokeo ya chanya kwa SARS, lakini hayo hayakuwa sahihi, iligunduliwa baadaye.[13] [14]

Ripoti hiyo ilisababisha kundi la madaktari katika hospitali ya Wuhan Central kutoa tahadhari kwa wenzao na mamlaka ya hospitali juu ya matokeo. Jioni hiyo, Tume ya afya ya Wuhan ilitoa taarifa taasisi mbalimbali za afya juu ya "matibabu ya nimonia yenye sababu isiyojulikana". Manane wa madaktari hao, wakiwemo Li Wenliang, baadaye walionywa na polisi kwa kueneza “uvumi wa uongo,” na mwengine, Ai Fen, alikemewa na wakuu wake kwa kupiga king’ora .Serikali ya Uchina iliwaadhibu Ai Fen, Li Wengliang, na madaktari wengine ambao walijaribu kuonya umma mwezi Desemba kuhusu virusi hivyo. Li Wengliang alikufa kutokana na COVID-19 tarehe 7 Februari. Hospitali zote nchini ziliweka chini ya utawala wa chama cha kikomunist mwaka 2018 [15] [16]

Tume ya afya ya Wuhan ilitangaza habari za ugonjwa wa mapafu wenye sababu isiyojulikana tarehe 31 Desemba, na kuthibitisha kesi 27 — kutosha ili kuanzisha uchunguzi. [17] Wakati wa awamu za mapema za mlipuko, idadi ya kesi iliongezeka mara mbili kila siku saba na nusu. [18]Mnamo mwanzo na katikati ya Januari 2020, virusi vilienea hadi mikoa mingine ya Kichina, kusaidiwa na uhamiaji kuhusu siku kuu ya mwaka mpya ya kichina kwa sababu Wuhan ni kitovu kikubwa cha usafiri. [19]Tarehe 20 Januari, Uchina iliripoti kesi mpya karibu na 140 kwa siku moja, zikiwemo watu wawili mjini Beijing na mmoja huko Shenzhen.[20] Baadaye takwimu rasmi zilionyesha watu 6,174 tayari wameshakuwa na dalili, na watu zaidi huenda waliambukizwa.[21] Ripoti ya Lancet tarehe 24 Januari iliashiria maambukizo miongoni mwa binadamu, ilipendekeza sana vifaa vya kinga binafsi kwa wafanyakazi wa afya, na kusema kupima kwa virusi kulikuwa muhimu kutokana na "uwezekano wa janga".[22] Tarehe 30 Januari, shirika la WHO lilitangaza Coronavirus vilikuwa dharura ya afya ya kimataifa. [23]

Tarehe 31 Januari 2020, Italia ilikuwa na kesi zake za kwanza zilizothibitishwa, watalii wawili waliotoka Uchina. Kuanzia tarehe 13 Machi 2020, shirika la WHO lilizingatia Ulaya kama katikati ya janga.[24] Tarehe 19 Machi 2020, Italia ilipitisha Uchina kama nchi yenye vifo vingi zaidi. Tarehe 26 Machi, Marekani ilipitisha Uchina na Italia kama nchi yenye idadi kubwa zaidi ya kesi zilizothibitishwa duniani.[25] Utafiti unaonyesha kesi nyingi zaidi mjini New York zilitoka wasafiri wanaotoka Ulaya, badala ya kutoka Uchina au nchi nyingine za Asia.[26] Upimaji upya wa sampuli zilizokusanyika mapema uligundua mtu mmoja nchini Ufaransa ambaye alikuwa na virusi tarehe 27 Desemba 2019 na mtu mmoja huko Marekani ambaye alikufa kutokana na COVID-19 tarehe 6 Februari 2020. [27] [28]

Zaidi ya nchi 120 zimeunga mkono uchunguzi wa asili ya mlipuko wa COVID-19. Mwanzoni Uchina ilipambana na juhudi zao na ilitisha kulipiza kisasi cha kiuchumi kwa nchi zilizotoa mwito huu. Lakini mnamo Mei Uchina hatimaye ilikubali kushirikiana na uchunguzi huo. [29]

Mnamo 11 Septemba 2020, zaidi ya kesi milioni 28.2 zimeripotiwa kote duniani; zaidi ya watu 910,000 wamekufa na zaidi ya watu milioni 19 wamepona.[30]

Uenezi wa Covid-19 nje ya China hariri

 
Uenezi wa virusi vya SARS-Covid-19 duniani (ramani inasahihishwa kila siku)
Idadi ya watu waliothibitishwa kuwa na maambukizi
      zaidi ya 10,000       1,000–9,999       100–999       10–99       1–9 (Tarehe 16 Machi mtu wa kwanza alipatikana nchini Tanzania)
 
Mlipuko wa Virusi vya Corona duniani hadi 2 Machi 2020.

Hadi mwisho wa Januari 2020 takriban watu 10,000 waliambukizwa, idadi ya vifo ilikuwa mnamo 200. Virusi vilienea hadi nchi nyingine kwa njia ya abiria wa ndege za kimataifa. Wakazi wa Wuhan na miji mingine ya China yenye wagonjwa wamekataliwa kuondoka kwao baada ya hali ya karantini kutangazwa.[31].

Maambukizi ya kwanza ya ndani ya virusi hivi nje ya Uchina yalitokea Vietnam kati ya wanafamilia,[32] wakati maambukizi ya kwanza ya ndani ambayo hayakuhusisha familia yalitokea Ujerumani, tarehe 22 Januari, wakati mwanamume mmoja wa Kijerumani alipata ugonjwa huo kutoka kwa mgeni wa China kwenye kikao cha biashara.[33]

Kesi nyingine zilizothibitishwa mapema ziliripotiwa huko Thailand, Korea Kusini, Japani, Taiwani, Makau, Hong Kong, Marekani (Everett, Washington na Chicago),[8] Singapore, [34] Vietnam, Ufaransa[35], Italia na Nepali.

Katika Februari 2019 virusi viliendelea kuenea nje ya China, kupitia watu waliosafiri baina ya China na nchi nyingine. Tabia ya virusi kutosababisha ugonjwa mkali kwa wengi ilikuwa msingi kwa uenezaji usiotambuliwa mwanzoni hadi kufikia watu waliogonjeka vibaya. Milipuko ya kwanza ilionekana katika Iran[36], Korea Kusini[37] na Italia[38] ambako serikali zilitangaza hali ya karantini kwa maeneo kadhaa. Kufikia mwisho wa mwezi huo, wagonjwa wa nchi nyingine kwa pamoja walikuwa wamezidi wale wa China.

Katika Machi 2020 idadi ya maambukizi mapya ilipungua nchini China na Korea Kusini lakini iliongezeka Ulaya na kuanza kusambaa Marekani. Katika Ulaya Italia ilikuwa nchi iliyoathiriwa vibaya zaidi; serikali ilifunga shule zote pamoja na maduka yasiyo ya chakulas na dawa na kupiga marufuku mikusanyiko yote, ikiwemo ile ya ibada. Hatua kama hizo zilichukuliwa pia katika nchi nyingine. Katika Asia ya Magharibi nchi iliyoathiriwa vibaya zaidi ni Iran.

Kwa jumla si rahisi kupata picha kamili ya uenezi halisi wa virusi hivi. Ilhali dalili za ugonjwa zinafanana na mafua ya kawaida na kifua kikuu, inawezekana mara nyingi maambukizi hayakutambuliwa. Kwa sababu hiyo makadirio ya asilimia ya watu wanaokufa yanatofautiana kati ya nchi na nchi.

Tarehe 11 Machi 2020 Shirika la Afya Duniani ilitamka uenezi wa virusi umefikia ngazi ya pandemia, yaani epidemia (mlipuko) katika nchi nyingi za dunia[39].

Katikati ya mwezi Machi 2020 idadi ya wagonjwa iliongezeka sana katika nchi za Ulaya. Marekani ilizuia wasafiri kutoka Ulaya kuingia. Nchi mbalimbali, pamoja na Ujerumani, zilianza kufunga shule na kukataza mikutano yote yaliyolenga zaidi ya watu 100-500, kwa hiyo kufunga mechi za mpira wa miguu au michezo mingine, pamoja na hoteli na sinema. Kampuni mbalimbali ziliamuru wafanyakazi kukaa nyumbani na kutekeleza shughuli kupitia kompyuta pekee. Tarehe 14 Machi Denmark na Poland zilifunga mipaka kwa wote wasio raia wao, kwa kuamuru raia waliorudi wapaswe kukaa karantini wiki 2.

Kwa jumla serikali zilitangaza kwamba asilimia kubwa ya wananchi wataambukizwa zikiona changamoto kuchelewesha mchakato wa maambukizi ili wale wataokuwa wagonjwa sana wasijitokeze mara moja lakini polepole ili waweze kuhudumiwa hospitalini.

Kufikia tarehe 19 Machi nchi 170 zilikuwa na mgonjwa walau mmoja.

Tarehe 21 Machi Italia ilikuwa imezidi China kwa wingi wa vifo, kwa kuwa siku hiyo walifariki huko watu 793, kuliko siku yoyote ya China.

Kufikia tarehe 23 Machi jumla ya waliothibitishwa kupatwa na virusi ilifikia 339,645 na vifo 14,717 kati nchi zaidi ya 40.

Takwimu za tarehe 27 Machi zinaonyesha waliopatwa kwa hakika ni walau 536,000 na kati yao walau 24,100 wamekufa kwa ugonjwa huo. Idadi kubwa ya walioambukizwa nchi kwa nchi imekuwa ile ya Marekani.

Kufikia tarehe 13 Aprili walioambukizwa walifikia 1,850,000 na waliofariki dunia 114,000.

Kufikia tarehe 2 Juni walioambukizwa walifikia 6,325,303 na waliofariki dunia 377,469.

Hadi tarehe 11 Juni walioambukizwa walifikia kuwa zaidi ya 7,360,000 na waliofariki dunia 416,000.

Afrika hariri

Mwanzoni mwa Machi 2020 hakukuwa na taarifa ya maambukizi mengi ndani ya Afrika. Wataalamu walijadiliana kama hilo ni jambo linalotokana na kukosa vifaa vya kupima na kutambua ugonjwa, au kama kuna sababu ya ugonjwa kutoenea katika Afrika. Wagonjwa wengi waliotambuliwa kusini kwa Sahara ni wasafiri waliofika kutoka nchi za nje.

Hadi 12 Machi wagonjwa walithibitishwa hasa katika Afrika Kaskazini: Misri wagonjwa 67 (1 alifariki), Algeria 20 (0), Moroko 6 (1) na Tunisia 7 (0). Upande wa kusini wa Sahara taarifa zilipatikana hasa kutoka Afrika Kusini walipotambulia wagonjwa 17 (0), wengi wao watu waliorudi kutoka safari za Italia. Togo ilikuwa na mgonjwa 1 (0) aliyethibitishwa, Senegal 4 (0), Nigeria 2 (0), Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo 1 (0), Kamerun 2 (0), Burkina Faso 2 (0)[40]

Tarehe 15 Machi jioni mtu wa kwanza alithibitishwa Tanzania ameambukizwa; msafiri aliyeleta virusi vya ugonjwa huo ni mwananchi aliyefika Arusha kutoka Ubelgiji na ambaye baadaye alipona. Hadi tarehe 30 idadi rasmi ilifikia waambukizwa 19.[41] Wengi waliambukizwa nje ya nchi wakagundulika baada ya kufika Tanzania. Tarehe 31 Machi 2020 Mtanzania wa kwanza alifariki huko Dar es Salaam. Waliobaki na virusi ni watu 17 kwa mujibu wa Waziri wa Afya[42].

Kenya kulikuwa na maambukizi 31 na kifo cha kwanza.

Hadi tarehe 13 Aprili katika Afrika Bara nchi pekee isiyothibitisha maambukizi ilikuwa Lesotho, mbali ya Sahara Magharibi na visiwa mbalimbali, kama Komoro.

Kufikia tarehe 2 Juni walioambukizwa walifikia 152,442 na waliofariki dunia 4,344 katika nchi 54.

Majibu ya kitaifa hariri

Jumla ya nchi na maeneo 188 yamekuwa na angalau kesi moja ya COVID-19 hadi sasa. Kutokana na janga la Ulaya, nchi nyingi katika eneo la Schengen zimezuia harakati huru na kuweka udhibiti wa mipaka. Majibu ya kitaifa yamejumuisha maagizo ya kukaa nyumbani au ufungaji. [43] [30]

Hadi 26 Machi, watu 1,700,000,000 duniani kote walikuwa chini ya aina ya ufungaji, idadi ambayo iliongezeka hadi watu 3,900,000,000 mnamo wiki ya kwanza ya mwezi Aprili-zaidi ya nusu ya idadi ya watu duniani. [44]

Kufikia mwisho wa mwezi Aprili, watu takriban 300,000,000 walikuwa chini ya maagizo hayo katika mataifa ya Ulaya, zikiwemo Italia, Uhispania, Ufaransa, na Uingereza, wakati watu wapatao 200,000,000 walikuwa chini ya ufungaji katika Amerika Kusini. Watu takriban 300,000,000, au asilimia 90 ya idadi ya watu, walikuwa chini ya aina fulani ya ufungaji katika Marekani, watu 100,000,000 huko Ufilipino, watu 59,000,000 nchini Afrika Kusini, na watu 1,300,000,000 wamekuwa chini ya ufungaji nchini India. Mnamo 21 Mei maambukizo 100,000 mapya yalitokea duniani kote, na tangu mwanzo wa janga hilo. Mnamo Augosti kumekuwa na zaidi ya kesi 26,000,000 duniani. [45][46]

Asia hariri

Tarehe 19 Mei 2020, kesi zimeripotiwa nchini kote kwa Asia isipokuwa Turkmenistan na Korea Kaskazini, ingawa pengine nchi hizi zina kesi pia. [47] [48]Licha kuwa eneo la kwanza duniani lililoathiriwa na mlipuko huo, itikio ya mapema ya baadhi ya mataifa ya Asia, hasa Korea Kusini, Taiwan, na Vietnam, imeziruhusu kufanya vizuri kuliko nchi nyingine. [49][50][51][52]

Uchina hariri

Inawezekana kupata asili ya kesi ya kwanza iliyothibitishwa ya COVID19 mnamo 1 Desemba 2019 mjini Wuhan; Ripoti moja isiyothibitishwa inaonyesha kesi ya mapema ilionekana tarehe 17 Novemba.[53] Daktari Zhang Jixian aliona kundi la ugonjwa wa mapafu wenye sababu isiyojulikana tarehe 26 Desemba, ambapo hospitali yake ilitoa taarifa Jianghan CDC tarehe 27 Desemba. Upimaji wa awali wa kijenetiki wa sampuli za wagonjwa tarehe 27 Desemba 2019 walionyesha uwepo wa Coronavirus kama SARS. Ilani ya umma ilitolewa na Tume ya afya ya Wuhan, tarehe 31 Desemba, kuthibitisha kesi 27 na kupendekeza kuvaa barakoa. Shirika la WHO liliambiwa siku hiyo hiyo. Kama taarifa hizi zilitokea, madaktari katika Wuhan walionywa na polisi juu ya "kueneza uvumi" kuhusu mlipuko. Tume ya afya ya Taifa ya Uchina ilisema hakukuwa na "ushahidi wazi" wa usambazaji wa binadamu ingawa madaktari mengi wamaangalia usambazaji huo ulikuwa ukifanyika. Katika mkutano siri tarehe 14 Januari, maafisa wa Uchina walisema kwa faragha kwamba maambukizo ya binadamu kwa binadamu yaliwezekana, na maandalizi ya janga yalihitajika. Katika taarifa iliyotolewa mnamo 14 – 15 Januari, Kamisheni ya afya ya Wuhan ilisema uwezekano wa maambukizo ya binadamu kwa binadamu haukuweza kupuuza. [54] [55]

Tarehe 20 Januari, Tume ya afya ya Taifa ya Uchina ilithibitisha maambukizo ya binadamu kwa binadamu. [56]Siku hiyo hiyo, Katibu Mkuu wa chama cha kikomunisti Xi Jinping na Mkuu wa Baraza la serikali, Li Keqiang, walitoa taarifa zao za kwanza kuhusu virusi, wakisema kwamba wale walioishi maeneo hayo wajitenge, kudumisha ubali wa kijamii, na kuepuka kusafiri.[57] Wakati wa kipindi cha kusafiri kuhusu mwaka mpya wa kichina, mamlaka za nchi ziliagiza ufungaji wa mji wa Wuhan. [58]Tarehe 10 Februari serikali ya Uchina ilizindua kampeni kali sana iliyoelezwa na kiongozi mkuu na Katibu Mkuu wa chama cha kikomunisti Xi kama "vita vya watu" ili nchi hiyo idhibiti virusi.[59] Katika "karantini kubwa zaidi katika historia ya binadamu", tarehe 23 Januari usafiri wote kuingia na kuondoka mjini Wuhan ulisimamishwa na baadaye marufuku hizo zilipanuliwa kwa miji kumi na mitano jimboni Hubei kuathiri watu 57,000,000. [60]Matumizi ya gari binafsi yalipigiwa marufuku jijini. Sherehe za mwaka mpya (tarehe 25 Januari) pia zilifutwa. Mamlaka ilitangaza ujenzi wa hospitali ya muda, Huoshenshan, iliyokamilika katika siku kumi. Baadaye Hospitali ya Leishenshan[61] ilijengwa kuwalaza wagonjwa wengine. Uchina pia iligeuka vituo vingine katika Wuhan, kama vile vituo vya maktaba na viwanja, katika hospitali za muda. [62][63]

Tarehe 26 Januari, serikali ilianzisha hatua zaidi za kudhibiti coronavirus, zikiwemo kutoa maazimio ya afya kwa wasafiri na kupanua sikukuu ya tamasha la spring.[64] Vyuo vikuu na shule nchini kote pia zilifungwa. Mikoa ya Hong Kong na Macau ilianzisha hatua kadhaa, hasa kuhusu shule na vyuo vikuu.[65] [66]Hatua za kazi za mbali ziliwekwa katika mikoa kadhaa. Vizuizi vya usafiri vilitekelezwa kuingia na kuondoka jimboni Hubei. Usafiri wa umma ulibadilishwa, na makumbusho kote nchini yalifungwa kwa muda. Udhibiti wa harakati za umma ulifanyika katika miji mingi, na inakadiriwa kuwa watu 760,000,000 (zaidi ya nusu ya watu nchini) walikabiliwa na aina fulani ya kizuizi cha kwenda nje.[67] Mnamo Januari na Februari 2020, wakati wa kilele cha mlipuko katika Wuhan, watu karibu na 5,000,000 walipoteza kazi zao.[68] Wengi wa wafanyakazi wahamiaji takriban 300,000,000 wamekuwa walikwama nyumbani mikoani mbalimbali au jimboni Hubei.

Baada ya mlipuko huo kufikia awamu yake ya kimataifa mwezi Machi, viongozi wa Uchina walichukua hatua kali za kuzuia virusi visingie tena nchini Uchina kutoka nchi nyingine. Kwa mfano, mji wa Beijing iliweka karantini ya siku 14 kwa wasafiri wote wa kimataifa wanaoingia mjini.[69] Wakati huo huo, chuki dhidi ya wageni, hasa waAfrika, iliibuka, na wageni walitendwa vibaya na wananchi na walilazimishwa kuondoka nyumba na hoteli. [70]

Tarehe 24 Machi, Mkuu wa Baraza Li Keqiang aliripoti kwamba kuenea kwa kesi za ndani kumezuiliwa na mlipuko huo umedhibitiwa nchini Uchina. Siku hiyo hiyo vizuizi vya kusafiri vilipunguzwa huko Hubei, isipokuwa mjini Wuhan, miezi miwili baada ya ufungaji ulianza. Wizara ya mambo ya nje ya Uchina ilitangaza tarehe 26 Machi kwamba viza za kuingia au kuishi zilisimimishwa kuanzia tarehe 28 Machi na kuendelea, bila maelezo maalum kuhusu sera hii itakapomalizika. Wale wanaotaka kuingia Uchina lazima waombe viza katika ubalozi wa Uchina au konsulat. Serikali ya Uchina ilitia moyo biashara na viwanda kufunguliwa tena tarehe 30 Machi, na kutoa msaada ya kiuchumi kwa makampuni. [71][72][73]

Baraza la Taifa lilitangaza siku ya maombolezo ya kitaifa kuanza na dakika tatu za kimya tarehe 4 Aprili, ikiunganishwa na tamasha la Qingming, ingawa serikali kuu iliziomba familia kuonyesha heshima mtandaoni ili kuzuia mlipuko mwingine. Tarehe 25 Aprili wagonjwa wa mwisho waliruhusiwa kuondoka hospitalini mjini Wuhan. Mnamo 13 Mei mji wa Jilin uliwekwa kwenye ufungaji, jambo lililochochea hofu ya wimbi la pili la maambukizo.[74]

Wachambuzi wengi wakiwemo wale wanaotoka shirika la Bill Gates wamekosoa Uchina kwa sababu majibu yake yalichelewa. Shirika la Gates limekadiria kwamba kama Uchina imetenda wiki moja mapema zaidi, idadi ya kesi ingepunguka asilimia 66; wiki mbili mapema zaidi, asilimia 86, na wiki tatu mapema zaidi—ambapo mamlaka nchini China iligundua kwamba virusi hivyo vinaweza kuenea binadamu kwa binadamu—idadi ya kesi ingepunguka asilimia 95. [75]

Irani hariri

Iran iliripoti kesi zake za kwanza zilizothibitishwa za COVID-19 tarehe 19 Februari mjini Qom, ambapo, kwa mujibu ya Wizara ya afya na elimu ya matibabu, watu wawili wamekuwa walifariki siku hiyo. [76]Hatua za mapema zilizotangazwa na serikali zikiwemo kufutwa kwa matamasha na matukio mengine ya kitamaduni, matukio ya michezo, maombi ya Ijumaa, na kufungwa kwa vyuo vikuu, taasisi za elimu ya juu, na shule.[77][78] Iran zilitenga pesa 5,000,000,000,000 (sawa na US $120000000) kupambana na virusi.[79] Rais Hassan Rouhani alisema tarehe 26 Februari hakukuwa na mipango kutumia karantini katika maeneo yaliyoathiriwa na mlipuko huo, na watu tu wangejitenga.[80] Mipango ya kupunguza usafiri kati ya miji ilitangazwa mwezi Machi, ingawa trafiki kubwa kati ya miji kuhusu mwaka mpya wa Kiajemi iliendelea.[81] Makaburi wa Shia huko Qom yalibaki kufungua hadi tarehe 16 Machi. [82]

Irani ilikuwa kituo cha usambazaji wa virusi baada ya Uchina mwezi wa Februari.[83] Zaidi ya nchi kumi zilikuwa zimepata asili ya kesi zao huko Iran mnamo 28 Februari, ikionyesha mlipuko huo ulikuwa mkali zaidi kuliko kesi 388 zilizorepotiwa na serikali ya Irani hadi siku hiyo.[84] Bunge la Iran lilifungwa, na wajumbe 23 wa 290 walipima chanya tarehe 3 Machi.[85] Tarehe 15 Machi, serikali ya Irani iliripoti vifo mia katika siku moja, ambayo ilikuwa kesi nyingi zaidi iliyorekodiwa nchini tangu mlipuko ulipoanza.[86] Angalau wanasiasa na maofisa wa serikali kumi na wawili wa sasa au wa zamani walifariki kutokana na ugonjwa huo mnamo 17 Machi. [87]Kufikia 23 Machi, Iran ilikuwa na kesi 50 mpya kila saa na kifo kimoja kipya kila dakika kumi. [88]Kwa mujibu ya ofisa wa WHO, inawezekana kuwa Iran ina kesi mara tano zaidi ya zile zilizoripotiwa. Pia imependekezwa kwamba vikwazo vya Marekani katika Irani viliathiri uwezo wa kifedha wa nchi kukabili mlipuko wa virusi. Shirika la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu limeitisha vikwazo vya kiuchumi vipunguze kwa mataifa yanayoathiriwa zaidi na janga hilo, yakiwemo Irani.[89] Tarehe 20 Aprili iliripotiwa kwamba Irani imefunguliwa maduka makubwa na maeneo mengine ya ununuzi nchini kote, ingawa kuna hofu ya wimbi la pili la maambukizo kutokana na hatua hizi. Mwezi Machi, na tena mwezi Aprili, kulikuwa na taarifa kwamba Irani haikuripoti kesi zote zilizothibitishwa nchini.[90]

Korea Kusini hariri

Kunenea kwa coronavirus hadi Korea Kusini kutoka Uchina kulithibitishwa tarehe 20 Januari 2020. Shirika la afya la Taifa liliripoti ongezeko kubwa la kesi zilizothibitishwa tarehe 20 Februari,[91] kwa kiasi kikubwa kuhusisha mkutano wa Kanisa la Shincheonji wa Yesu mjini Daegu. [92]Wale waliotembelea Shincheonji kutoka Wuhan walituhumiwa kuwa chanzo cha mlipuko. Mnamo 22 Februari, kati ya wafuasi 9,336 wa Kanisa, watu 1,261 au asilimia 13 waliripoti dalili. Korea Kusini ilitangaza kiwango cha juu zaidi cha tahadhari tarehe 23 Februari 2020. Tarehe 28 Februari, zaidi ya kesi 2,000 zilizothibitishwa ziliripotiwa, kuongeza hadi 3,150 tarehe 29 Februari. Vituo vyote vya kijeshi vya Korea Kusini viliwekwa karantini baada ya vipimo vilagundua wanajeshi watatu wenye virusi. Ratiba za ndege pia zilibadilishwa. [93][94]

Korea Kusini ilianzisha ile iliyofikiriwa kuwa programu kubwa zaidi na kupangwa bora duniani ili ipime idadi kwa virusi, kujitenga watu walioambukizwa, na kuwaweka katika karantini wale wanaowasiliana nao.[95] [96]Mbinu za uchunguzi zilijumuisha kujitoa taarifa za lazima za dalili na wasafiri wa kimataifa kutumia simu, kupima kwenye gari na matokeo yanayopatikana siku ijayo, na kuongeza uwezo wa kupima ili watu 20,000 wapimwe kila siku. Mpango wa Korea Kusini unafikiriwa kuwa mafanikio kudhibiti mlipuko bila ufungaji wa miji yote. [97]

Mwanzoni wananchi wa Korea Kusini waligawanyika kuhusu maoni ya majibu ya Rais Moon Jae-in kukabili mgogoro huo, na watu wengi walitia saini ama kusifa serikali hiyo au kutoa wito wa kuiondoa. [98]Tarehe 23 Machi, iliripotiwa kwamba Korea Kusini ilikuwa na idadi ya kesi ndogo zaidi kwa siku moja mnamo wiki nne.[99] Tarehe 29 Machi iliripotiwa kwamba kuanzia tarehe 1 Aprili wale wote waliofika kutoka nchi nyingine wangelazimishwa kukaa karatini kwa wiki mbili. [100]Kwa mujibu ya ripoti za vyombo vya habari tarehe 1 Aprili, Korea Kusini imepokea maombi ya msaada ya kupima virusi kutoka nchi 121 tofauti. [101]Tarehe 15 Mei iliripotiwa kwamba biashara 2000 ziliambiwa kufunga tena ambapo kundi la watu mia moja walioambukizwa liligunduliwa; uchunguzi wa mawasiliano unafanywa kwa watu 11,000. [102]

Ulaya hariri

Kufikia tarehe 13 Machi 2020, idadi ya kesi mpya ilipokuwa kubwa kuliko zile huko Uchina, Shirika la (WHO) walianza kuzingatia Ulaya kama kituo hai cha janga hilo. Kesi kwa nchi kote Ulaya zimeongeza mara mbili kila siku tatu au nne, na baadhi ya nchi zilionyesha ongezeko hilo kila siku mbili. [103][104]

Mnamo 17 Machi, nchi zote za Ulaya zimethibitisha kesi ya COVID-19, na Montenegro kuwa nchi ya mwisho ya Ulaya kutoa taarifa ya angalau kesi moja. Angalau kifo kimoja kimeripotiwa katika nchi zote za Ulaya, isipokuwa mjini Vatican. [105]

Kuanzia tarehe 18 Machi, zaidi ya watu 250,000,000 walikuwepo ufungaji huko Ulaya. [106]

Mnamo 24 Mei, siku 68 tangu kesi yake ya kwanza iliripotiwa, Montenegro ilikuwa nchi ya kwanza bila COVID-19 katika Ulaya. [107]

Tarehe 21 Augosti iliripotiwa kwamba idadi ya kesi za COVID-19 iliongezeka miongoni mwa vijana huko Ulaya.[108]

Italia hariri

Ilithibitishwa kwamba mlipuko huo umeenea hadi Italia tarehe 31 Januari, watalii wawili wa Kichina walipopima chanya kwa SARS-CoV-2 mjini Roma.[109] Kesi zilianza kuongezeka kwa kasi, na serikali ya Italia ilisimamisha safari zote kwenda na kutoka nchini Uchina na kutangaza hali ya dharura.[75] Kundi lingine liligunduliwa baadaye, kuanzia na kesi 16 zilizothibitishwa huko Lombardia tarehe 21 Februari. [110]

Tarehe 22 Februari, Baraza la mawaziri lilitangaza amri mpya ya sheria ili idhibiti mlipuko huo, ikiwemo karantini zaidi ya watu 50,000 kutoka mijini kaskazini ya Italia. [111]Waziri Mkuu Giuseppe Conte alisema, "Katika maeneo ya mlipuko huo, kuingia na kuondoka hakutaruhusiwa. Kusimamishwa kwa shughuli za kazi na matukio ya michezo tayari kumeshaagizwa katika maeneo hayo." [112]

Tarehe 4 Machi, serikali ya Italia iliagiza kufungwa kikamilifu shule zote na vyuo vikuu nchini kote Italia ilipofikia vifo mia moja.[113] Matukio yote makubwa ya michezo yalifanyika bila watazamaji hadi mwezi Aprili, lakini tarehe 9 Machi yote yalisitishwa kabisa kwa angalau mwezi mmoja.[114] Tarehe 11 Machi, Waziri Mkuu wa serikali, aliagiza shughuli za biashara zisimamishwe isipokuwa maduka ya chakula na dawa. [115]

Tarehe 6 Machi, Chuo kikuu cha Italia cha matibabu maalum ilichapisha mapendekezo ya maadili ya matibabu kuhusu jinsi ya kuamua wagonjwa wapi wapate kipaumbele. [116][117]Tarehe 19 Machi, Italia ilipitisha Uchina kama nchi yenye vifo zaidi kutokana na COVID-19 duniani baada ya kutoa taarifa ya vifo 3,405.[118] Tarehe 22 Machi, iliripotiwa kwamba Urusi iliitumia Italia ndege za kijeshi tisa zenye vifaa vya matibabu. [119]Mnamo 9 Mei, kulikuwa na kesi 217,185 zilizothibitishwa, vifo 30,201, na watu 99,023 waliopona nchini Italia, na nyingi za kesi hizo zilitokea mkoani Lombardia. Ripoti ya CNN ilionyesha kwamba mchanganyiko wa idadi kubwa ya wazee na ukosefu wa kupima vilichangia kiwango cha juu cha kifo.[120] Tarehe 19 Aprili, iliripotiwa kwamba nchi hiyo ilikuwa na vifo vichache zaidi vya 433 kwa wiki moja na baadhi ya biashara ziliomba vizuizi vipunguzwe baada ya wiki sita za ufungaji. [121]

Uhispania hariri

Usambazaji wa janga hilo uilithibitishwa hadi Uhispania tarehe 31 Januari 2020, mtalii wa Kijerumani alipopima chanya kwa SARS-CoV-2 huko La Gomera, Visiwa vya Canary. [122]Uchunguzi baada ya muda umeonyesha kwamba angalau aina 15 za virusi zilikuwa zimetambuliwa, na maambukizo ya jamii yalianza mnamo katikati ya mwezi Februari. Mnamo 13 Machi, kesi zilikuwa zimethibitishwa katika majimbo yote 50 nchini. [123]

Ufungaji uliagizwa tarehe 14 Machi 2020. Tarehe 29 Machi ilitangazwa kwamba, kuanzia siku iliyofuata, wafanyakazi wote wasio muhimu waliamriwa wabaki nyumbani kwa siku 14 zijazo. [124]Mwishoni mwezi Machi, Jumuiya ya Madrid imerekodi kesi na vifo vingi zaidi nchini. Wataalamu wa matibabu na wale wanaoishi nyumbani kwa kustaafu wamekuwa walikuwa na viwango vya juu sana vya maambukizo.[125] Mnamo 25 Machi, idadi ya vifo nchini Hispania ilipitisha vifo nchini Uchina, na Italia tu ilikuwa na vifo zaidi. [126]Tarehe 2 Aprili, watu 950 walifariki kutokana na virusi katika kipindi cha masaa 24—wakati huo kulikuwa na zaidi ya vifo katika siku moja kuliko duniani.[127] Mnamo 25 Mei 2020 idadi ya vifo kwa siku iliyotangazwa na serikali ya Kihispania imekuwa chini ya 100 kwa mara ya kwanza katika miezi miwili. [128]

Idadi halisi ya kesi ilifikiriwa kuwa juu zaidi, kwa sababu watu wengi wenye dalili sio kali au wasio na dalili pengine hawakupimwa.[129] Tarehe 13 Mei, matokeo ya wimbi la kwanza la utafiti wa serikali ya Kihispania yalionyesha kuwa asilimia tano ya watu pengine waliambukizwa, au watu takriban 2,000,000, takwimu mara kumi ya idadi ya kesi zilizothibitishwa muda huo. Kulingana na utafiti huu uliohusisha sampuli za zaidi ya watu 63,000, Madrid na Castilla – La Mancha ilikuwa mikoa iliyoathirika zaidi duniani yenye asilimia ya zaidi ya kumi ya maambukizo. Idadi ya vifo halisi pia inaaminika kuwa juu zaidi kutokana na ukosefu wa kupima na kuripoti, labda kwa kesi 12,000 kulingana na Wizara ya Afya ya Kihispania.[130][131]

Uingereza hariri

Kabla ya tarehe 18 Machi 2020, serikali ya Uingereza haikuagiza aina yoyote ya kujitenga kwa kijamii au karantini kwa raia wake. Kwa sababu hiyo serikali ilipokea ukosoaji kwa majibu yake pole pole. [132][133]

Tarehe Machi 16, Waziri Mkuu Boris Johnson alitangaza kushauri dhidi ya usafiri usio muhimu na mawasiliano ya kijamii, na alipendekeza watu wafanye kazi nyumbani inapowezekana na kuepuka mahali kama vile baa, migahawa, na sinema. [134][135]Tarehe 20 Machi, serikali ilitangaza kwamba vituo vyote vya burudani kama vile baa na gym vifungwe karibu iwezekanavyo, na serikali aliahidi kulipa hadi asilimia 80 ya mishahara ya wafanyakazi au hadi £2,500 kwa mwezi kuzuia ukosefu wa ajira wakati wa mgogoro. [136][137]

Tarehe 23 Machi, Waziri Mkuu alitangaza hatua kali zaidi za kujitenga kwa kijamii, kupiga marufuku za mikusanyiko ya zaidi ya watu wawili na kuzuia kusafiri nje nyumbani kwa sababu sio muhimu sana. Tofauti na hatua zilizopita, polisi waliruhusiwa kutoa faini na kueneza mikusanyiko ili watekeleze vizuizi hivyo. Biashara nyingi ziliagizwa kufunga, isipokuwa biashara muhimu sana, kama vile maduka ya chakula na dawa, benki, maduka ya vifaa, vituo vya mafuta, na gereji. [138]

Tarehe 24 Aprili iliripotiwa kwamba majaribio ya chanjo yaliyotia chumvi yameanza nchini Uingereza; Serikali imeahidi zaidi ya paundi 50,000,000 kuunga mkono utafiti huo. [139]

Ili kuhakikisha huduma za afya za Uingereza zilikuwa na uwezo wa kutosha wa kuwatiba watu wenye COVID-19, hospitali za huduma muhimu za muda zilijengwa. [140]Hospitali ya kwanza iliyofunguliwa ilikuwa hospitali ya Nightingale mjini London yenye kitanda 4,000, iliyojengwa ndani ya kituo cha mikutano mikubwa ExCel katika siku tisa.[141] Mnamo 4 Mei, ilitangazwa kuwa hospitali hiyo ingefungwa kwa muda kwa sababu wagonjwa 51 tu walitibwa pale wakati wa wiki tatu za kwanza. [142] [143]Mnamo 5 Mei, takwimu rasmi zilionyesha kwamba Uingereza ilikuwa na kiwango cha kifo kibaya zaidi huko Ulaya, ikianzisha wito wa uchunguzi wa jinsi serikali ilivyosimamia janga hilo. Idadi ya vifo nchini Uingereza ilikuwa karibu 29,427 kwa wale waliopima chanya kwa virusi. Baadaye, ilihesabu kama 32,313, baada ya kujumuisha takwimu rasmi kutoka Scotland na Ireland Kaskazini. Tarehe 16 Aprili iliripotiwa kwamba Uingereza ingekuwa nchi ya kwanza kupata chanjo ya Oxford, kutokana na mkataba wa awali; kama majaribio yangefanikiwa, chanjo 30,000,000 ingepatikana nchini. [144]

Ufaransa hariri

Ingawa ilifikiriwa mwanzo wa janga hilo lilifikia Ufaransa tarehe 24 Januari 2020, wakati huo kesi ya kwanza ya Ulaya ilithibitishwa mjini Bordeaux, baadaye iligunduliwa kwamba mtu karibu na Paris alipima chanya kwa virusi tarehe 27 Desemba 2019 baada ya sampuli za zamani zilipimwa tena.[145][146] Tukio muhimu katika kuenea kwa ugonjwa huo nchini lilikuwa mkutano wa kila mwaka wa Kanisa la Chrisitan Open Door kati ya 17 na 24 Februari mjini Mulhouse, ambao ulihudhuriwa na watu 2,500, angalau nusu ya wale wanaaminika kuambukizwa na virusi hivyo. [147]

Tarehe 13 Machi, Waziri Mkuu Édouard Philippe aliagiza mahali pa umma pasio muhimu pafungwe, na tarehe 16 Machi, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alitangaza watu wote wakae nyumbani, sera ambayo ilipanuliwa angalau hadi 11 Mei.[148] Mnamo 23 Aprili, Ufaransa imeripoti zaidi ya kesi 120,804 zilizothibitishwa, vifo 21,856, na watu 42,088 waliopona, cheo cha nne katika idadi ya kesi zilizothibitishwa. [149]Mwezi Aprili, kulikuwa na ghasia katika sehemu nyingine za Paris.[150] Tarehe 18 Mei iliripotiwa kwamba shule nchini Ufaransa zilibidi zifunge tena baada ya kufunguliwa upya, kutokana na mlipuko mwingine. [151]

Swideni hariri

Swideni ni tofauti kuliko nchi nyingine za Ulaya kwa sababu ilibaki wazi kwa jumla.[152] Kwa mujibu ya katiba ya Kiswidi, Shirika la afya ya umma la Uswidi lina uhuru na hali hiyo inazuia uingiliaji wa kisiasa, na sera ya shirika hilo halikupendelea ufungaji ili nchi ifikie kinga ya umma. Gazeti la New York Times lilisema kwamba, mnamo Mei 2020, mlipuko nchini Swideni umesababisha vifo vingi zaidi lakini haukuathiri uchumi sana kuliko nchi nyingine kwa sababu waSwideni wameendelea kufanya kazi na shughuli. Mnamo 19 Mei, iliripotiwa kwamba nchi hiyo ilikuwa na vifo vingi zaidi kwa idadi ya nchi wakati wa wiki ya tarehe 12 – 19 kuliko Ulaya, vifo 6.25 kwa watu wamilioni moja kwa siku. [153][154][155]

Amerika Kaskazini hariri

Kesi ya kwanza katika Amerika Kaskazini iliripotiwa huko Marekani mwezi Januari 2020. Kesi ziliripotiwa katika nchi zote za Amerika Kaskazini baada ya Saint Kitts na Nevis ilithibitisha kesi tarehe 25 Machi, na katika maeneo yote ya Amerika Kaskazini baada ya Bonai ilithibitisha kesi tarehe 16 Aprili. [156]

Tarehe 26 Machi 2020, Marekani ilikuwa nchi iliyo na idadi kubwa zaidi ya maambukizo, yenye zaidi ya kesi 82,000. Tarehe 11 Aprili 2020, Marekani ilikuwa nchi yenye idadi kubwa ya vifo kutokana na virusi hivyo, vifo 20,000. Mnamo 15 Mei 2020 kulikuwa na kesi 1,571,908 na vifo 95,764 kwa jumla. [157][158]

Kanada iliripoti kesi 60,616 na vifo 3,842 tarehe 4 Mei, wakati Mexico iliripoti kesi 23,471 na vifo 2,154. Jamhuri ya Dominika, Haiti na Cuba ni nchi pekee za nchi za Caribbean ambazo zimeripoti zaidi ya kesi 1,000 (16,908, 2,124 na 2,025, kwa mtiririko huo), wakati Panama na Honduras ziliongoza Amerika ya kati na kesi 7,197 na 1,055, kwa mtiririko huo. [159]

Marekani hariri

Tarehe 20 Januari 2020, kesi ya kwanza inayojulikana ya coronavirus ilithibitishwa jimbo la Washington kuhusu mtu aliyerudi kutoka mjini Wuhan tarehe 15 Januari. Tarehe 31 Januari, utawala wa Rais Trump ulitangaza dharura ya afya ya umma, na kuzuia wasafiri kutoka Uchina wasiingie nchi kama hawakuwa raia. [160][161]

Tarehe 28 Januari, shirika la Vituo Vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) lilitangaza kuwa walitengeneza vifaa vyao vya kupima wenyewe.[162] Lakini Marekani ilianza kupima pole pole, na hali hiyo ilificha kiwango cha mlipuko.[163] Upimaji uliharibiwa na vifaa vya kupima kasoro vilivyozalishwa na serikali mwezi Februari, ukosefu wa kibali cha serikali kutumia vipimo havikuzalishwi na serikali, na vigezo vikali mno vilivyowazuia watu wengi wasipimwe.[164]

Mnamo 2 Machi kulikuwa na kesi 80 zilithibitishwa, na nusu ya kesi ilikuwepo jimbo la California. Majimbo ya Florida na New York yalitangaza kesi mbili zao za kwanza na jimbo la Washington liliripoti kesi nyingi zilizotuhumiwa na kifo cha kwanza. Makamu wa Rais Pence alisisitiza kuwa tishio la virusi kusambaa kote nchini Marekani lilikuwa dogo. [165]

Tarehe 6 Machi, Rais Trump alisaini sheria ya maandalizi na mwitikio ya Coronavirus, ambayo ilitoa fedha za dharura $8,300,000,000 ili mashirika ya serikali yajibu mlipuko huo. Makampuni yaliwahamasisha wafanyakazi wao kufanya kazi kutoka nyumbani. Matukio ya michezo yalifutwa. [166][167]

Tarehe 13 Machi, Trump alitangaza hali ya dharura ya kitaifa, ambayo ilifanya fedha za serikali ziliozopatikana kukabili mgogoro huo. [168]Kuanzia tarehe 15 Machi, biashara na shule nyingi zilifungwa. Mnamo 17 Machi, janga hilo lilikuwa limethibitishwa katika majimbo yote 50 na katika wilaya ya Columbia.[169] [170][171]Mnamo 26 Machi, Marekani ilikuwa na kesi zilizothibitishwa zaidi kuliko nchi nyingine yoyote. [172]Wakaguzi wa afya wa serikali walichunguza hospitali 323 mwishoni mwezi Machi; walitoa taarifa za "upungufu mkubwa sana" wa vifaa vya kupima, "upungufu mkubwa" wa vifaa vya kinga (PPE), na rasilimali nyingine mbaya kutokana na wagonjwa wakikaa hospitali kwa muda mrefu wakati wa kusubiri matokeo ya vipimo. [173]

Tarehe 22 Aprili iliripotiwa kwamba waCalifornia wawili walifariki kutokana na virusi vya COVID-19 tarehe 6 na 17 Februari, wiki tatu kabla ya kifo rasmi cha kwanza nchini kilikiriwa. [174]Mnamo 24 Aprili, kesi 889,309 zilikuwa zimethibitishwa na watu 50,256 walikuwa wamefariki.[175] Mnamo 17 Mei, kwa mujibu ya takwimu za New York Times, zaidi ya watu 1,474,600 walikuwa wameambukizwa na angalau 88,600 walikufa nchini Marekani. Gazeti hilo lilieleza kwamba, kabla ya tarehe 29 Aprili, vifo vilivyothibitishwa kupitia upimaji tu viliripotiwa, lakini vigezo vipya vilijumuisha kesi na vifo vilivyowezekana. Mnamo 17 Mei, Marekani, ambaye ina asilimia 4.25 ya idadi ya watu duniani, ilikuwa na asilimia ya 29 ya vifo kutokana na Coronavirus. [176]

Ikulu imekuwa ilikosolewa kwa kupunguza tisho na kudhibiti habari kwa kuagiza maafisa wa afya na wanasayansi kuratibu taarifa za umma na machapisho yanayohusu virusi pamoja na ofisi ya Makamu wa Rais Mike Pence. Mnamo 14 Aprili, Rais Trump alifuta fedha kwa shirika la afya duniani (WHO), akisema wamekuwa walisimamia vibaya janga hilo. Pia alisema Marekani haingeshiriki katika jitihada za kimataifa pamoja na WHO kuendeleza chanjo na madawa kupambana na virusi. [177][178]

Mnamo katikati ya mwezi Mei ripoti za kesi mpya zilianza kukaa sawa na majimbo mengi yalianza kufungua migahawa na mahali pengine pa biashara, kuweka mipaka ya idadi ya watu walioruhusiwa ndani wakati huo huo. Mkuu wa shirika la magonjwa ya maambukizo (NIAID), Dk Anthony Fauci, alionya kwamba kama tahadhari haikutumika kiwango cha maambukizo kingeongezeka tena na alikuwa na wasiwasi hasa kuhusu kufungua shule kwa mwaka mpya wa shule. Mnam kati kati ya mwezi Juni, idadi ya kesi ilianza kuongezeka tena hasa majimbo ya Texas, California, Florida, na Arizona. [179][180] Tarehe 16 Julai Marekani ilikuwa na kesi zaidi kwa siku moja (kesi 75,000) tangu mwanzo wa mlipuko. [181]

Amerika Kusini hariri

Janga hilo lilithibitishwa kuwa kufika Amerika Kusini tarehe 26 Februari Brazil ilipothibitisha kesi mjini São Paulo. Mnamo 3 Aprili, nchi zote za maeneo ya Amerika Kusini zilikuwa zimeandikisha angalau kesi moja. [182][183]

Mnamo Aprili 17, idadi kubwa zaidi ya wagonjwa na vifo viliandikishwa nchini Brazili, ikifuatiliwa na Peru na Chile katika idadi ya kesi zilizothibitishwa. [184]

Tarehe 13 Mei, iliripotiwa kwamba Amerika Kusini na eneo la Caribbean ziliripoti zaidi ya kesi 400,000 na vifo 23,091. Tarehe 22 Mei, likitaja hasa ongezeko la maambukizo la haraka nchini Brazil, shirika la WHO lilitangaza kwamba Amerika Kusini sasa ni kati ya janga la Coronavirus. Mnamo 25 Mei, eneo hilo lilikuwa na zaidi ya kesi 636,000 na zaidi ya vifo 31,000. Hata hivyo, kutokana na ukosefu wa kupima na vifaa vya matibabu inaaminika kwamba mlipuko huo ni mkubwa zaidi kuliko takwimu rasmi zinaonyesha. [185]

Brazili hariri

Tarehe 20 Aprili iliripotiwa kwamba Brazil ilikuwa na rekodi ya vifo 1,179 kwa siku moja, kwa jumla ya karibu 18,000. Kukiwa na idadi ya kesi takriban 272,000, Brazil ikawa nchi yenye idadi kubwa ya tatu ya kesi, kufuata Urusi na Marekani. Mnamo 25 Mei, Brazil ilizidi idadi ya kesi nchini Urusi iliporipoti kwamba kesi mpya 11,687 zilikuwa zimethibitishwa katika masaa 24 yaliyopita, na kufikia zaidi ya kesi 374,800, na zaidi ya vifo 23,400. Rais Jair Bolsonaro amechochea utata mkubwa akitaja virusi hivyo kama "homa ndogo" na mara nyingi kukosoa hatua za ufungaji na karantini. [186][187]

Afrika hariri

Kwa mujibu ya Michael Yao, ambaye ni mkuu wa operesheni za dharura barani Afrika kwa WHO, kugundua mapema ni muhimu kwa sababu mifumo ya afya ya bara "tayari imeshindwa na milipuko mingi ya ugonjwa unaoendelea". [188] Washauri wanasema kwamba mkakati wenye msingi wa kupima ungeruhusu nchi za Afrika kupunguza ufungaji ambao unaosababisha ugumu mkubwa kwa wale wanaotegemea mapato siku kwa siku ili waweze kuwalisha wenyewe na familia zao. Hata katika hali bora zaidi, shirika la Umoja wa Mataifa linasema kuwa vifaa 74,000,000 vya kupima na vifaa 30,000 vinavyosaadia kupumua vitahitajika na wananchi 1,300,000,000 wa bara mwaka 2020.[189] Kesi nyingi zilizoripotiwa zinatoka nchi sita: Afrika Kusini, Nigeria, Ghana, Morocco, Misri na Algeria, lakini inaaminika kwamba kuna uwezekano mkubwa kuna kesi nyingi zaidi ambazo hazijaripotiwa huko nchi nyingine za Afrika zenye mifumo maskini ya huduma za afya.[190] Kesi zimethibitishwa katika nchi zote za Afrika, na Lesotho ilikuwa nchi ya mwisho kuripoti kesi yake ya kwanza tarehe 13 Mei 2020. Hajakuwa na kesi zilizoripotiwa katika maeneo ya nje ya Uingereza ya Saint Helena, Ascension, na Tristan da Cunha.[191][192]

Oceania hariri

Janga hilo lilithibitishwa kufikia Oceania tarehe 25 Januari 2020 kesi ya kwanza iliyothibitishwa iliporipotiwa mjini Melbourne, Australia. Tangu wakati huo, virusi hivyo vimeenea mahali pengine katika eneo hilo, ingawa mataifa mengi madogo ya Pasifiki hadi sasa yameepuka mlipuko huo kwa kufunga mipaka yao ya kimataifa. Mnamo 13 Agosti 2020, Mataifa ya Oceania rasmi bado hayajaripoti kesi. [193][194]

Tarehe 19 Mei 2020, Australia ilifungua hoja katika Umoja wa Mataifa kudai uchunguzi wa asili ya virusi na miitikio wa Umoja wa Mataifa na serikali mbalimbali. Zaidi ya nchi 100 ziliunga mkono hoja hii, na ilipitishwa mara moja. [195][196]

Miitikio ya kimataifa hariri

Vizuizi vya usafiri hariri

Kutokana na janga hilo, nchi nyingi na maeneo mengi yaliweka karantini, marufuku za kuingia, au vikwazo vingine, ama kwa raia, wasafiri waliosafiri hivi karibuni maeneo yaliyoathirika, au wasafiri wote. Pamoja na upungufu wa hamu la kusafiri, sekta ya usafiri imeathirika vibaya. Kuna wasiwasi kuhusu ufanisi wa vikwazo vya kusafiri ili kuzuia virusi visisambae. Utafiti katika gazeti la Sayansi uligundua kwamba vizuizi vya usafiri vilikuwa na athari ndogo tu kuchelewa usambaji wa awali, isipokuwa vilipojumuisha na hatua nyingine za kuzuia na kudhibiti maambukizo. Watafiti walihitimisha kuwa "vikwazo vya kusafiri ni muhimu zaidi katika awamu za mapema na mwisho za janga" na "vikwazo vya kusafiri kutoka Wuhan kwa bahati mbaya vilifanywa kuchelewa sana". [197][198][199]

Umoja wa Ulaya ilikataa wazo la kusitisha eneo la usafiri la bure la Schengen na kuanzisha udhibiti wa mpaka na Italia, uamuzi ambao umekosolewa na wanasiasa wengine wa Ulaya.[200]

Uhamishaji wa raia wa kigeni hariri

Kutokana na karantini ufanisi wa usafiri wa umma huko Wuhan na Hubei, nchi kadhaa ziliwahamisha raia wao na wafanyakazi wa kidiplomasia kutoka eneo hilo, hasa kwa ndege maalum, na mamlaka ya Uchina kutoa kibali. Kanada, Marekani, Japani, India, Sri Lanka, Australia, Ufaransa, Argentina, Ujerumani, na Thailand zilikuwa miongoni mwa kwanza kupanga uhamishaji wa raia wao. Brazil na New Zealand pia zilihamisha raia wao wenyewe na baadhi ya watu wengine.[201] Tarehe 14 Machi, Afrika Kusini iliwahamisha Waafrika Kusini 112 ambao walipima hasi kwa virusi kutoka Wuhan, wakati watu wanne ambao walionyesha dalili waliachwa nyuma ili ipunguze hatari.[202] Pakistani ilisema isingewahamisha raia kutoka Uchina.[203]

Tarehe 15 Februari, Marekani ilitangaza ingewahamisha Wamarekani kutoka meli ya Diamond Princess,[204] na tarehe 21 Februari, Kanada iliwahamisha abiria wa kiKanada 129 kwenye meli hiyo. Mwanzo wa mwezi Machi, serikali ya India ilianza kuwazuia raia wake wasitoke Irani.[205] Tarehe 20 Machi, Marekani ilianza kuwaondoa wanajeshi wake kutoka Iraki kutokana na janga hilo.[206]

Misaada ya kimataifa hariri

Msaada kwa Uchina hariri

Baadhi ya wanafunzi wa Kichina huko vyuo vikuu Marekani walituma msaada, ukiwemo barakoa N95 50,000 tarehe 30 Januari.[207] Shirika la msaada wa kibinadamu moja kwa moja liliotumia hospitali ya Wuhan barakoa 200,000 na vifaa vingine vya kujilinda binafsi siku hiyo hiyo. [208]Tarehe 5 Februari, Wizara ya mambo ya nje ya Uchina ilisema nchi 21 (zikiwemo Belarus, Pakistan, Trinidad na Tobago, Misri, na Iran) zilikuwa zimetumia Uchina msaada, na Bill na Melinda Gates walitangaza mchango wa $100,000,000 kwa WHO kufadhili utafiti wa chanjo na matibabu na kulinda "watu wenye hatari katika Afrika na Asia Kusini.”[209][210] Interaksyon ilisema serikali ya Uchina ilichangia Ufilipino barakoa 200,000 tarehe 6 Februari baada ya Seneta wa Ufilipino Richard Gordon alitumia Wuhan barakoa 3,160,000. Tarehe 19 Februari, Shirika la Msalaba Mwekundu la Singapore lilitangaza lingetumia Uchina msaada wenye thamani $2,260,000.[211][212]

Nchi kadhaa walichangia Uchina barakoa, vifaa vya matibabu au fedha, zikiwemo Japan, Uturuki, Russia, Malaysia, Ujerumani, na Kanada. [213]Wizara ya Mambo ya Nje Marekani ilisema tarehe 7 Februari imekuwa iliwezesha usafirishaji wa tani karibu 17.8 za za vifaa vya matibabu kwa Uchina. [214]Siku hiyo hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje Marekani Pompeo alitangaza ahadi ya $100,000,000 kwa Uchina na nchi nyingine kusaidia mapambano yao dhidi ya virusi. Makampuni kadhaa pia yamechangia Uchina fedha au vifaa vya matibabu.[215][216]

Msaada kwa dunia hariri

Baada ya kesi nchini Uchina zimetulia, nchi hiyo ilianza kupelekea mataifa mengine msaada.[217] Mwezi Machi, Uchina ilitumia Italia vifaa vya matibabu na wataalamu kusaidia kukabiliana na mlipuko wake Coronavirus; Uchina zilitumia Italia timu tatu za matibabu na kuchangia zaidi ya tani 40 za vifaa vya matibabu. [218]Mfanyabiashara Jack Ma alitumia Ethiopia vifaa vya kupima 1,100,000, barakoa 6,000,000, na suti za kinga 60,000 kwa Umoja wa Afrika. Yeye baadaye alitumia Panama vifaa vya kupima 5,000, barakoa 100,000, na mashini za kupumua tano.[219]

Uholanzi, Uhispania, Uturuki, Georgia, na Jamhuri ya Czech zilitaja wasiwasi juu ya barakoa na vifaa vya kichina. Kwa mfano, Uhispania iliondoa vifaa vya kupima vya kichina 58,000 vyenye kiwango cha usahihi cha asilimia 30, na Uholanzi ilirudisha barakoa 600,000 zilizotuhumiwa kasoro, lakini Uchina ilisema hii ilitokana na matumizi mabaya. Ubelgiji iliondoa barakoa 100,000 ambazo hazikutumika zilizofikiriwa kutoka nchini Uchina lakini kwa kweli kutoka nchini Colombia. Ufilipino imesimamisha kutumia vifaa vya kupima vilivyotolewa na Uchina kutokana na usahihi wao wa asilimia 40. Serikali ya Uchina ilisema maagizo ya bidhaa pengine hayakufuatiliwa, na kwamba baadhi ya bidhaa hazikununuliwa moja kwa moja kutoka makampuni yanayothibitishwa. Msaada wa Kichina ulipokelewa vizuri katika sehemu za Amerika Kusini na Afrika. Tarehe 2 Aprili, Benki ya Dunia ilianzisha shughuli za msaada wa dharura kwa nchi zinazoendelea. Kwa mujibu ya taarifa ya Wizara ya mambo ya nje, Uturuki inatoa kiasi kikubwa cha msaada ya kibinadamu duniani huku ina cheo cha tatu duniani kutoa msaada ya matibabu.[220][221][222][223][224]

Hatua za majibu za WHO hariri

Taiwan ilijulisha WHO kuhusu virusi vipya tarehe 31 Desemba 2019. [225]WHO limeisifu mamlaka za Kichina kwa kutoa "habari mara kwa mara", kuliko mlipuko wa SARS mnamo 2002-2004 Uchina iliposhtakiwa ya usiri.[226] WHO lilieleza tarehe 5 Januari kwamba kesi za ugonjwa wa mapafu wenye sababu isiyojulikana zilikuwa zimeripotiwa, [227]na shirika hilo lilitoa taarifa za kiufundi tarehe 10 na 11 Januari pamoja na onyo ya hatari ya maambukizo ya binadamu na kushauri tahadhari kwa sababu hali hiyo ilifanana na mizuko ya awali ya SARS na MERS.[228] Ingawa katika matangazo ya umma lilisema "Hakuna ushahidi wazi wa maambukizo miongoni mwa binadamu" mnamo 14 January.[229] Tarehe 20 Januari, shirika la WHO lilisema kwamba ilikuwa "sasa ni wazi kabisa" maambukizo miongoni mwa binadamu ya Coronavirus yamekuwa yalitokea, kwa sababu wafanyakazi wa afya walikuwa wameambukizwa.[230] Tarehe 27 Januari, WHO lilisema hatari ya mlipuko ilikuwa "juu katika ngazi ya kimataifa".[231]

Tarehe 30 Januari, WHO lilitangaza mlipuko huo kama dharura ya afya ya umma ya wasiwasi wa kimataifa (PHEIC), likionya "nchi zote zinapaswa kujitayarisha kuchukua hatua za kudhibiti, zikiwemo uangalizi, kugundua mapema, kutenga na kusimamia kwa kesi, kuchunguza mawasiliano na kuzuia usambazaji zaidi,” kufuatia ongozeka la kesi nje ya Uchina.[232] Hiyo ilikuwa PHEIC ya sita daima tangu sera hiyo ilianzishwa mwaka 2009 wakati wa janga la mafua ya nguruwe. Mkurugenzi Mkuu Tedros Adhanom alisema PHEIC inatokana na "hatari ya kuenea kwa kimataifa, hasa kwa nchi zenye kipato cha chini au cha kati bila ya mifumo nguvu ya afya" lakini WHO halikupendekeza “kupunguza biashara na harakati".[233]

Tarehe 11 Februari, WHO lilianzisha jina la COVID-19, na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alikubali kutoa "nguvu ya mfumo mzima wa Umoja wa Mataifa kwa majibu". Timu ya usimamizi wa migogoro ya Umoja wa Mataifa ilianzishwa, kuruhusu uratibu wa Umoja wa Mataifa, ambayo WHO lilisema ingewaruhusu "kuzingatia usaidizi wa afya wakati wa mashirika mengine kufanya kazi kuhusu athari za kiuchumi, kijamii, na manendeleo za mlipuko huo ". [234]Tarehe 25 Februari, WHO lilitangaza "ulimwengu unapaswa ufanye zaidi kujiandaa kwa uwezekano wa janga la COVID-19," na kusema kwamba ingawa ilikuwa mapema mno kuita janga, ilikuwa lazima nchi zifanye “awamu ya maandalizi".[235] Tarehe 28 Februari, maafisa wa WHO walisema madadirio ya tishio ya kimataifa la Coronavirus yangeongeza kutoka “juu” hadi “juu sana,” kiwango chake cha juu ya tahadhari. [236]Tarehe 11 Machi, WHO lilitangaza mlipuko wa Coronavirus ulikuwa janga. Mkurugenzi Mkuu alisema WHO "linajihusisha sana na viwango vya kutisha vya kuenea na ukali, na pia viwango vya kutisha vya kutotenda". [237]Wakosoaji wamesema WHO lilijibu janga hilo vibaya na tangazo la dharura la afya ya umma lilichelewa.[238]

Athari hariri

Uchumi hariri

Mlipuko huo ni tishio kubwa kwa uchumi wa dunia. Agathe Demarais kutoka Economist Intelligence Unit anatarajia kwamba masoko ya fedha yataendelea kutetemeka hadi kuna uwazi zaidi kuhusu matokea yanayowezekana. Makadirio moja ya mtaalamu huko Chuo Kikuu cha Washington mjini St. Louis yalitoa athari ya dola bilioni 300 + kwenye biashara ya kimataifa ambayo ingedumu miaka miwili.[239] Masoko ya hisa duniani yalianguka tarehe 24 Februari kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya kesi nje ya Uchina. [240]Tarehe 27 Februari, kutokana na wasiwasi kuhusu mlipuko wa Coronavirus, soko la hisa la Marekani lilianguka zaidi tangu mwaka 2008, na DOW lilianguka pointi 1,191 (thamani kubwa zaidi katika siku moja tangu mgogoro wa fedha mnamo 2007 – 08) na masoko yote matatu yalimaliza wiki hiyo chini ya asilimia 10. [241][242] Masoko ya hisa yalishuka tena kutokana na hofu ya Coronavirus, kuanguka kubwa zaidi tarehe 16 Machi. Wengi wanadhani kushuka kubwa kwa uchumi kutafanyika.[243]

Benki ya Lloyd ya London inakadiria kuwa sekta ya bima ya kimataifa itakuwa na hasara ya US $204 bilioni, hasara zaidi kuliko majira ya kimbunga cha Atlantiki mwaka 2017 na mashambulio ya kigaidi ya 9/11 mwaka 2001, kuashiria uwezekano wa janga la COVID-19 litakuwa janga baya katika historia ya binadamu.[244]

Utalii ni sekta moja inayoathiriwa vibaya zaidi kutokana na marufuku za usafiri, ufungaji mahali pa umma kama vile vivutio vya kusafiri, na ushauri wa serikali dhidi ya kusafiri. Makampuni ya ndege mbalimbali yamefuta safari, na makampuni madogo ya ndege yameshindwa. Sekta ya meli iliathirika vibaya pia, na vituo vya meli vimefungwa. Posta ya kimataifa kati ya nchi nyingine imesimama au kuchelewa kutokana na kupungua kwa usafiri baina yao au kusimamishwa kwa huduma za ndani.[245][246][247][248]

Sekta ya rejareja imeathiriwa duniani kote, na maduka mengi yamefunga kwa muda au yamepunguza masaa ya biashara. Ziara za wateja katika Ulaya na Amerika Kusini zilianguka kwa asilimia 40. Huko Amerika Kaskazini na Mashariki ya kati wauzaji waliona kushuka kwa asilimia 50-60. Hii pia ilisababisha kushuka kwa trafiki ya miguu kwa asilimia 33-43 vituoni kwa ununuzi mwezi Machi ikilinganishwa na mwezi Februari. Wakurugenzi wa maduka ya biashara duniani kote waliweka hatua za ziada, kama vile kuongezeka kwa usafi, ufungaji wa scanners ili kuangalia joto la wanunuzi, na kufuta matukio.[249][250][251]

Mamia ya mamilioni ya kazi yamepotezwa duniani kote. Zaidi ya Wamarekani 40,000,000 walipoteza kazi zao na kufanya madai ya bima ya ukosefu wa ajira.[252][253]

Kwa mujibu ya makadirio ya Tume ya uchumi ya Umoja wa Mataifa ya Amerika Kusini, kushuka kwa uchumi kutokana na janga kungewalazimisha watu milioni 14-22 katika umaskini kuliko idadi bila janga hilo.[254][255]

Uchumi wa nchi zinazoendelea umeharibu sana hasa nchi za Afrika ambazo zimeshakuwa na deni kubwa sana. Zaidi ya deni ni kiChina na sasa kuna shinikizo kubwa juu ya Uchina kufuta deni hiyo. Shirika la IMF na Benki ya Duniani na nchi za G-20, zikiwemo Uchina, vimekubali kuchelewesha kulipa deni hiyo. Lakini kuna waswasi huko Afrika kwamba Uchina itauliza kulipwa hivi karibuni kwa sababu uchumi wa kiChina pia una matatizo. Wachambuzi wengi wanaamini kwamba pengine Uchina itajaribu kufaidika hali hiyo kwa kuchukua miundo mbinu kwa mfano bandari kama nchi za Afrika hazitaweza kulipa deni. [256][257][258]

Ukosefu wa bidhaa hariri

Mlipuko huo umelaumuliwa kwa uhaba wa ugavi, kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya vifaa vinavyohitajika kupambana na virusi hivyo, kununua bidhaa zaidi zinazohitajika kutokana na hofu, na kuvuruga operesheni za kiwanda na utaritibu wa ugavi. [259]Kuenea kwa kununua kutokana na hofu kumesababishwa na watu wanoamini kwamba kutakuwa na uhaba au tishio fulani, hofu ya mustakubali, au sababu kisaikolojia na kijamii (kwa mfano, ushawishi wa kijamii na uaminifu).[260] Sekta ya teknolojia, hasa, imeonya juu ya ucheleweshaji wa shehena ya bidhaa za elektroniki.[261] Kwa mujibu ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom, mahitaji ya vifaa vya kujilinda binafsi yamefufuka mara mia, na kusababisha bei mara ishirini kuliko bei za kawaida na pia kuchelewa kwa ugavi wa vitu vya matibabu kwa miezi minne hadi sita.[262] Pia imesababisha uhaba wa vifaa vya kinga binafsi duniani kote, na WHO limeonya kwamba hali hiyo itahatarisha wafanyakazi wa afya.[263]

Athari ya mlipuko Coronavirus ilikuwa duniani kote. Virusi vilisababisha uhaba wa kemikali zinazotumika katika kutengenza dawa za fentanyl na methamphetamine. Kundi la Yuancheng, liko Wuhan, Uchina, ni moja ya makampuni yanayosambaza kemikali hizo.[264] Kuongezeka kwa bei na upungufu wa dawa hizi haramu vimeangaliwa mitaani huko Uingereza. Polisi wa Marekani pia waliambia gazeti la New York Post kwamba makundi ya madawa ya kulevya ya kiMexico yanakuwa na changamoto kupata kemikali hizo.[265][266]

Janga hilo limevuruga ugavi wa chakula cha kimataifa na kutishia kusababisha matatizo lipya la chakula. David Beasley, mkuu wa Shirika la chakula duniani (WFP), alisema "Tungekabiliwa na njaa nyingi mnamo miezi michache ijayo."[267][268]

Maafisa wa Umoja wa Mataifa walikadiria mwezi Aprili 2020 kwamba watu wa ziada 130,000,000 wangekufa kutokana na njaa, kwa jumla ya watu 265,000,000 mwishoni 2020.[269]

Mafuta na masoko ya nishati hariri

Mwanzo wa Februari 2020, Shirika la nchi za mafuta (OPEC) lilichochoea baada ya kupungua kwa bei ya mafuta kutokana na mahitaji ya chini kutoka Uchina. Tarehe 20 Aprili, bei ya hisa za West Texas Intermediate (WTI) alianguka chini ya sifuri hadi rekodi ya chini (- $37.63) kutokana na wanaomili hisa wakiziuza. Mwezi Juni bei zilikuweko chini lakini bora, na pipa la WTI liliuzwa $20.[270][271]

Utamaduni hariri

Sekta za sanaa na urithi wa utamaduni zimeathiriwa sana na janga hilo, ambalo limeathiri operesheni za mashirika pamoja na watu — wote walioajiriwa na waliojitegemea — duniani kote. Mashirika ya utamaduni yalijaribu kulinda malengo (mara nyingi inayofadhiliwa kwa umma) ya kutoa huduma za kitamaduni kwa jamii, kulinda usalama wa waajiriwa wao na pia umma, na kuwasaidia wasanii kama iwezekanavyo. Mnamo Machi 2020, kote ulimwenguni, makumbusho, maktaba, na taasisi nyingine za kitamaduni zilikuwa zimefungwa na maonyesho na matukio yao yalifutwa au kuahirishwa. Kulikuwa na juhudi kubwa kutoa huduma mbadala mtandaoni.[272][273][274]

Matukio ya wiki ya Pasaka mjini Roma yalifutwa. Viongozi wengi wamependekeza Wakristo wazee wakae nyumbani badala ya kuhudhuria mikutano ya kidini; mingi yalipatikana kupitia kwa redio, mtandaoni na televisheni, ingawa baadhi ya kanisa imefanya mikutano kwenye magari. Pamoja na Vatican na makanisa ya kikatoliki, makundi ya kidini mengine pia yalifuta mikutano ya umma katika makanisa, misikiti, masinagogi, mahekalu na gurdwaras. Wizara ya afya ya Irani ilitangaza kwamba sala za Ijumaa zilifutwa katika maeneo yaliyoathiriwa na mlipuko na baadaye makaburi yalifungwa pia, na Saudi Arabia ilipiga marufuku wasafiri wa kigeni pamoja na wakazi wake kuingia maeneo matakatifu ya Makka na Medina.[275][276][277]

Janga hilo limesababisha usumbufu mkubwa zaidi kwa kalenda ya michezo duniani kote tangu vita vya dunia ya pili. Matukio makubwa yamekatwa au kuahirishwa, yakiwemo Ligi ya Mabingwa ya UEFA 2019-20, Ligi Kuu 2019-20, UEFA Euro 2020, msimu wa NBA 2019-20, na msimu wa NHL 2019- 20. Mlipuko huo ulivurugu michezo ya Olimpiki ya 2020, ambayo ilikuwa imepangwa kuanza mwishoni mwezi Julai; Kamati ya Olimpiki ya kimataifa ilitangaza tarehe 24 Machi kwamba michezo hiyo "itafanyika tarehe mpya baada ya mwaka 2020 lakini si baada ya majira ya joto 2021".[278][279][280][281][282]

Sekta ya burudani pia imekuwa iliathiriwa, na makundi mengi ya muziki yamesitisha au kufuta ziara ya tamasha. Mashindano ya wimbo wa Eurovision, ambayo yalipangwa kufanyika nchini Uholanzi mwezi Mei, yaliahirishwa hadi mwaka 2021. Thamthilia kubwa kama vile Broadway pia zilisitisha maonyesho yote. Wasanii wengine wametafuta njia mabadala kuendelea kuzalisha na kushiriki kazi yao mtandaoni, kama vile matamasha na sherehe. Pia kuna mizaha mingi na ucheshi kuhusu virusi vya COVID-10 mtandaoni, kama watu wengi watafuta njia za kuvumilia ukosefu wa uhakika.[283][284][285][286][287]

Siasa hariri

Janga hilo limeathiriwa mifumo ya kisiasa ya nchi nyingi, kuvuruga shughuli za kisheria. Wanasiasa wengi wameambukizwa na kujitenga na wengine wamekufa. Ratiba ya uchaguzi kadhaa imebadilishwa kutokana na hofu ya virusi.[288][289][290]

Uchina hariri

Serikali ya Uchina imekosolewa na serikali ya Marekani, Waziri wa ofisi ya Baraza la mawaziri wa Uingereza Michael Gove, na wengine kutokana na utunzaji wao wa janga hilo.[291] [292]Baadhi ya wasimamizi wa ngazi za majimbo wa chama cha kikomunisti wa Uchina walifukuzwa kwa sababu jinsi walivyosimamia juhudi za karantini huko Uchina ya kati, ishara ya kutoridhika kwa majibu yao ya mlipuko. [293]Baadhi ya wachambuzi waliamini hatua hizi zilikusudiwa kumlinda Waziri Mkuu wa Kichina, Xi Jinping kutoka utata huo. Jumuiya ya upelelezi ya Marekani inasema kwamba serikali ya Uchina haikuripoti idadi sahihi ya kesi za coronavirus kwa maksudi.[294]

Marekani hariri

Mlipuko huo ulisababisha wito kwa Marekani kuunga sera za kijamii sawa ya nchi nyingine tajiri, zikiwemo huduma za afya kwa kila raia, huduma za watoto wote, msaada wa wagonjwa, na viwango vya juu vya fedha za umma za afya.[295] [296]Wachambuzi wa kisiasa walitarajia kwamba hali hiyo pengine ingepunguza nafasi ya Donald Trump kushinda uchaguzi mpya mwezi Novemba.[297] Kuanzia kati ya Aprili 2020, kulikuwa na maandamano katika majimbo kadhaa ya Marekani dhidi ya ufungaji wa biashara ulioagizwa na serikali na vikwazo vya kusafiri na mawasailiano.[298]

Nchi nyingine hariri

Mazoezi ya kijeshi ya NATO ya 2020 yanaohusisha Ujerumani, Poland, na nchi za Baltic, mazoezi makubwa zaidi tangu mwishoni kwa vita baridi, yatafanyika kwa kiwango kidogo zaidi.[299]

Serikali ya Irani imeathiriwa sana na virusi, na wabunge takriban ishirini na nne na wanasiasa wa sasa au zamani kumi na tano waliambukizwa.[300] Rais wa Irani Hassan Rouhani aliwaandikia viongozi wa dunia barua ya umma akiomba msaada tarehe 14 Machi 2020, akisema walikuwa na changamoto kupambana na mlipuko huo kutokana na vikwazo vya Marekani dhidi ya Irani.[301] Saudi Arabia, ambayo ilianza kuingilia kwa kijeshi nchini Yemeni mwezi Machi 2015, ilitangaza kukoma kwa vita.[302]

Mahusiano ya kidiplomasia baina ya Japan na Korea Kusini yaliharibika kutokana na janga.[303] Korea Kusini iliikosoa Japan kwa sababu "juhudi zao karantini mbaya" baada ya Japani ilitangaza wale wote waliofika kutoka Korea Kusini lazimia waende karantini kwa wiki mbili mahali panapochaguliwa na serikali.[304] Mwanzoni wananchi wa Korea Kusini waligawanyika kuhusu majibu ya Rais Moon Jae-in; wengi walipiga saini ama iliyomsifa na pia ama iliyosema aondolewe.[305]

Nchi nyingine zimepitisha sheria ya dharura kujibu janga hilo. Baadhi ya wachambuzi wameonyesha wasiwasi kwamba ingeruhusu serikali kuimarisha madaraka yao.[306] Nchini Ufilipino, wabunge walimpa Rais Rodrigo Duterte madaraka za dharura wakati wa janga hilo. Nchini Hungary, wabunge walipiga kura kumruhusu Waziri Mkuu, Viktor Orbán, kutawala kwa kutoa amri kwa muda usiojulikana, kusimamisha bunge pamoja na uchaguzi, na kuwaadhibu wale wanaotuhumiwa kusambaza taarifa za uongo kuhusu virusi na sera za serikali. [307]Katika baadhi ya nchi, kama vile Misri, Uturuki, na Thailand, wanaharakati wa upinzani na wakosoaji wa serikali wamekamatwa kwa kutuhumiwa kueneza habari ambazo serikali hizo zinadai ni bandia kuhusu janga hilo.[308] [309]

Elimu hariri

Janga la coronavirus limeathiri mifumo ya elimu duniani kote, kusababisha ufungaji wa shule, vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu.[310]

Serikali nyingi duniani kote zimefunga taasisi za elimu kwa muda kama jaribio kudhibiti usambazaji wa virusi hivyo. Mnamo 24 Mei 2020, wanafunzi takriban 1,725,000,000 waliathiriwa na kufungwa kwa shule. Kwa mujibu ya shirika la UNICEF, nchi 153 zimetekeleza ufungaji wa nchi nzima na 24 kutekeleza ufungaji wa wenyeji, kuathiri asilimia 98.6 ya idadi ya wanafunzi duniani. Shule za nchi 10 kwa sasa ziko wazi.[311][312]

Tarehe 23 Machi 2020, mitihani ya kimataifa ya Cambridge (CIE) ilitangaza kufutwa mitihani yake. Mitihani ya kimataifa ya Baccalaureate pia imefutwa. Pia mitihani ya AP, SAT, na ACT nchini Marekani imehamisha mtandaoni au kufutwa.[313]

Kufungwa kwa shule kunaathiri sio wanafunzi tu, lakini pia walimu, na familia. Kuna matokeo makubwa ya kiuchumi na kijamii. Hali hiyo imevutia macho masuala mengi, kwa mfano, madeni ya wanafunzi,[314] mafunzo ya dijitali,[315] ukosefu wa chakula,[316] na kukosa makazi,[317] pamoja na utunzaji wa watoto,[318] huduma za afya, nyumba, mtandao, na huduma za ulemavu. Athari hiyo ilikuwa kali zaidi kwa watoto wasio na mahitaji na familia zao, kuvuruga kujifunza, lishe ya watoto, matatizo ya kiuchumi kwa familia bila ajira.[319][320][321]

Kujibu kwa kufungwa kwa shule, shirika la UNESCO lilipendekeza matumizi ya mipango ya kujifunza mbali kama mtandaoni na kufungua majukwaa ya elimu ambayo shule na waalimu wanaweza kutumia ili wapunguze usumbufu wa elimu.

Masuala mengine ya afya hariri

Janga hilo limekuwa na athari nyingi za afya duniani zaidi ya zile zinazosababishwa na coronavirus. Limesababisha upungufu wa ziara hospitalini kwa sababu zingine. Kumekuwa na upungufu wa asilimia 38 wa ziara za hospitalini kwa ajili ya dalili za matatizo ya moyo nchini Marekani na asilimia 40 nchini Hispania.[322] Mtaalamu wa moyo huko Chuo Kikuu cha Arizona alisema, "Nina wasiwasi kwamba watu wengi wanakufa nyumbani kwa sababu wana ogopa sana kwenda hospitalini."[323] Pia kuna wasiwasi kwamba watu wenye matatizo ya afya mengine hawachelewi kwenda hospitalini. Upungufu wa vifaa vya matibabu umeathiri watu wenye magonjwa mbalimbali.[324]

Katika nchi kadhaa kumekuwa na upungufu wa magonjwa ya maambukizo ya zinaa, kama vile HIV, kutokana na sera za karantini na kujitenga na mapendekezo ya kutofanya ngono ya kawaida. [325]Vile vile, katika baadhi ya maeneo, viwango vya maambukizo ya mafua na virusi vingine vimeanguka kwa kiwango kikubwa wakati wa janga hilo. Janga pia limeathiri vibaya afya ya akili duniani kote.[326][327]

Ubaguzi wa rangi hariri

Tangu mwanzo wa mlipuko huo, kuchochea chuki, ubaguzi, na ubaguzi wa rangi vimeripotiwa duniani kote dhidi ya watu wa Kichina na Asia Mashiriki.[328][329]Taarifa mnamo Februari (kesi nyingi zaidi zilipokuweko Uchina) zilionyesha hisia za ubaguzi kuhusu watu wa Kichina, na ongezeko la wazo la wachina walistahili kupata virusi. [330] [331]Raia za nchi kadhaa zikiwemo Malaysia, New Zealand, Singapore, Japani, Vietnam, na Korea Kusini walishinikiza serikali zao kupiga marufuku watu wa kichina kuingia nchi zao. Watu wa Kichina na Waasia wengine nchini Uingereza na Marekani wameripoti ongezeko la viwango vya unyanyasaji wa rangi na mashambulizi.[332][333]

Kufuatia usambazaji hadi nchi nyingine, watu wanaotoka Italia (nchi ya kwanza huko Ulaya yenye mlipuko mkubwa) walikabiliwa na ubaguzi, na pia watu wanaotoka nchi nyingine zenye kesi nyingi.[334] Ubaguzi dhidi ya Waislamu nchini India uliongezeka baada ya mamlaka ya afya ya umma ilitambua mkusanyiko wa umisionari wa kiislamu mjini New Delhi mwezi Machi 2020 kama chanzo cha kuenea.[335] Paris imekuwa na ghasia kuhusu jinsi polisi walivyowatendea watu wenye rangi wakati wa ufungaji.[336] Ubaguzi wa rangi dhidi ya watu wanaotoka Asia Kusini na Asia Kusini Mashiriki uliongezeka katika mataifa ya Kiarabu. Jamii ya LGBTQ ya Korea Kusini iliwalaumuliwa na watu wengine kwa kuenea virusi hivyo mjini Seoul.[337][338]

Nchini Uchina, ubaguzi wa rangi dhidi ya wakazi wasio Kichina umechochewa na janga hilo, na wageni waliitwa "takataka za kigeni" na walilengwa kwa "utupaji". [339]Baadhi ya watu weusi walifukuzwa na polisi kutoka nyumbani kwao na kuambiwa kuondoka Uchina kabla ya masaa 24, kutokana na taarifa za uongo za wageni wakieneza virusi. Ubaguzi wa rangi huko ulikosolewa na serikali za kigeni na kundi la kidiplomasia, hasa serikali za nchi za Afrika, na Uchina iliomba samehe, lakini pia serikali ya Uchina imedai kwamba vyombo vya habari vya kigeni vimetia chumvi matukio hayo ili vionyeshe picha mbaya ya Uchina. Ubaguzi wa rangi dhidi ya watu waAfrika umeendelea. WaAfrika wameondolewa migahawani, madukani, na mahali pengine nchini Uchina.[340][341][342]

Usambazaji wa habari hariri

Magazeti mengi yameruhusu kusoma makala zote kuhusu virusi hivyo kwa bure mtandaoni, wakati wachapishaji wa kisayansi walifanya upatikanaji karatasi za kisayansi kuhusu mlipuko huo wazi. Baadhi ya wanasayansi walichagua kugawa matokeo yao haraka zaidi kwenye seva za kuchapisha kama vile bioRxiv.[343][344][345]

Taarifa potofu hariri

Janga hilo limesababisha taarifa potofu na taarifa na nadharia za janja kuhusu virusi kama vile asili, kuzuia, utambuzi, na matibabu ya ugonjwa huo.[346][347] Habari za uongo, zikiwemo taarifa kama hizo zilizosambazwa kwa makusudi, zimeenezwa kutumia mtandao ya kijamii, ujumbe, na vyombo vya habari vya serekali za nchi zikiwemo Uchina, Urusi, Irani, na Turkmenistan.[348] [349] [350] [351]Pia habari hizo zimekuwa kueneza kwa operesheni za siri za serikali ili zizalishe hofu nchini nyingine. Katika nchi nyingine, kama vile India, Bangladesh, na Ethiopia, waandishi wa habari wamekamatwa kwa tuhuma za kueneza habari bandia kuhusu janga hilo.[352]

Taarifa potofu zimeenezwa na watu maarufu na wanasiasa.[353] Wabiashara wa kudanganya wamedai kuuza vipimo vinavyoweza kutumiwa nyumbani, kinga, na matibabu ya "muujiza". [354]Makundi kadhaa ya kidini yamedai imani yao itawalinda dhidi ya virusi. [355]Baadhi ya watu wamedai virusi ni silaha ya kibiolojiki iliyoruhusu kutolewa maabarani kwa ajali au kwa makusudi, mpango wa udhibiti wa idadi ya watu, matokeo ya operesheni ya kijasusi, au matokeo ya jumla ya uboreshaji wa 5G kwenye mitandao ya simu.[356][357]

Shirika la afya duniani limetangaza "janga la habari potofu" kuhusu virusi, ambalo linasababisha hatari kwa afya ya kimataifa.[358]

Mfululizo wa matukio ya janga la COVID-19 hariri

Makala hii inahusu mfululizo na historia ya SARS-CoV-2, virusi vinavyosababisha COVID-19 vyenye wajibu wa janga la sasa. Kesi za kwanza zilizohusisha binadamu zilitambuliwa mjini Wuhan, Uchina mwezi Desemba 2019.[359]

Historia ya Janga hariri

Kuanzia mwezi Januari 2020 utafiti wa timu tofauti ulieleza hali ya matibabu na pia kuchambua maendeleo ya virusi hivyo.[360]

Kesi za mapema zilizotambuliwa na maabara ziligunduliwa baadaye. [361]

Kwa ajili ya utafiti mapema, chanzo cha virusi hivyo pengine kiliendeleza mnamo 22-24 Novemba 2019 . Mnamo May 2020 nadharia hiyo ilithibitishwa na takwimu zaidi na mwanzo wa virusi COVID-19 ilitambuliwa mnamo 6 Octoba 2019 hadi 11 Desemba 2019. Pia ushahidi nguvu unaashiria kwamba virusi vilianza katika popo lakini vilienea binadamu kupitisha aina nyingine ya mnyama kutoka popo hadi binadamu. Inawezekana uwezo wa kuenea miongoni kwa binadamu uliendeleza baadaye. [362][363][364]

17 Novemba 2019 hariri

Kwa ajili ya utafiti uliofanywa baadaye, mgonjwa wa kwanza aliambukizwa na COVID-19, ingawa ugonjwa huo umekuwa haujatambulishwa.  Aliishi jimbo la Hubei, Uchina.[360]

1 Desemba hariri

Utafiti unaonyesha kwamba dalili za “Mgonjwa Sifuri” au mgonjwa wa kwanza zilianza tarehe 1 Desemba. Yeye alikuwa mwanamume na hakuenda Soko la Samaki mjini Wuhan na familia yake haikuathiriwa na hakuwa na uhusiano baina yake na kesi nyingine. Baadaye ilithibitishwa kwamba alikuwa na miaka sabini, alikuwa na ugonjwa wa Alzheimer na aliishi mbali kutoka sokoni na kwa kawaida hakuondoka nyumbani.[365][366]

16 Desemba hariri

Watu wa kwanza wenye virusi hivyo walilazwa hospitalini tarehe 16 Desemba. Wazee wawili wenye homa na kohoa walienda hospitalini Hubei Provincial. Mkuu wa matibatu ya kupumua Dk Zhang Jixian aliyewatiba alitambua ugonjwa wao kama pengine mafua au nimonia.[367][368]

24 Desemba hariri

Sampuli ya mate ya kifua ilitumia maabara Vision Medicals kutoka Hospitali Wuhan Central kwa uchambuzi wa kijenetiki. [369]

27 Desemba hariri

Baada ya kuangalia picha za CT za wazee hazikuwa kwaida, Dk Jixian alimwuliza mvulana wa wazee hao kupata CT na matokeo yalikuwa sawa. Jixian alifanya kazi kuhusu janga la SARS na alituhuma kulikuwa na mlipuko mengine wa maambukizo hayo. Mgonjwa mwengine, mfanyabiashara katika soko la samaki mjini Wuhan, alifikia hospitalini siku hiyo hiyo mwenye dalili sawa. Damu za wagonjwa wote zilipimwa na matokeo yanaonyesha walikuwa na aina ya virusi lakini sio mafua. Dk Jixian aliwaripotia wakuu wake na aliweka sehemu ya karantini. [370][371]

Hospitali ya Wuhan Central alipata ujumbe kutoka maabara Vision Medicals ukisema kwamba sampuli tarehe 24 Desemba ilikuwa na aina mpya ya coronavirus.  Mgonjwa huyo aliwekwa karantini. Pia huko hospitali ya Wuhan Central, sampuli nyingine ilikusanyika kutoka mgonjwa mwengine mwenye ugonjwa usiojulikana na sampuli hiyo ilitumia maabara CapitalBio Medlab mjini Beijing. [372][373]

29 Desemba hariri

Siku hiyo na jana kesi tatu zilifikia hospitalini Hubei Provincial, zote zilizohusiana na soko la samaki. Mamlaka ya afya ilikuwa imejulishwa na wataalamu wa magonjwa ya maambukizo walikuja kutoka hospitali Wuhan Central ili wawahamishe wagonjwa sita wa saba. Dk Jixian aliamua kuwaruhusu wafanyakazi wa matibabu katika idara yake kuvaa barakoa na aliagiza makoti ya kinga. [374]

Wakuu wa hospitali ya Hubei Provincial walikutana na jupo la madaktari ambao walimaliza kwamba kesi hizo hazikuwa kawaida na kuhitajika mwangalizi maalum na pia, kwa sababu walikuwa wamejifunza juu ya kesi mbili nyingine mjini, waliamua kuripoti hitimisho zao mamlaka ya afya ya mji na jimbo. [375][376]

30 Desemba hariri

Hospitali ya Wuhan Central ilipokea ripoti kutoka maabara ya CapitalBio Medlab iliyodai kesi ya SARS. Kwa mujibu ya mtandao ya kijamii, matokeo hayo yaligunduliwa si kweli baadaye. Madaktari kadhaa wakiwemo Dk Ai Fen waliweka matokeo ya kipimo mtandaoni kwa kijamii kwa wenzao, wakiwemo Dk Li Wenliang. [377][378]

Ujumbe rasmi wa kwanza hariri

Tume ya afya ya mji wa Wuhan ilitumia taasisi zake ujumbe: [379]

Madaktari wanaosimamia watekeleze udhibiti na kuanzisha timu maalum.

Wafanyakazi wote wakae macho, hasa kuangalia wagonjwa wenye dalili kama zile za numonia inayoambukiza.

Ni lazima takwimu zikusanyike kwa kawaida na kutumia tume ya afya ya Wuhan na jimbo la Hubei.

Takwimu za wiki iliyopita, kuhusu wagonjwa wenye dalili za numonia inayoambukiza, zitumie tume ya afya ya Wuhan kabla ya saa kumi jioni siku hiyo hiyo.

Bila ruhusu kutoka mamlaka hakuna mtu ye yote anayeruhusiwa kueneza habari juu ya matibabu. 

31 Desemba hariri

Ujumbe wa umma wa kwanza hariri

Tume ya afya ya Wuhan ilijulisha jamii juu ya ishara mapema za mlipuko wa numonia. Ujumbe huo unatoa picha ya tahadhari; ulijumuisha maagizo ya siku iliyopita kwa hospitali za mji; ulitia mkazo utafiti ulioendelea na kutafuta matibabu ambapo kulikuwa na dalili za numonia; na ulishauri umma kuvaa barakoa na kuepuka mahali ndani pa umma penye watu wengi. [380]

Mnamo siku hiyo, kulikuwa na kesi 266 huko jimbo la Hubei. [381]

Qu Shiqan, mwuzaji sokoni kwa samaki, alisema kwamba maofisa ya serikali walisafisha mahali hapo terehe 31 Desemba na waliwaambia wauzaji wavae barakoa. Qu alisema kwamba alijifunza juu ya mlipuko wa numonia kutoka ripoti za vyombo vya habari tu. “Awali nilifikiri kwamba walikuwa na mafua,” alisema. “Si kali sana. Sisi tunauza samaki. Tunaweza kuambukizwa vipi?” Wachambuzi wengi walisema baadaye kwamba kusafisha sokoni kuliharibu ushahidi muhimu uliohitajika kugundua asili ya COVID-19.[382]

Dk Li Wenliang aliyesimamia idara ya dharura ya hospitali Wuhan Central alikabiliwa na maofisa ya usalama mjini Wuhan kwa sababu alichapisha habari za ugonjwa mtandaoni kwa kijamii. Walimwonya akome “kueneza uongo.” [383]

Kwa mujibu ya kituo cha afya cha serikali ya Hong Kong, hatua mbalimbali kuangalia na kudhibiti mipaka zilianza, zikiwemo uangalizi wa joto. [384]

Tume ya afya ya Wuhan ilitumia taasisi zake ujumbe kwenye karatasi wenye mwongozo wa kukabiliana na mlipuko wa numonia unaowezekana. Siku hiyo hiyo nakala mbili pia ziliwekwa mtandaoni kwa kijamii Weibo.  [385][386]

Ofisi ya shirika la WHO mjini Beijing ilijulishwa juu ya “aina ya numonia yenye sababu isiyojulikana” ambayo iligunduliwa mjini Wuhan. [387]

Vyombo vya habari vya kimataifa Reuters na Deutsche Welle vilipata habari hiyo na pia gazeti la South China Morning Post huko Hong Kong:

Hong Kong ichukua hatua za dharura kama numonia ya fumbo iwaambukiza watu 27 Wuhan [388]

Uchina ichunguza virusi kama SARS kama wagonjwa wengi waathiri [389]

Maofisa wa Uchina wachunguza mlipuko wa numonia Wuhan [390]

1 Januari 2020 hariri

Dk Ai alionywa na wakuu wake kwa sababu aliwaambia wenzake juu ya virusi vipya.  [29]

3 Januari hariri

Uchina iliambia rasmi Marekani juu ya virusi hivyo na ilianza kulipa shirika la WHO habari kila siku. [391] [392]

Tume ya afya ya kitaifa ya Uchina iliagiza taasisi mjini Wuhan zisichapishe habari zo zote kuhusu virusi hivyo na ziangamize sampuli za ugonjwa huo.[29]

Dk Li alionywa na polisi kukoma kueneza habari kuhusu virusi hivyo.  [393]

6 Januari hariri

Serikali ya Marekani ilitolea Uchina timu ya wataalamu wazuri wa magonjwa ya maambukizo ili wasaidie.  Uchina ilikataa. [29]

9 Januari hariri

Uchina ilitangaza kwamba wanasayansi wa kiChina wamemaliza uchambuzi wa kijenetiki wa COVID-19. [394][395]

14 Januari hariri

Katika mkutano siri wa maofisa wa Uchina, mkuu wa tume ya afya kitaifa alisema kwamba hali hiyo ilikuwa “changamoto kali zaidi tangu SARS.”[396]

Shirika la WHO lilirudia habari kutoka Uchina kwamba virusi hivyo havienei miongoni mwa binadamu.  [359]

20 Januari hariri

Mkuu wa Uchina Xi Jinping alijadili virusi hivyo kwa umma kwa mara ya kwanza.  [397]

Katika hoja na vyombo vya habari vya serikali, Dk Zhong Nanshan alithibitisha virusi hivyo vinaweza kuenea miongoni mwa binadamu. [398]

Korea Kusini na Marekani zilithibitisha kesi zao za kwanza. [399][400]

23 Januari hariri

Mji yote ya Wuhan iliwekwa ufungaji au karantini kwa siku 72. Siku ijayo serikali ya Uchina ilipiga marufuku za usafiri kuingia na kuondoka jimbo la Hubei. [401]

24 Januari hariri

Ufaransa ilithibitisha kesi yake ya kwanza, lakini baadaye iligunduliwa kwamba kulikuwa na kesi nyingine tarehe 27 Desemba 2019 nchini Ufaransa. [402]

27 Januari hariri

Serikali ya Uchina ilipiga marufuku za usafiri wa makundi ya watu kwenda nchi nyingine. [401]

Meya wa Wuhan alisema kwamba hakuweza kutoa taarifa juu ya hali halisi mapema zaidi kutokana na mfumo wa kisiasa wa Uchina.  “Serikali ya kienyeji hairuhusiwi kufanya hivyo bila ruhusu kutoka serikali ya kitaifa,” alisema. [403]

30 Januari hariri

Shirika la WHO lilitangaza Coronavirus vilikuwa dharura ya afya ya kimataifa.[404]

31 Januari hariri

Rais Trump wa Marekani alipiga marufuku za usafiri kutoka Uchina isipokuwa Wamarekani.  [161]

Uingereza na Urusi zilithibitisha kesi zao za kwanza za COVID-19. [405]

6 February hariri

Mtu wa kwanza nchini Marekani alikufa kutokana na COVID-19. [406]

7 Februari hariri

Dk Li alikufa kutokana na COVID-19. [29]

19 Februari hariri

Irani ilithibitisha vifo vyake ya kwanza kutokana na COVID-19.[407]

13 Machi hariri

Rais Trump wa Marekani alitangaza hali ya dharura ya kitaifa. [161]

19 Machi hariri

Italia ilikuwa nchi yenye vifo vingi zaidi duniani kutokana na COVID-19.

26 Machi hariri

Marekani ilikuwa nchi yenye kesi zilisothibitishwa nyingi zaidi duniani. [408]

17 Aprili hariri

Serikali ya Uchina ilikiri kwamba kulikuwa na vifo vingi zaidi mjini Wuhan kuliko hivyo vilivyoripotiwa.  Serikali iliongeza idadi ya vifo kwa 50%. [29]

19 Aprili hariri

Serikali ya Australia ilidai uchunguzi huru wa asili ya janga hilo. Baadaye zaidi ya nchi 100 ziliunga mkono hatua hiyo.  [29]

17 Aprili hariri

Uchina iliita hatua hiyo ni “hatari” na ilitisha kulipiza kisasi cha kiuchumi kwa nchi zilizounga mkono. Lakini baadaye Uchina ilikubali kushirikiana na uchunguzi huo. [29]

Ufupisho hariri

Utafiti wa kihistoria unaamini kwamba SARS-CoV-2 viliendeleza mwezi Novemba. Ufahamu wa kisayansi wa aina mpya ya SARS coronavirus ulifanyika maabarani Vision Medicals jimbo la Guangzhou mnamo 24-27 Desemba 2019.  Ufahamu wa kikliniki wa janga linalokuja lilianza hospitalini Hubei Provincial karibu na wakati huo huo mnamo 27-29 Desemba. Tarehe 31 Desemba mamlaka ya afya ya Wuhan ilitoa takwimu ya kesi.  Wachambuzi wengi nchini nyingi wamedai Uchina kwa kuchelewa habari za virusi hivyo na kujaribu kuficha ukali wa virusi hivyo baada ya ilikuwa wazi kwamba kulikuwa na aina mpya ya virusi vilivyosambaa kwa rahisi.  [29][359]

Picha hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

  1. Hui, David S.; Azhar, Esam EI; Madani, Tariq A.; Ntoumi, Francine; Kock, Richard; Dar, Osman; Ippolito, Giuseppe; Mchugh, Timothy D.; Memish, Ziad A.; Drosten, Christian; Zumla, Alimuddin (14 January 2020). "The continuing epidemic threat of novel coronaviruses to global health – the latest novel coronavirus outbreak in Wuhan, China". International Journal of Infectious Diseases (kwa English) 91: 264–266. ISSN 1201-9712. doi:10.1016/j.ijid.2020.01.009.  Check date values in: |date= (help)
  2. "Undiagnosed pneumonia - China (HU) (01): wildlife sales, market closed, RFI Archive Number: 20200102.6866757". Pro-MED-mail. International Society for Infectious Diseases. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 22 January 2020. Iliwekwa mnamo 13 January 2020.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  3. Cohen, Jon; Normile, Dennis (17 January 2020). "New SARS-like virus in China triggers alarm". Science (kwa Kiingereza) 367 (6475): 234–235. ISSN 0036-8075. PMID 31949058 Check |pmid= value (help). doi:10.1126/science.367.6475.234. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 17 January 2020. Iliwekwa mnamo 17 January 2020.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); Unknown parameter |url-access= ignored (help); Check date values in: |date=, |archivedate=, |accessdate= (help)
  4. Parry, Jane (20 January 2020). "China coronavirus: cases surge as official admits human to human transmission". British Medical Journal 368. ISSN 1756-1833. doi:10.1136/bmj.m236.  Unknown parameter |url-access= ignored (help); Check date values in: |date= (help)
  5. "Chinese premier stresses curbing viral pneumonia epidemic". China Daily. Beijing: Xinhua News Agency. 21 January 2020. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 22 January 2020. Iliwekwa mnamo 22 January 2020.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); Check date values in: |date=, |archivedate=, |accessdate= (help)
  6. Deutsche Welle (www.dw.com). "Hali ilivyo kuhusu Corona duniani | DW | 23.03.2020". DW.COM (kwa sw-TZ). Iliwekwa mnamo 2020-03-23. 
  7. Qin, Amy. "China Reports First Death From New Virus", The New York Times, 10 January 2020. 
  8. 8.0 8.1 Field, Field. "Nine dead as Chinese coronavirus spreads, despite efforts to contain it", The Washington Post, 22 January 2020. 
  9. Here's how long coronaviruses may linger on contaminated surfaces, according to science, tovuti ya CNN, tar 18-02-2020
  10. Fernando Duarte. "Who is 'patient zero' in the coronavirus outbreak?". www.bbc.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  11. "China’s first confirmed Covid-19 case traced back to November 17". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2020-03-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  12. Areddy, James T. (2020-05-26), "China Rules Out Animal Market and Lab as Coronavirus Origin", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  13. "404_财新网". other.caixin.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  14. "24h精彩新闻_新闻中心_中华网". news.china.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  15. Yu, Verna (2020-02-07), "'Hero who told the truth': Chinese rage over coronavirus death of whistleblower doctor", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  16. Kuo, Lily (2020-03-11), "Coronavirus: Wuhan doctor speaks out against authorities", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  17. "Mystery pneumonia virus probed in China", BBC News (kwa en-GB), 2020-01-03, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  18. Li, Qun; Guan, Xuhua; Wu, Peng; Wang, Xiaoye; Zhou, Lei; Tong, Yeqing; Ren, Ruiqi; Leung, Kathy S.M.; Lau, Eric H.Y. (2020-03-26). "Early Transmission Dynamics in Wuhan, China, of Novel Coronavirus–Infected Pneumonia". The New England Journal of Medicine 382 (13): 1199–1207. ISSN 0028-4793. PMC 7121484 Check |pmc= value (help). PMID 31995857 Check |pmid= value (help). doi:10.1056/NEJMoa2001316. 
  19. "COVID-19 pandemic", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-11, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  20. "China confirms sharp rise in cases of SARS-like virus across the country". France 24 (kwa Kiingereza). 2020-01-20. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  21. Team, The Novel Coronavirus Pneumonia Emergency Response Epidemiology (2020-02-01). "The Epidemiological Characteristics of an Outbreak of 2019 Novel Coronavirus Diseases (COVID-19) — China, 2020". China CDC Weekly (kwa Kiingereza) 2 (8): 113–122. ISSN 2096-7071. doi:10.46234/ccdcw2020.032. 
  22. https://www.thelancet.com/action/showPdf?pii=S0140-6736%2820%2930183-5
  23. Flattery and foot dragging: China’s influence over the WHO under scrutiny, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  24. Bob Fredericks (2020-03-13). "WHO says Europe is new epicenter of coronavirus pandemic". New York Post (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  25. Jr, Donald G. McNeil (2020-03-26), "The U.S. Now Leads the World in Confirmed Coronavirus Cases", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  26. "Studies Show N.Y. Outbreak Originated in Europe", The New York Times (kwa en-US), 2020-04-08, ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  27. Staff, Reuters (2020-05-04), "After retesting samples, French hospital discovers COVID-19 case from December", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  28. "2 died with coronavirus weeks before 1st U.S. virus death". PBS NewsHour (kwa en-us). 2020-04-22. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  29. 29.0 29.1 29.2 29.3 29.4 29.5 29.6 29.7 29.8 "The Great Wall of Silence," The Australian, 8 May 2020.
  30. 30.0 30.1 "ArcGIS Dashboards". www.arcgis.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  31. 5 million people left Wuhan before China quarantined the city to contain the coronavirus outbreak, taarifa ya gazeti Business Insider USA, kupitia www.pulselive.co.ke, tarehe 27-01-2020
  32. "China coronavirus: 'family cluster' in Vietnam fuels concerns over human transmission". South China Morning Post. 29 January 2020. Iliwekwa mnamo 29 January 2020.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  33. "Germany confirms human transmission of coronavirus". Deutsche Welle. 28 January 2020. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 28 January 2020. Iliwekwa mnamo 29 January 2020.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); Check date values in: |date=, |archivedate=, |accessdate= (help)
  34. Goh, Timothy; Toh, Ting Wei (23 January 2020). "Singapore confirms first case of Wuhan virus; second case likely". The Straits Times. Iliwekwa mnamo 23 January 2020.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  35. "France confirms two cases of deadly coronavirus". The Independent (kwa Kiingereza). 2020-01-24. Iliwekwa mnamo 2020-01-24. 
  36. Turkey and Pakistan close borders with Iran ove Coronavirus deaths, gazeti la Guardian (UK) ya 23 Feb 2020
  37. Coronavirus: South Korea to test 200,000 sect members as pandemic fears hit markets, gazeti la Guardian (UK) ya 25 Feb 2020
  38. Coronavirus: Britons returning from northern Italy told to self-isolate,BBC ya 25 Feb 2020
  39. WHO characterizes COVID-19 as a pandemic, tovuti ya WHO, iliangaliwa 12 Machi 2020
  40. Confirmed Cases and Deaths by Country, Territory, or Conveyance, tovuti ya worldometers.com ya tar. 12.042020
  41. Coronavirus cases in Tanzania rises to Six
  42. https://www.mwananchi.co.tz/habari/kitaifa/Ndugu-wa-Mtanzania-aliyekufa-kwa-corona-azungumza/1597296-5509666-cpgxwl/index.html
  43. "Schengen Area Crisis: EU States Close Borders as Coronavirus Outbreak Grips Bloc". SchengenVisaInfo.com (kwa Kiingereza). 2020-03-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  44. Alasdair Sandford (2020-04-02). "Coronavirus: Half of humanity on lockdown in 90 countries". euronews (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  45. "Infographic: What Share of the World Population Is Already on COVID-19 Lockdown?". Statista Infographics (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  46. https://www.washingtonpost.com/nation/2020/05/21/coronavirus-update-us/
  47. Abdurasulov, Abdujalil (2020-04-07), "Why has this country reported no virus cases?", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  48. Tan, Yvette (2020-04-03), "Scepticism over N Korea's claim to be virus free", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  49. Erkhembayar, Ryenchindorj; Dickinson, Emma; Badarch, Darmaa; Narula, Indermohan; Warburton, David; Thomas, Graham Neil; Ochir, Chimedsuren; Manaseki-Holland, Semira (2020-09-01). "Early policy actions and emergency response to the COVID-19 pandemic in Mongolia: experiences and challenges". The Lancet Global Health (kwa English) 8 (9): e1234–e1241. ISSN 2214-109X. PMID 32711684 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/S2214-109X(20)30295-3. 
  50. Dennis NormileMar. 17, 2020, 8:00 Am (2020-03-17). "Coronavirus cases have dropped sharply in South Korea. What’s the secret to its success?". Science | AAAS (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  51. Chan, Wilfred (2020-04-03), The WHO Ignores Taiwan. The World Pays the Price. (kwa en-US), ISSN 0027-8378, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  52. "Vietnam’s response to coronavirus crisis earns praise from WHO". 7NEWS.com.au (kwa Kiingereza). 2020-04-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  53. Jon CohenJan. 26, 2020, 11:25 Pm (2020-01-26). "Wuhan seafood market may not be source of novel virus spreading globally". Science | AAAS (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  54. hermesauto (2020-02-28). "How early signs of the coronavirus were spotted, spread and throttled in China". The Straits Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  55. Bill Bostock. "China knew the coronavirus could become a pandemic in mid-January but for 6 days claimed publicly that there was no evidence it could spread among humans". Business Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  56. Kuo, Lily (2020-01-21), "China confirms human-to-human transmission of coronavirus", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  57. "How China Delayed Warnings to Public During 6 Key Days in January | RealClearPolitics". www.realclearpolitics.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  58. "Bloomberg - Are you a robot?". www.bloomberg.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  59. "Xi stresses winning people's war against novel coronavirus - Xinhua | English.news.cn". www.xinhuanet.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-28. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  60. "COVID-19 pandemic", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-11, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  61. "COVID-19 pandemic", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-11, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  62. "China halts flights and trains out of Wuhan as WHO extends talks". CNA (kwa Kiingereza). Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-01-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  63. "China seeks to signal coronavirus under control", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-10, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  64. 李雪晴. "China's State Council extends Spring Festival holiday". www.chinadaily.com.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  65. "COVID-19 pandemic", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-11, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  66. www.bjnews.com.cn. "湖北这些学校推迟开学 北大等暂停参观". www.bjnews.com.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  67. Zhong, Raymond; Mozur, Paul (2020-02-15), "To Tame Coronavirus, Mao-Style Social Control Blankets China", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  68. "COVID-19 pandemic", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-11, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  69. "China deploys measures to curb imported COVID-19 cases, rebound in indigenous cases | english.scio.gov.cn". english.scio.gov.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  70. Akinwotu, Jason Burke Emmanuel; Beijing, and Lily Kuo in (2020-04-27), "China fails to stop racism against Africans over Covid-19", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  71. "China deploys measures to curb imported COVID-19 cases, rebound in indigenous cases | english.scio.gov.cn". english.scio.gov.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  72. Wang, Vivian; Wee, Sui-Lee (2020-03-24), "China to Ease Coronavirus Lockdown on Hubei 2 Months After Imposing It", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  73. James Griffiths CNN. "As coronavirus cases spike worldwide, China is closing itself off". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  74. "China to stage day of mourning for the thousands lost to Covid-19". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2020-04-03. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  75. 75.0 75.1 "The Great Wall of Silence," The Australian, 8 May 2020.
  76. "Coronavirus Arrives in Iran: Two People Test Positive in Qom". irangov.ir. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  77. "Iranian Doctors Call For 'Long Holiday' To Contain Coronavirus, As Sixth Victim Dies". RFE/RL (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  78. "Iran Announces Closure Of Universities, Schools As Coronavirus Death Toll Rises". RFE/RL (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  79. "اختصاص 530 میلیارد تومان به وزارت بهداشت برای مقابله با کرونا". پایگاه خبری جماران (kwa Kiajemi). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  80. "Coronavirus: Iran has no plans to quarantine cities, Rouhani says", BBC News (kwa en-GB), 2020-02-26, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  81. Wintour, Sam Jones Patrick (2020-03-06), "Coronavirus cases pass 100,000 globally as Iran threatens force to restrict travel", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  82. Ramin Mostaghim, Mostafa Salem and Tamara Qiblawi CNN. "Iran was already struggling with one crisis. Now it has the worst coronavirus outbreak in the Middle East". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  83. Kirkpatrick, David D.; Fassihi, Farnaz; Mashal, Mujib (2020-02-24), "‘Recipe for a Massive Viral Outbreak’: Iran Emerges as a Worldwide Threat", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  84. Robin Wright. "How Iran Became a New Epicenter of the Coronavirus Outbreak". The New Yorker (kwa en-us). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  85. John Haltiwanger. "8% of Iran's parliament has the coronavirus, and it released 54,000 prisoners as the country descends into chaos". Business Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  86. Stephen Sorace (2020-03-15). "Iran reports biggest single-day jump of coronavirus deaths as president rules out quarantine". Fox News (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  87. "Coronavirus pandemic 'could kill millions' in Iran". www.aljazeera.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  88. "How serious is the coronavirus crisis in Iran?". news.yahoo.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  89. Cunningham, Erin, "As coronavirus cases explode in Iran, U.S. sanctions hinder its access to drugs and medical equipment", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  90. "Iran opens up as economic woes trump virus infection fears". news.yahoo.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  91. Cha, Hyonhee Shin, Sangmi (2020-02-20), "'Like a zombie apocalypse': Residents on edge as coronavirus cases surge in South Korea", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  92. 김수연 (2020-02-29). "42 Shincheonji followers came to S. Korea from virus-hit Wuhan over 8 months: gov't". Yonhap News Agency (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  93. "S Korea declares highest alert over coronavirus", BBC News (kwa en-GB), 2020-02-23, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  94. The Korea Herald (2020-02-21). "Airlines to suspend more flights over coronavirus". www.koreaherald.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  95. Dennis NormileMar. 17, 2020, 8:00 Am (2020-03-17). "Coronavirus cases have dropped sharply in South Korea. What’s the secret to its success?". Science | AAAS (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  96. Bicker, Laura (2020-03-12), "Is S Korea's rapid testing the key to coronavirus?", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  97. "This is how South Korea flattened its coronavirus curve". NBC News (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  98. Suki Kim. "How South Korea Lost Control of Its Coronavirus Outbreak". The New Yorker (kwa en-us). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  99. "South Korea reports lowest number of new cases", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-23, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  100. "South Korea to impose mandatory coronavirus quarantine on all arrivals". news.yahoo.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  101. https://www.usnews.com/news/world/articles/2020-04-01/over-100-countries-ask-south-korea-for-coronavirus-testing-help-official
  102. "South Korea confirms second wave of coronavirus", BBC News (kwa en-GB), 2020-06-22, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  103. Bob Fredericks (2020-03-13). "WHO says Europe is new epicenter of coronavirus pandemic". New York Post (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  104. Roser, Max; Ritchie, Hannah; Ortiz-Ospina, Esteban; Hasell, Joe (2020-03-04). "Coronavirus Pandemic (COVID-19)". Our World in Data. 
  105. "https://twitter.com/megovernment/status/1239992049350447104". Twitter (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  106. Henley, Jon; Oltermann, Philip (2020-03-18), "Italy records its deadliest day of coronavirus outbreak with 475 deaths", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  107. "https://twitter.com/megovernment/status/1264598489318776832". Twitter (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  108. Beachum, Lateshia; Hawkins, Derek; Bellware, Kim; O'Grady, Siobhán; Shaban, Hamza; Kornfield, Meryl; Firozi, Paulina, "Pence claims Biden’s handling of coronavirus would be worse than Trump’s", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  109. Chiara Severgnini e Redazione Online (2020-01-30). "Coronavirus, primi due casi in Italia: sono due turisti cinesi". Corriere della Sera (kwa Kiitaliano). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  110. Amante, Elisa Anzolin, Angelo (2020-02-21), "First Italian dies of coronavirus as outbreak flares in north", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  111. "Coronavirus, in dieci comuni lombardi: 50 mila persone costrette a restare in casa. Quarantena all'ospedale milanese di Baggio". la Repubblica (kwa Kiitaliano). 2020-02-21. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  112. "Coronavirus, decreto del governo: nei comuni focolaio stop ad ingressi ed uscite. Conte: "Non trasformeremo l'Italia in un lazzaretto"". la Repubblica (kwa Kiitaliano). 2020-02-22. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  113. Palermo, Angela Giuffrida Lorenzo Tondo in; Beaumont, Peter (2020-03-04), "Italy orders closure of all schools and universities due to coronavirus", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  114. "All sport in Italy suspended", BBC Sport (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  115. Rome, Eric Sylvers in Milan and Giovanni Legorano in (2020-03-12), "Italy Hardens Nationwide Quarantine", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  116. Greta Privitera (2020-03-09). "Italian doctors on coronavirus frontline face tough calls on whom to save". POLITICO. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  117. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-03-12. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  118. "Italy coronavirus death toll overtakes China". The Independent (kwa Kiingereza). 2020-03-19. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  119. Casaubon says (2020-03-23). "'From Russia with Love': Putin sends aid to Italy to fight virus". www.euractiv.com (kwa en-GB). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  120. Valentina Di Donato, Sheena McKenzie and Livia Borghese CNN. "Italy's coronavirus death toll passes 10,000. Many are asking why the fatality rate is so high". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  121. Justine Coleman (2020-04-19). "Italy sees fewest coronavirus deaths in a week". TheHill (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  122. Linde, Pablo (2020-02-01), "Sanidad confirma en La Gomera el primer caso de coronavirus en España", El País (kwa Kihispania), ISSN 1134-6582, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  123. Manuel Ansede (2020-04-22). "El análisis genético sugiere que el coronavirus ya circulaba por España a mediados de febrero". EL PAÍS (kwa Kihispania). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  124. "Spain poised to tighten coronavirus lockdown after record daily toll". www.msn.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  125. Guy Hedgecoe in Madrid. "‘Top of the curve’? Spain hopes Covid-19 peak reached as deaths pass 4,000". The Irish Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  126. "Britain’s Prince Charles tests positive for Covid-19". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2020-03-25. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  127. Ashley Collman. "Spain recorded 950 coronavirus deaths in a day, the highest single-day toll of any country". Business Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  128. "White House: CDC 'let country down' on testing - COVID-19 updates". www.aljazeera.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  129. Oriol Güell, Elena Sevillano, Pablo Linde (2020-03-18). "Lack of testing hampering Spain’s efforts to slow coronavirus outbreak". EL PAÍS (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  130. "Estudio de seroprevalencia: sólo el 5% de los españoles tiene anticuerpos frente al coronavirus". ELMUNDO (kwa Kihispania). 2020-05-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  131. Europa Press (2020-05-13). "Coronavirus.- El 5% de la población española ha superado el Covid-19". www.europapress.es. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  132. "The U.K. is aiming for deliberate 'herd immunity'". Fortune (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  133. "Scottish health secretary criticises virus messaging", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  134. "Coronavirus: What next in the UK coronavirus fight?", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-23, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  135. editor, Sarah Boseley Health (2020-03-16), "New data, new policy: why UK's coronavirus strategy changed", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  136. Sam Meredith (2020-03-20). "UK PM Boris Johnson announces nationwide lockdown measures, telling cafes, pubs and restaurants to close". CNBC (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  137. "UK to pay wages for workers facing job losses", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-20, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  138. "Strict new curbs on life in UK announced by PM", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-24, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  139. "Large-scale human trial of potential COVID-19 vaccine kicks off at Oxford". www.cbsnews.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  140. Rebecca Gilroy (2020-03-30). "More temporary hospitals announced ready for coronavirus peak". Nursing Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  141. Davies, Caroline (2020-04-03), "Prince Charles to open NHS Nightingale to treat Covid-19 patients", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  142. "Nightingale Hospital in London placed on standby", BBC News (kwa en-GB), 2020-05-04, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  143. "Coronavirus: London's NHS Nightingale 'treated 51 patients'", BBC News (kwa en-GB), 2020-04-27, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  144. "Coronavirus updates: Texas reports single highest daily rate increase of infections". www.msn.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  145. Staff, Reuters (2020-05-04), "After retesting samples, French hospital discovers COVID-19 case from December", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  146. Deslandes, A.; Berti, V.; Tandjaoui-Lambotte, Y.; Alloui, Chakib; Carbonnelle, E.; Zahar, J.R.; Brichler, S.; Cohen, Yves (2020-6). "SARS-CoV-2 was already spreading in France in late December 2019". International Journal of Antimicrobial Agents 55 (6): 106006. ISSN 0924-8579. PMC 7196402 Check |pmc= value (help). PMID 32371096 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/j.ijantimicag.2020.106006.  Check date values in: |date= (help)
  147. "ENQUETE FRANCEINFO. "La majorité des personnes étaient contaminées" : de la Corse à l'outre-mer, comment le rassemblement évangélique de Mulhouse a diffusé le coronavirus dans toute la France". Franceinfo (kwa Kifaransa). 2020-03-28. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  148. "France imposes 15-day lockdown and mobilises 100,000 police to enforce coronavirus restrictions". The Independent (kwa Kiingereza). 2020-03-16. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  149. "etalab-covid19-dashboard". etalab-covid19-dashboard. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  150. McAuley, James, "Violent protests in Paris suburbs reflect tensions under lockdown", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  151. "Coronavirus flare-ups force France to re-close some schools". www.cbsnews.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  152. Leatherby, Lauren; McCann, Allison (2020-05-15), "Sweden Stayed Open. A Deadly Month Shows the Risks.", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  153. Richard Milne (2020-05-08). "Architect of Sweden’s no-lockdown strategy insists it will pay off". www.ft.com (kwa en-GB). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  154. Leatherby, Lauren; McCann, Allison (2020-05-15), "Sweden Stayed Open. A Deadly Month Shows the Risks.", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  155. "Coronavirus: Sweden records highest weekly deaths per capita in Europe". www.yahoo.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  156. Susan Davis for The Bonaire Insider (2020-04-16). "Update on Coronavirus (COVID-19) by Bonaire's Lt. Governor". InfoBonaire (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  157. Trotta, Maria Caspani, Daniel (2020-03-27), "As of Thursday, U.S. had most coronavirus cases in world", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  158. Shumaker, Lisa (2020-04-11), "U.S. coronavirus deaths top 20,000, highest in world exceeding Italy: Reuters tally", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  159. "CSSEGISandData/COVID-19". GitHub (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  160. Holshue, Michelle L.; DeBolt, Chas; Lindquist, Scott; Lofy, Kathy H.; Wiesman, John; Bruce, Hollianne; Spitters, Christopher; Ericson, Keith; Wilkerson, Sara (2020-03-05). "First Case of 2019 Novel Coronavirus in the United States". The New England Journal of Medicine 382 (10): 929–936. ISSN 0028-4793. PMC 7092802 Check |pmc= value (help). PMID 32004427 Check |pmid= value (help). doi:10.1056/NEJMoa2001191. 
  161. 161.0 161.1 161.2 "Trump Declares Coronavirus A Public Health Emergency And Restricts Travel From China". NPR.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  162. District of Columbia 1100 Connecticut Ave NW Suite 1300B Washington, Dc 20036. "PolitiFact - Biden falsely says Trump administration rejected WHO coronavirus test kits (that were never offered)". @politifact (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  163. Whoriskey, Peter; Satija, Neena, "How U.S. coronavirus testing stalled: Flawed tests, red tape and resistance to using the millions of tests produced by the WHO", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  164. "How the CDC’s Restrictive Testing Guidelines Hid the Coronavirus Epid…". archive.li. 2020-03-22. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-03-22. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  165. A. B. C. News. "Washington governor declares state of emergency over virus". ABC News (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  166. Pilkington, Ed (2020-04-04), "How science finally caught up with Trump's playbook – with millions of lives at stake", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  167. finanzen net GmbH. "Trump signs emergency coronavirus package, injecting $8.3 billion into efforts to fight the outbreak | Markets Insider". markets.businessinsider.com (kwa en-us). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  168. Priscilla Alvarez CNN. "Here's what Trump's coronavirus emergency declaration does". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  169. Katie Dowd SFGATE (2020-03-15). "These stores are closing or changing hours due to coronavirus". SFGate (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  170. Lily Altavena, Max Londberg and Justin Murphy. "After coronavirus school closings, will states need to hold kids back, institute summer school?". USA TODAY (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  171. "Coronavirus Maps: How Severe Is Your State's Outbreak?". NPR.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  172. Jr, Donald G. McNeil (2020-03-26), "The U.S. Now Leads the World in Confirmed Coronavirus Cases", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  173. Lori Robertson (2020-04-07). "The HHS Inspector General Report". FactCheck.org (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  174. "2 died with coronavirus weeks before 1st U.S. virus death". PBS NewsHour (kwa en-us). 2020-04-22. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  175. "Global COVID-19 Tracker & Interactive Charts | Real Time Updates & Digestable Information for Everyone | 1Point3Acres". coronavirus.1point3acres.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  176. Times, The New York (2020-07-20), "Covid in the U.S.: Latest Map and Case Count", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  177. Shear, Michael D.; Haberman, Maggie (2020-02-27), "Pence Will Control All Coronavirus Messaging From Health Officials", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  178. "Trump calls for halt to US funding for World Health Organization amid coronavirus outbreak". www.msn.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  179. "Trump Criticizes Fauci’s Warning Against Opening Schools Too Soon In Latest Public Disagreement". Kaiser Health News (kwa en-US). 2020-05-14. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  180. Jasmine Kim (2020-06-25). "Record spikes in U.S. coronavirus cases push up hospitalization rates in 16 states". CNBC (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  181. Stephanie Soucheray | News Reporter | CIDRAP News | Jul 17, 2020. "US sets daily COVID-19 record: 75,000 new cases". CIDRAP (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  182. Luisa Horwitz, Paola Nagovitch, Holly K. Sonnel, Carin Zissis. "The Coronavirus in Latin America". AS/COA (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  183. "Uncollected bodies lie for days in the streets of Ecuador: The emerging epicenter of the coronavirus in Latin America". Stuff (kwa Kiingereza). 2020-04-03. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  184. Afp (2020-05-13). "Superan AL y el Caribe más de 400 mil casos de coronavirus - Mundo - La Jornada". www.jornada.com.mx (kwa Kihispania). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  185. Alex Ward (2020-05-26). "How South America became a coronavirus epicenter". Vox (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  186. Fonseca, Pedro (2020-05-20), "Brazil suffers record coronavirus deaths, Trump mulls travel ban", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  187. Shasta Darlington, Flora Charner, Taylor Barnes and Seán Federico-O'Murchú CNN. "Brazil faces a dark week as Covid-19 toll soars". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  188. "Coronavirus: Could African countries cope with an outbreak?", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-12, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  189. "‘It's just beginning here’: Africa turns to testing as pandemic grips the continent". the Guardian (kwa Kiingereza). 2020-04-26. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  190. correspondent, Jason Burke Africa (2020-08-06), "Total confirmed coronavirus cases in Africa pass 1 million", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  191. Gurman Bhatia, Manas Sharma. "The last places on earth without coronavirus". Reuters (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  192. Silence Charumbira in Maseru (2020-05-13). "Lesotho records first coronavirus case a week after lifting lockdown". the Guardian (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  193. Australian Government Department of Health (2020-01-25). "First confirmed case of novel coronavirus in Australia". Australian Government Department of Health (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  194. "WHO Coronavirus Disease (COVID-19) Dashboard". covid19.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  195. Meghan Roos On 5/20/20 at 1:52 PM EDT (2020-05-20). "U.S. stands with Australia after China threatens economic retribution over coronavirus origins inquiry, Pompeo says". Newsweek (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  196. Anthony Galloway, Eryk Bagshaw (2020-05-19). "China signs on to World Health Assembly inquiry resolution". The Sydney Morning Herald (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  197. Salcedo, Andrea; Yar, Sanam; Cherelus, Gina (2020-07-16), "Coronavirus Travel Restrictions, Across the Globe", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  198. "Coronavirus spikes outside China show travel bans aren’t working". Science (kwa Kiingereza). 2020-02-24. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  199. "Coronavirus spikes outside China show travel bans aren’t working". Science (kwa Kiingereza). 2020-02-24. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  200. Stevis-Gridneff, Matina (2020-02-26), "Coronavirus Nightmare Could Be the End for Europe’s Borderless Dream", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  201. Associated Press. "Countries Evaluate Evacuation of Citizens Amid Wuhan Coronavirus Panic". thediplomat.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  202. "Repatriated citizens to be reunited with families". SAnews (kwa Kiingereza). 2020-03-29. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  203. "Pakistan cancels flights to China as fears of coronavirus spread". Dialogue Pakistan (kwa en-US). 2020-01-31. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-01-31. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  204. Wang, Vivian; Rich, Motoko; Bradsher, Keith (2020-02-15), "Shifting Ground in Coronavirus Fight: U.S. Will Evacuate Americans From Cruise Ship", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  205. "4th batch of 53 Indians evacuated from Iran: S Jaishankar", The Economic Times, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  206. Rebecca Kheel (2020-03-20). "US-led coalition in Iraq drawing down over coronavirus concerns". TheHill (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  207. "Students mobilize aid for Hubei province in China following coronavirus outbreak". The Tufts Daily (kwa Kiingereza). 2020-02-05. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  208. Staff (2020-01-28). "Direct Relief Rushes Facial Masks to China to Fight Coronavirus Spread". Direct Relief (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  209. Lisette Voytko. "Bill And Melinda Gates Donate $100 Million To Coronavirus Vaccine Research And Treatment". Forbes (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  210. https://armenpress.am/eng/news/1003716/
  211. Catalina Ricci S. Madarang (2020-02-06). "Should we thank China for face mask donation when Filipinos donated first?". Interaksyon (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  212. hermesauto (2020-02-19). "Coronavirus: Singapore Red Cross to send $2.3m worth of aid to China, steps up local outreach to seniors". The Straits Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  213. "21 countries donate medical supplies to China: spokesperson - Xinhua | English.news.cn". www.xinhuanet.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-09. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  214. "The United States Announces Assistance To Combat the Novel Coronavirus". United States Department of State (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  215. Joseph Guzman (2020-02-07). "US pledges $100 million to help fight coronavirus in China". TheHill (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  216. MedTech Intelligence Staff (2020-02-26). "U.S. Companies Donate Nearly $27 Million in Medical Products to Aid in COVID-19 Outbreak in China". MedTech Intelligence (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  217. Joe Penney (2020-03-18). "As the U.S. Blames China for the Coronavirus Pandemic, the Rest of the World Asks China for Help". The Intercept (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  218. Staff, Reuters (2020-03-13), "China sends medical supplies, experts to help Italy battle coronavirus", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  219. "Jack Ma Foundation donates masks, testing kits to Africa for coronavirus control". Daily Monitor (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. [dead link]
  220. "Coronavirus: Countries reject Chinese-made equipment", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-30, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  221. Eric Ol, er. "Africans Worry About Quality of Donated Chinese COVID-19 Aid Following Reports of Defective Masks in Europe". The China Africa Project (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  222. "China denies it donated defective COVID-19 kits". www.msn.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  223. "China’s ‘Mask Diplomacy’ Is Faltering. But the U.S. Isn’t Doing Any Better". Time. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  224. "Bloomberg - Are you a robot?". www.bloomberg.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  225. "Here's What Taiwan Told the WHO at the Start of the Virus Outbreak". Time. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  226. Staff, Reuters (2020-01-23), "Wuhan lockdown 'unprecedented', shows commitment to contain virus: WHO representative in China", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  227. "WHO | Pneumonia of unknown cause – China". WHO. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  228. Washington, Peter Beaumont Julian Borger in (2020-04-09), "WHO warned of transmission risk in January, despite Trump claims", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  229. "WHO | Novel Coronavirus – Thailand (ex-China)". WHO. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  230. https://www.washingtonpost.com/politics/2020/04/17/trumps-false-claim-that-who-said-coronavirus-was-not-communicable/
  231. "WHO says global risk of China virus is 'high' | The Star". www.thestar.com.my. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  232. "Statement on the second meeting of the International Health Regulations (2005) Emergency Committee regarding the outbreak of novel coronavirus (2019-nCoV)". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  233. "Coronavirus declared global health emergency", BBC News (kwa en-GB), 2020-01-31, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  234. "WHO Director-General's remarks at the media briefing on 2019-nCoV on 11 February 2020". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  235. "World must prepare for pandemic, says WHO", BBC News (kwa en-GB), 2020-02-25, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  236. Berkeley Lovelace Jr (2020-02-28). "WHO raises coronavirus threat assessment to its highest level: 'Wake up. Get ready. This virus may be on its way'". CNBC (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  237. "WHO Director-General's opening remarks at the media briefing on COVID-19 - 11 March 2020". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  238. Sandy Tolliver (2020-03-17). "China and the WHO's chief: Hold them both accountable for pandemic". TheHill (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  239. "WashU Expert: Coronavirus far greater threat than SARS to global supply chain | The Source | Washington University in St. Louis". The Source (kwa en-US). 2020-02-07. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  240. Rob McLean, Laura He and Anneken Tappe, CNN Business. "Dow plunges 1,000 points, posting its worst day in two years as coronavirus fears spike". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  241. Anneken Tappe, CNN Business. "Dow falls 1,191 points -- the most in history". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  242. Sunny Oh. "Stocks record worst week since financial crisis as coronavirus concerns heat up". MarketWatch (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  243. "Scope Ratings GmbH". Scope Ratings. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  244. Callum Keown. "Global insurers face losses of $204 billion from Coronavirus, more than 9/11 and 2017 hurricanes, says Lloyd’s of London". MarketWatch (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  245. "Collapsed Flybe: 'Do not travel to the airport'", BBC News (kwa en-GB), 2020-03-05, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  246. Brook Turner (2020-04-03). "'Most significant crisis in the history of travel': where to now for tourism?". The Sydney Morning Herald (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  247. Reuters New DelhiFebruary 27, 2020UPDATED: February 28, 2020 18:58 Ist. "Coronavirus scare: Complete list of airlines suspending flights". India Today (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  248. Kong, Mike Cherney in Sydney and Lucy Craymer in Hong (2020-05-05), "You’ve Got Mail...Finally: The Pandemic Is Jamming Up the World’s Post", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  249. "Coronavirus Resources for Retailers". NRF (kwa Kiingereza). Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-05-14. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  250. "How Retailers Globally are Responding to Coronavirus". Aislelabs (kwa en-US). 2020-04-02. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-05-14. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  251. Danny Santos (2020-03-23). "How Shopping Centres Globally are Responding to Coronavirus (Updated Frequently)". Aislelabs (kwa en-US). Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-05-08. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  252. James Brownsell. "Half the world's workers face losing their jobs, says ILO". www.aljazeera.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  253. Romm, Tony, "Americans have filed more than 40 million jobless claims in past 10 weeks, as another 2.1 million filed for benefits last week", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  254. Ignacio Fariza (2020-04-03). "La pandemia amenaza con dejar entre 14 y 22 millones de personas más en pobreza extrema en Latinoamérica". EL PAÍS (kwa Kihispania). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  255. "Updated estimates of the impact of COVID-19 on global poverty". blogs.worldbank.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  256. Peter Fabricius for ISS TODAY (2020-04-30). "ISS TODAY: Is Covid-19 enabling debt-trap diplomacy?". Daily Maverick (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  257. Salem Solomon (2020-06-03). "Africa: China-Africa Blanket Debt Forgiveness Not in the Cards". allAfrica.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  258. "Pandemic reveals rifts in China-Africa relations". www.efe.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  259. Kelly Tyko, Jessica Guynn and Mike Snider. "Coronavirus fears empty store shelves of toilet paper, bottled water, masks as shoppers stock up". USA TODAY (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  260. Yuen, Kum Fai; Wang, Xueqin; Ma, Fei; Li, Kevin X. (2020-5). "The Psychological Causes of Panic Buying Following a Health Crisis". International Journal of Environmental Research and Public Health 17 (10). ISSN 1661-7827. PMC 7277661 Check |pmc= value (help). PMID 32443427 Check |pmid= value (help). doi:10.3390/ijerph17103513.  Check date values in: |date= (help)
  261. Strumpf, Dan (2020-01-31), "Tech Sector Fears Supply Delays as Effects of Virus Ripple Through China", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  262. "WHO warns of global shortage of face masks and protective suits". the Guardian (kwa Kiingereza). 2020-02-07. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  263. "Shortage of personal protective equipment endangering health workers worldwide". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  264. "Corona snijdt ook in het vlees van de drugsmaffia". De Standaard (kwa nl-BE). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  265. correspondent, Jamie Grierson Home affairs (2020-04-12), "Coronavirus triggers UK shortage of illicit drugs", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  266. Isabel Vincent (2020-03-28). "Coronavirus pandemic drives up price of heroin, meth and fentanyl". New York Post (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  267. Maximo Torero. "How to Stop a Looming Food Crisis". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  268. "World risks 'biblical' famines due to pandemic - UN", BBC News (kwa en-GB), 2020-04-21, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  269. "Senior Officials Sound Alarm over Food Insecurity, Warning of Potentially ‘Biblical’ Famine, in Briefings to Security Council | Meetings Coverage and Press Releases". www.un.org. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  270. Reed, Stanley (2020-02-03), "OPEC Scrambles to React to Falling Oil Demand From China", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  271. "US oil prices turn negative as demand dries up", BBC News (kwa en-GB), 2020-04-21, iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  272. "Here are the museums that have closed (so far) due to coronavirus". www.theartnewspaper.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-03-29. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  273. Daniel Burke, CNN Religion Editor. "What churches, mosques and temples are doing to fight the spread of coronavirus". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  274. Joey Hadden, Laura Casado. "Here are the latest major events that have been canceled or postponed because of the coronavirus outbreak, including the 2020 Tokyo Olympics, Burning Man, and the 74th Annual Tony Awards". Business Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  275. Daniel Burke, CNN Religion Editor. "What churches, mosques and temples are doing to fight the spread of coronavirus". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  276. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21.  Unknown parameter |= ignored (help)
  277. By Jomana Karadsheh and Tamara Qiblawi CNN. "'Unprecedented' Hajj begins -- with 1,000 pilgrims, rather than the usual 2 million". CNN (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  278. "Tokyo 2020 Olympics postponed until 2021", BBC Sport (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  279. "NHL statement on coronavirus". NHL.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  280. David Close, Amanda Jackson and Jason Hanna CNN. "NBA suspends season after Jazz center Rudy Gobert tests positive for coronavirus". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  281. "Premier League coronavirus announcement: 2019/20 season suspended after cases at Chelsea, Arsenal & others". Squawka (kwa en-GB). 2020-03-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  282. UEFA.com (2020-03-15). "All of this week's UEFA matches postponed | Inside UEFA". UEFA.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  283. "Coronavirus brings entertainment world to a standstill". AP NEWS. 2020-03-12. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  284. Taylor Romine, Eric Levenson and Javi Morgado CNN. "Broadway theaters to suspend all performances because of coronavirus". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  285. Savage, Mark (2020-03-18), "Eurovision Song Contest cancelled over coronavirus", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-11 
  286. Wayne Alan Brenner, 5:30PM, Sun Mar. 15, 2020. "The Social Distancing Festival Is Live Online". www.austinchronicle.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  287. Margot Harris. "Coronavirus memes are spreading as the disease travels across the world — here's what they look like and why creators say they're important". Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-11. 
  288. "Federal government announces aggressive measures to battle COVID-19 as parliament suspended until April". National Post (kwa en-CA). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  289. Darcy Palder, Amy Mackinnon. "Coronavirus in the Corridors of Power". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  290. Corasaniti, Nick; Saul, Stephanie (2020-08-10), "16 States Have Postponed Primaries During the Pandemic. Here’s a List.", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  291. Proctor, Kate (2020-03-29), "Michael Gove appears to blame China over lack of UK coronavirus testing", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  292. Colum Lynch, Robbie Gramer. "U.S. and China Turn Coronavirus Into a Geopolitical Football". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  293. Bill Bostock. "China sacked a brace of top officials in Hubei province, likely in a move to protect Xi Jinping from people's anger over the coronavirus outbreak". Business Insider. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  294. Barnes, Julian E. (2020-04-16), "C.I.A. Hunts for Authentic Virus Totals in China, Dismissing Government Tallies", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  295. Miller, Claire Cain (2020-04-11), "Could the Pandemic Wind Up Fixing What’s Broken About Work in America?", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  296. Ian Swanson (2020-05-02). "Five ways the coronavirus could change American politics". TheHill (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  297. Haberman, Maggie; Martin, Jonathan (2020-03-12), "Trump’s Re-election Chances Suddenly Look Shakier", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  298. "Coronavirus: Anti-lockdown protests grow across US - BBC News". web.archive.org. 2020-04-17. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-04-17. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  299. www.spectator.co.uk https://www.spectator.co.uk/article/how-coronavirus-derailed-the-largest-nato-exercise-in-25-years. Iliwekwa mnamo 2020-09-21.  Missing or empty |title= (help)
  300. Cunningham, Erin; Bennett, Dalton, "Coronavirus pummels Iran leadership as data show spread is far worse than reported", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  301. Staff, Reuters (2020-03-14), "U.S. sanctions 'severely hamper' Iran coronavirus fight, Rouhani says", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  302. Robbie Gramer, Jack Detsch, Dan Haverty. "Coronavirus Pandemic Forces a Cease-Fire in Yemen". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  303. William Sposato. "Japan and Korea Won't Let A Pandemic Stop Them Fighting". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  304. Farrer, Justin McCurry Martin (2020-03-06), "Coronavirus quarantine plans ignite row between South Korea and Japan", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  305. Suki Kim. "How South Korea Lost Control of Its Coronavirus Outbreak". The New Yorker (kwa en-us). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  306. Walker, Shaun (2020-03-31), "Authoritarian leaders may use Covid-19 crisis to tighten their grip", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  307. A. B. C. News. "Some leaders use pandemic to sharpen tools against critics". ABC News (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  308. hermesauto (2020-04-10). "Asia cracks down on coronavirus 'fake news'". The Straits Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  309. Jacob Mchangama, Sarah McLaughlin. "Coronavirus Has Started a Censorship Pandemic". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  310. https://plus.google.com/+UNESCO (2020-03-04). "Education: From disruption to recovery". UNESCO (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  311. https://plus.google.com/+UNESCO (2020-03-04). "Education: From disruption to recovery". UNESCO (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  312. https://plus.google.com/+UNESCO (2020-03-04). "Education: From disruption to recovery". UNESCO (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  313. "May 2020 examinations will no longer be held". International Baccalaureate® (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  314. Jamerson, Josh Mitchell and Joshua (2020-03-20), "Student-Loan Debt Relief Offers Support to an Economy Battered by Coronavirus", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  315. "'Clear as mud': schools ask for online learning help as coronavirus policy confusion persists". the Guardian (kwa Kiingereza). 2020-03-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  316. "Schools Race To Feed Students Amid Coronavirus Closures". NPR.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  317. BEN SESSOMS bsessoms@statesville.com. "Homeless students during the coronavirus pandemic: 'We have to make sure they're not forgotten'". Statesville.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  318. "Coronavirus Forces Families to Make Painful Childcare Decisions". Time. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  319. Bao, Xue; Qu, Hang; Zhang, Ruixiong; Hogan, Tiffany P. (2020/1). "Modeling Reading Ability Gain in Kindergarten Children during COVID-19 School Closures". International Journal of Environmental Research and Public Health (kwa Kiingereza) 17 (17): 6371. doi:10.3390/ijerph17176371.  Check date values in: |date= (help)
  320. https://plus.google.com/+UNESCO (2020-03-10). "Adverse consequences of school closures". UNESCO (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  321. Jared Lindzon (2020-03-12). "School closures are starting, and they’ll have far-reaching economic impacts". Fast Company (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  322. Garcia, Santiago; Albaghdadi, Mazen S.; Meraj, Perwaiz M.; Schmidt, Christian; Garberich, Ross; Jaffer, Farouc A.; Dixon, Simon; Rade, Jeffrey J.; Tannenbaum, Mark (2020-06-09). "Reduction in ST-Segment Elevation Cardiac Catheterization Laboratory Activations in the United States During COVID-19 Pandemic". Journal of the American College of Cardiology (kwa Kiingereza) 75 (22): 2871. PMID 32283124 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/j.jacc.2020.04.011. 
  323. "Covid phobia keeping people with heart symptoms away from ERs". STAT (kwa en-US). 2020-04-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  324. Jeremy Samuel Faust (2020-04-28). "Medication Shortages Are the Next Crisis". The Atlantic (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  325. Jamie Wareham. "U.K. Lockdown Has ‘Broken HIV Chain’ With Huge Reduction In New STI Cases". Forbes (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  326. Alice Klein. "Australia sees huge decrease in flu cases due to coronavirus measures". New Scientist (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  327. "Weekly U.S. Influenza Surveillance Report | CDC". www.cdc.gov (kwa en-us). 2020-09-18. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  328. Nylah Burton (2020-02-07). "The coronavirus exposes the history of racism and "cleanliness"". Vox (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  329. "Fears of coronavirus trigger anti-China sentiment worldwide". koreatimes (kwa Kiingereza). 2020-02-02. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  330. Smith, Nicola; Torre, Giovanni (2020-02-01), "Anti-Chinese racism spikes as virus spreads globally", The Telegraph (kwa en-GB), ISSN 0307-1235, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  331. Gorce, Tammy La (2020-04-10), "Chinese-Americans, Facing Abuse, Unite to Aid Hospitals in Coronavirus Battle", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  332. Tavernise, Sabrina; Jr, Richard A. Oppel (2020-06-02), "Spit On, Yelled At, Attacked: Chinese-Americans Fear for Their Safety", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  333. "Hunt for racist coronavirus attackers: Police release CCTV after assault". ITV News (kwa Kiingereza). 2020-03-04. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  334. Nadeau, Barbie Latza (2020-02-29), "Italy Shows Just How Crazy Coronavirus Panic Can Get", The Daily Beast (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  335. Namrata Kolachalam (2020-04-09). "Indian Muslims Are Being Scapegoated for the Coronavirus". Slate Magazine (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  336. "Violence flares in tense Paris suburbs as heavy-handed lockdown stirs ‘explosive cocktail’". France 24 (kwa Kiingereza). 2020-04-21. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  337. "Covid-19 Fueling Anti-Asian Racism and Xenophobia Worldwide". Human Rights Watch (kwa Kiingereza). 2020-05-12. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  338. "Covid-19 Backlash Targets LGBT People in South Korea". Human Rights Watch (kwa Kiingereza). 2020-05-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  339. Kwasi Gyamfi Asiedu. "After enduring months of lockdown, Africans in China are being targeted and evicted from apartments". Quartz Africa (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  340. Jenni Marsh CNN. "Beijing faces a diplomatic crisis after reports of mistreatment of Africans in China causes outrage". CNN. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  341. Akinwotu, Jason Burke Emmanuel; Beijing, and Lily Kuo in (2020-04-27), "China fails to stop racism against Africans over Covid-19", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  342. "China’s African traders try to move on from Covid-19 racism and business ruin". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2020-06-26. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  343. "Major Publishers Take Down Paywalls for Coronavirus Coverage" (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  344. "Coronavirus (COVID-19): sharing research data | Wellcome". wellcome.org. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  345. "Coronavirus Research Is Moving at Top Speed—With a Catch", Wired (kwa en-us), ISSN 1059-1028, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  346. Monitoring, B. B. C. (2020-01-30), "China coronavirus: Misinformation spreads online", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  347. "Disinformation and coronavirus". www.lowyinstitute.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  348. Jessica McDonald (2020-01-24). "Social Media Posts Spread Bogus Coronavirus Conspiracy Theory". FactCheck.org (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  349. Elise Thomas. "As the Coronavirus Spreads, Conspiracy Theories Are Going Viral Too". Foreign Policy (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  350. "'American coronavirus': China pushes propaganda casting doubt on virus origin". the Guardian (kwa Kiingereza). 2020-03-13. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  351. Stubbs, Raphael Satter, Robin Emmott, Jack (2020-04-25), "China pressured EU to drop COVID disinformation criticism: sources", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  352. Ashwanee Budoo. "Controls to manage fake news in Africa are affecting freedom of expression". The Conversation (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  353. https://www.theguardian.com/media/2020/apr/08/influencers-being-key-distributors-of-coronavirus-fake-news
  354. https://www.theguardian.com/world/2020/mar/31/coronavirus-covid-19-fake-tests-cures
  355. https://www.theguardian.com/world/2020/apr/16/as-coronavirus-spreads-around-the-world-so-too-do-the-quack-cures
  356. https://www.independent.co.uk/news/world/middle-east/iran-coronavirus-us-target-country-special-version-covid19-a9417206.html
  357. https://www.bbc.com/news/technology-51646309
  358. https://www.lowyinstitute.org/the-interpreter/disinformation-and-coronavirus
  359. 359.0 359.1 359.2 Erin H, ley, wires (2020-01-29). "From fish market to global pandemic: Key dates in the coronavirus outbreak". ABC News (kwa en-AU). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  360. 360.0 360.1 "Who is 'patient zero' in the coronavirus outbreak? - BBC Future". web.archive.org. 2020-02-26. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-26. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  361. Huang, Chaolin; Wang, Yeming; Li, Xingwang; Ren, Lili; Zhao, Jianping; Hu, Yi; Zhang, Li; Fan, Guohui; Xu, Jiuyang (2020). "Clinical features of patients infected with 2019 novel coronavirus in Wuhan, China". Lancet (London, England) 395 (10223): 497–506. ISSN 0140-6736. PMC 7159299 Check |pmc= value (help). PMID 31986264 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/S0140-6736(20)30183-5. 
  362. "Q&A on coronaviruses (COVID-19)". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  363. "Coronavirus disease (COVID-19) – World Health Organization". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  364. Li, Xingguang; Zai, Junjie; Zhao, Qiang; Nie, Qing; Li, Yi; Foley, Brian T.; Chaillon, Antoine (2020-03-11). "Evolutionary history, potential intermediate animal host, and cross‐species analyses of SARS‐CoV‐2". Journal of Medical Virology. ISSN 0146-6615. PMC 7228310 Check |pmc= value (help). PMID 32104911 Check |pmid= value (help). doi:10.1002/jmv.25731. 
  365. Huang, Chaolin; Wang, Yeming; Li, Xingwang; Ren, Lili; Zhao, Jianping; Hu, Yi; Zhang, Li; Fan, Guohui; Xu, Jiuyang (2020). "Clinical features of patients infected with 2019 novel coronavirus in Wuhan, China". Lancet (London, England) 395 (10223): 497–506. ISSN 0140-6736. PMC 7159299 Check |pmc= value (help). PMID 31986264 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/S0140-6736(20)30183-5. 
  366. "Who is 'patient zero' in the coronavirus outbreak? - BBC Future". web.archive.org. 2020-02-26. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-26. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  367. Huang, Chaolin; Wang, Yeming; Li, Xingwang; Ren, Lili; Zhao, Jianping; Hu, Yi; Zhang, Li; Fan, Guohui; Xu, Jiuyang (2020). "Clinical features of patients infected with 2019 novel coronavirus in Wuhan, China". Lancet (London, England) 395 (10223): 497–506. ISSN 0140-6736. PMC 7159299 Check |pmc= value (help). PMID 31986264 Check |pmid= value (help). doi:10.1016/S0140-6736(20)30183-5. 
  368. "Xinhua Headlines: Chinese doctor recalls first encounter with mysterious virus - Xinhua | English.news.cn". www.xinhuanet.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-04-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  369. "独家|新冠病毒基因测序溯源:警报是何时拉响的_政经频道_财新网". web.archive.org. 2020-02-27. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  370. "Ringing the alarm - Global Times". www.globaltimes.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  371. "Xinhua Headlines: Chinese doctor recalls first encounter with mysterious virus - Xinhua | English.news.cn". www.xinhuanet.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-04-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  372. "Timeline of the COVID-19 pandemic in 2019", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-21, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  373. "独家|新冠病毒基因测序溯源:警报是何时拉响的_政经频道_财新网". web.archive.org. 2020-02-27. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  374. "Xinhua Headlines: Chinese doctor recalls first encounter with mysterious virus - Xinhua | English.news.cn". www.xinhuanet.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-04-23. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  375. "Timeline of the COVID-19 pandemic in 2019", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2020-09-21, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  376. "她最早发现新冠肺炎疫情苗头 第一时间上报可疑病例-中工民生-中工网". society.workercn.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  377. "独家|新冠病毒基因测序溯源:警报是何时拉响的_政经频道_财新网". web.archive.org. 2020-02-27. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  378. "独家|新冠病毒基因测序溯源:警报是何时拉响的_政经频道_财新网". web.archive.org. 2020-02-27. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  379. "Promed Post – ProMED-mail" (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  380. "武汉市卫生健康委员会". web.archive.org. 2020-01-09. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-01-09. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  381. "27 cases of viral pneumonia reported in central China's Wuhan City". news.cgtn.com (kwa Kiingereza). Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-03-10. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  382. "Hong Kong takes emergency steps as mystery ‘pneumonia’ infects 27 in Wuhan". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2019-12-31. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  383. "独家|新冠病毒基因测序溯源:警报是何时拉响的_政经频道_财新网". web.archive.org. 2020-02-27. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-27. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  384. "CHP closely monitors cluster of pneumonia cases on Mainland". www.info.gov.hk. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  385. "[新闻直播间]湖北武汉发现不明原因肺炎 国家卫健委专家组已抵达武汉_CCTV节目官网-CCTV-13_央视网(cctv.com)". tv.cctv.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  386. "Promed Post – ProMED-mail" (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  387. Borger, Julian (2020-04-18), "Caught in a superpower struggle: the inside story of the WHO's response to coronavirus", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  388. "Hong Kong takes emergency steps as mystery ‘pneumonia’ infects 27 in Wuhan". South China Morning Post (kwa Kiingereza). 2019-12-31. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  389. Deutsche Welle (www.dw.com). "China investigates SARS-like virus as dozens struck by pneumonia | DW | 31.12.2019". DW.COM (kwa en-GB). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  390. Staff, Reuters (2019-12-31), "Chinese officials investigate cause of pneumonia outbreak in Wuhan", Reuters (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  391. Shear, Michael D.; Goodnough, Abby; Kaplan, Sheila; Fink, Sheri; Thomas, Katie; Weiland, Noah (2020-04-01), "The Lost Month: How a Failure to Test Blinded the U.S. to Covid-19", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  392. Harris, Shane; Miller, Greg; Dawsey, Josh; Nakashima, Ellen, "U.S. intelligence reports from January and February warned about a likely pandemic", Washington Post (kwa en-US), ISSN 0190-8286, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  393. Hegarty, Stephanie (2020-02-06), "The Chinese doctor who tried to warn about coronavirus", BBC News (kwa en-GB), iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  394. The Thaiger (2020-01-09). "Chinese scientists identify the 'Wuhan Virus'. Screening continues on Thai-bound flights.". The Thaiger (kwa en-TH). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  395. Lisa Schnirring | News Editor | CIDRAP News | Jan 11, 2020. "China releases genetic data on new coronavirus, now deadly". CIDRAP (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  396. "China didn't warn public of likely pandemic for 6 key days". AP NEWS. 2020-04-15. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  397. 郭凯. "Chinese premier stresses curbing viral pneumonia epidemic". www.chinadaily.com.cn. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  398. Kuo, Lily (2020-01-21), "China confirms human-to-human transmission of coronavirus", The Guardian (kwa en-GB), ISSN 0261-3077, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  399. 박상수 (2020-01-20). "S. Korea reports 1st confirmed case of China coronavirus". Yonhap News Agency (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  400. Shear, Michael D.; Goodnough, Abby; Kaplan, Sheila; Fink, Sheri; Thomas, Katie; Weiland, Noah (2020-04-01), "The Lost Month: How a Failure to Test Blinded the U.S. to Covid-19", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  401. 401.0 401.1 Chinazzi, Matteo; Davis, Jessica T.; Ajelli, Marco; Gioannini, Corrado; Litvinova, Maria; Merler, Stefano; Piontti, Ana Pastore y; Mu, Kunpeng; Rossi, Luca (2020-04-24). "The effect of travel restrictions on the spread of the 2019 novel coronavirus (COVID-19) outbreak". Science (New York, N.y.) (kwa Kiingereza) 368 (6489): 395. PMID 32144116 Check |pmid= value (help). doi:10.1126/science.aba9757. 
  402. Thomson Reuters Foundation. "France declares first two confirmed cases of coronavirus". news.trust.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-08-31. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  403. Chin, Josh (2020-01-28), "Wuhan Mayor Says Beijing Rules Partially Responsible for Lack of Transparency", Wall Street Journal (kwa en-US), ISSN 0099-9660, iliwekwa mnamo 2020-09-21 
  404. "Statement on the second meeting of the International Health Regulations (2005) Emergency Committee regarding the outbreak of novel coronavirus (2019-nCoV)". www.who.int (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  405. Doug Stanglin. "Federal quarantine order issued for 195 Americans who returned from China". USA TODAY (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  406. Matt Kawahara (2020-04-22). "First known U.S. coronavirus death occurred on Feb. 6 in Santa Clara County". SFChronicle.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  407. "Two die of coronavirus in Iran, first fatalities in Middle East". www.aljazeera.com. Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 
  408. "Coronavirus: Number of COVID-19 deaths in Italy surpasses China as total reaches 3,405". Sky News (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-09-21. 

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: