Filipo (kwa Kigiriki Φίλιππος, Philippos) ni jina la mfuasi wa Yesu Kristo anayeshika nafasi ya tano katika orodha zote nne za Mitume wa Yesu katika Agano Jipya.

Kifodini cha Mt. Filippo, 1639, José de Ribera.
Kaburi la Mtume Filipo huko Hierapoli.
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu na Kanisa Katoliki na madhehebu mengine yote ya Ukristo yanayokubali heshima hiyo, lakini kwa tarehe tofauti. Kwa Wakatoliki ni tarehe 3 Mei[1]

Maisha hariri

Habari zake zinapatikana hasa katika Injili na Matendo ya Mitume.

Mtu wa Bethsaida, kama Mtume Petro, alikuwa mfuasi wa Yohane Mbatizaji alipoitwa na Yesu amfuate.

Ndiye aliyemletea rafiki yake Natanaeli wa Kana (Injili ya Yohane 1:43-46).

Baadaye aliulizwa na Kristo bei ya mikate inayohitajiwa na umati kabla hajawazidishia ile michache iliyokuwepo (Yoh 6:5-7}.

Pia alimletea Yesu Wagiriki ambao walifika Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka wakataka kumfahamu (Yoh 12:20-22).

Hatimaye, katika karamu ya mwisho ya Yesu na mitume wake alimuomba awaonyeshe Baba (Yoh 14:8) akalaumiwa naye kwa kutomtambua ndani yake (Yoh. 14:9).

Eusebi wa Kaisarea, katika Historia ecclesiastica, iii.39, aliripoti maneno ya Papias, askofu wa Hierapoli kwamba Filipo alikuwa na mke na watoto na kwamba alifia dini Hierapolis (mwaka 80 hivi).

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Marejeo hariri

  • Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtume Filipo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.