"Mwana wa Mungu" ni jina linalotumiwa katika dini mbalimbali ili kusisitiza uhusiano wa mtu fulani na Mungu au mmojawapo wa miungu. Kwa maana hiyo lilitumika hasa kwa ajili ya watawala.

Mungu Baba na Roho Mtakatifu pamoja na mtoto Yesu kadiri ya Murillo, 1670 hivi.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Pengine linamaanisha viumbe vingine, kama vile malaika.

Katika Biblia hariri

Katika Biblia ya Kikristo jina hilo linamhusu kwa namna ya pekee sana Yesu, na katika madhehebu karibu yote ya Ukristo linafafanuliwa kumaanisha asili yake ya milele katika Mungu pekee kabla ya kujifanya binadamu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kwa njia ya Bikira Maria.[1]

 
Ukurasa wa kwanza wa Injili ya Marko: "Mwanzo wa habari njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu", karne ya 14.

Kadiri ya Injili, Yesu Kristo mwenyewe alisisitiza mara nyingi uhusiano wake wa pekee na Baba wa mbinguni kutokana na asili yake toka juu, tofauti na ile ya watu wengine wote.

 
Kupaa Bwana kadiri ya Pietro Perugino (1500 hivi), Lyon, Ufaransa.

Kila mmoja kwa namna yake, Mtume Paulo, Wainjili na waandishi wengine wa Agano Jipya walitumia sana jina hilo, hata kuliweka pembeni kidogo jina lingine lililotumiwa sana na Yesu mwenyewe, yaani Mwana wa Adamu.

Katika historia ya Kanisa hariri

Jina hilo lilizidi kutafsiriwa kwa namna tofauti kadiri teolojia ilivyostawi, hasa baada ya kaisari Konstantino Mkuu kuruhusu Ukristo katika Dola la Roma (313).

Kutokana na fujo zilizojitoleza hata kuhatarisha amani ya dola, mwenyewe, akishirikiana na Papa Silvesta I, aliitisha mtaguso mkuu wa kwanza uliofanyika mwaka 325 huko Nisea.

Mtaguso huo ulitunga kanuni ya imani iliyokiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu kwa maana ana hali moja na Mungu Baba, hakuumbwa bali alizaliwa naye tangu milele yote.

 
Konstantino Mkuu na mababu wa Mtaguso wa kwanza wa Nisea.

Wakristo wanapomkiri Yesu kuwa Mwana pekee wa Mungu maana yake ni kwamba, kabla hajazaliwa kama mtu duniani ni Mungu, sawa na Baba anayemzaa yeye tu tangu milele. “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu… Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu… Amwaminiye yeye hahukumiwi, asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu” (Yoh 1:1,14; 3:18).

Msimamo wa Uislamu hariri

Uislamu unamheshimu Yesu kama nabii mmojawapo, lakini unakanusha kabisa jina hilo na maana yake yoyote ili kusisitiza upekee wa Mungu.[2][3]

Tanbihi hariri

  1. Catholic Encyclopedia: Son of God
  2. Jesus: A Brief History by W. Barnes Tatum 2009 ISBN 1-4051-7019-0 page 217
  3. The new encyclopedia of Islam by Cyril Glassé, Huston Smith 2003 ISBN 0-7591-0190-6 page 86

Marejeo hariri

  • Borgen, Peder. Early Christianity and Hellenistic Judaism. Edinburgh: T & T Clark Publishing. 1996.
  • Brown, Raymond. An Introduction to the New Testament. New York: Doubleday. 1997.
  • Essays in Greco-Roman and Related Talmudic Literature. ed. by Henry A. Fischel. New York: KTAV Publishing House. 1977.
  • Dunn, J. D. G., Christology in the Making, London: SCM Press. 1989.
  • Ferguson, Everett. Backgrounds in Early Christianity. Grand Rapids: Eerdmans Publishing. 1993.
  • Greene, Colin J. D. Christology in Cultural Perspective: Marking Out the Horizons. Grand Rapids: InterVarsity Press. Eerdmans Publishing. 2003.
  • Holt, Bradley P. Thirsty for God: A Brief History of Christian Spirituality. Minneapolis: Fortress Press. 2005.
  • Josephus, Flavius. Complete Works. trans. and ed. by William Whiston. Grand Rapids: Kregel Publishing. 1960.
  • Letham, Robert. The Work of Christ. Downers Grove: InterVarsity Press. 1993.
  • Macleod, Donald. The Person of Christ. Downers Grove: InterVarsity Press. 1998.
  • McGrath, Alister. Historical Theology: An Introduction to the History of Christian Thought. Oxford: Blackwell Publishing. 1998.
  • Neusner, Jacob. From Politics to Piety: The Emergence of Pharisaic Judaism. Providence, R. I.: Brown University. 1973.
  • Norris, Richard A. Jr. The Christological Controversy. Philadelphia: Fortress Press. 1980.
  • O'Collins, Gerald. Christology: A Biblical, Historical, and Systematic Study of Jesus. Oxford:Oxford University Press. 2009.
  • Pelikan, Jaroslav. Development of Christian Doctrine: Some Historical Prolegomena. London: Yale University Press. 1969.
  • _______ The Emergence of the Catholic Tradition (100-600). Chicago: University of Chicago Press. 1971.
  • Schweitzer, Albert. Quest of the Historical Jesus: A Critical Study of the Progress from Reimarus to Wrede. trans. by W. Montgomery. London: A & C Black. 1931.
  • Tyson, John R. Invitation to Christian Spirituality: An Ecumenical Anthology. New York: Oxford University Press. 1999.
  • Wilson, R. Mcl. Gnosis and the New Testament. Philadelphia: Fortress Press. 1968.
  • Witherington, Ben III. The Jesus Quest: The Third Search for the Jew of Nazareth. Downers Grove: InterVarsity Press. 1995.
  • _______ “The Gospel of John.” in The Dictionary of Jesus and the Gospels. ed. by Joel Greene, Scot McKnight and I. Howard
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwana wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.