Polynesia ya Kifaransa

Polinesia ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Polynésie française; kwa Kitahiti: Pōrīnetia Farāni) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa katika Pasifiki ya kusini. Eneo lake ni mafunguvisiwa mbalimbali ya Polinesia.

Polynesia ya Kifaransa


Kisiwa kinachojulikana zaidi ni Tahiti pamoja na mji mkuu wake wa Papeete ambayo ni pia mji mkuu wa eneo lote.

Jiografia hariri

 
Ramani ya Polinesia ya Kifaransa

Visiwa, funguvisiwa na atolli za Polinesia ya Kifaransa kwa jumla vina eneo la nchi kavu la km² 4,167 jumla vilivyosambazwa katika kilomita za mraba 2,500,000 za bahari.

Visiwa vyote vimegawiwa katika tarafa tano ambazo ni vikundi vya visiwa vyenye mafunguvisiwa ndani yake; ni kama zifuatazo:

Watu hariri

Wakazi ni 268,270 (sensa ya mwaka 2012), ambao kati yao 2/3 ni Wapolinesia asilia na 11,9% ni Wazungu.

Kati yao wote, 68,5% wanatumia kwa kawaida lugha ya Kifaransa, iliyo lugha rasmi pekee.

Upande wa dini, 54% ni Waprotestanti, 30% ni Wakatoliki, halafu kuna Wamormoni na Mashahidi wa Yehova.

Tazama pia hariri


  Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.