Palau (kwa Kipalau: Belau) ni nchi ya visiwani ya Mikronesia katika Bahari ya Pasifiki. Iko takriban km 500 upande wa mashariki wa Ufilipino.

Jamhuri ya Palau
Beluu er a Belau
Bendera ya Palau [[Picha:|110px|Nembo ya Palau]]
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa: Belau loba klisiich er a kelulul
Lokeshen ya Palau
Mji mkuu Melekeok1
7°21′ N 134°28′ E
Mji mkubwa nchini Koror
Lugha rasmi Kiingereza, Kipalau, Kijapani (kisiwani Angaur)
Serikali Jamhuri
inayoshirikiana na Marekani

Johnson Toribiong
Uhuru
Tarehe
1 Oktoba 1994
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
466 km² (ya 195)
--
Idadi ya watu
 - Julai 2021 kadirio
 - 2020 sensa
 - Msongamano wa watu
 
18,024 (ya 192)
17,614
38.4/km² (ya 155)
Fedha US Dollar (USD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+9)
(UTC)
Intaneti TLD .pw
Kodi ya simu +680

-

1 Tar. 7 Oktoba 2006 ofisi za serikali zilihamia Melekeok kutoka Koror mji mkuu wa awali. 2  Jumla la pato la taifa pamoja na msaada wa Marekani (2001)



Ramani ya Palau

Jumla kuna visiwa 250 hadi 350: idadi inategemea namna gani mtazamaji anapendelea kuhesabu sehemu ya nchi kavu kuwa kisiwa kufuatana na ukubwa au udogo wake. Visiwa tisa vimekaliwa na watu na kisiwa kikubwa chenye km² 331 ni Babelthuap.

Hadi mwaka 1994 ilikuwa nchi lindwa chini ya Marekani kwa niaba ya Umoja wa Mataifa. Marekani inaendelea kuwajibika kwa mambo ya kijeshi kufuatana na mkataba uliofanywa baada ya uhuru.

Mji mkuu ni Melekeok kwenye kisiwa cha Babelthuap.

Wakazi ni 18,000 hivi, ambao 65.2% ni wenyeji wenye asili mchanganyiko kutoka visiwa vya Pasifiki, na 31.6% wametokea Asia, hasa Ufilipino.

Kuna lugha tano ambazo huzungumzwa nchini Palau. Lugha rasmi ni Kipalau na Kiingereza.

Upande wa dini, 78.7% ni Wakristo (46.9% ni Wakatoliki, 25.9% Waprotestanti mbali ya 5% ambao ni Waadventista Wasabato). 5.1% wanafuata dini ya Modekngei ambayo inachanganya Ukristo na dini ya jadi. 4.9% ni Waislamu.

Mikoa 16 ya Palau

Tazama pia hariri


  Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.