Bab

(Elekezwa kutoka Báb)

Bab (kwa Kiarabu: الباب al-bab, wa maana ya "Geti la Mungu"; 20. Oktoba 1819 huko Shiraz, Iran; 9. Julai 1850 huko Tabriz, Iran) ni jina la heshima la kidini la Seyyed ʿAli Muhammad Shirazi (kwa Kifarsi: سيد علی ‌محمد شیرازی ) aliyekuwa mwanzilishi wa dini ya Ubabi. Wababi na Wabahai wanaamini alikuwa ufunuo wa Mungu.

Kaburi la Bab (Bustani ya Wabahai huko Haifa, Israeli).
Nyumba ya Bab huko Shiraz iliharibiwa na kubadilishwa kuwa msikiti.

Familia hariri

Baba wa Sayyid Ali Muhammad alikuwa mfanyabiashara mashuhuri mjini Shiraz, alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa kwake, kwa hiyo alilelewa na mjomba Haji Mirza Sayyid Ali, mfanyabiashara pia.

Alipofikia umri alijiunga na biashara ya familia akishirikiana na mjomba wake. Alitambuliwa na wenzake kuwa mtu mwaminifu aliyeonyesha ukarimu kwa wale walio na uhitaji. Hakufurahia sana biashara akipendelea kusoma vitabu vya dini ma kutumia muda mwingi katika sala. Mjomba alimtuma Bushehr iliyokuwa wakati ule bandari kubwa ya Uajemi kwenye Ghuba ya Uajemi. Mwaka 1842 alimwoa Khadíjih-Bagum akazaa naye mtoto mmoja aliyeitwa Aḥmad lakini alifariki mapema.

Mazingira ya kidini hariri

Wakati ule kulikuwa na harakati ya "Washeikhi" waliokuwa wafuasi wa Sheikh Ahmad aliyehubiri kurudi kwa Imamu wa 12 aliye Mahdi wa Washia kulikuwa karibu sana. Kiongozi wa pili baada ya Sheikh Ahmad alikuwa Kazim Rashti (1793–1843) aliyewaambia wafuasi wake kuwa Mahdi ameshafika tayari, aliwatuma waende wamtafute. Mmoja wa wafuasi hao alikuwa Mulla Husain aliyesafiri katika miji mingi ya Uajemi (Iran) akimtafuta Mahdi.

Ufunuo hariri

 
Msikiti mkuu wa Shiraz.

Katika Mei 1844 Mulla Husein alifika Shiraz alipokutana na Ali Muhammad aliyemkaribisha kwake nyumbani. Husein akieleza alimtafuta nani, mwenyeji wake alimjibu ni yeye aliyemtafuta.

Usiku ule akiwa mjini Shiraz, Sayyid Ali Muhammad aliandika kwa kasi kubwa mlango wa kwanza wa kitabu chake cha tafsir ya sura 12 ya Kurani huku Mulla Husain na mke wake wakimtazama. Kuanzia usiku ule alijiita Bab, alidai kuwa ni mdomo wa Mungu ulioahidiwa na manabii wa siku za zamani akiwa yeye mlango au geti linalounganisha waumini na Mahdi anayetarijiwa. Mulla Husain alikuwa mwumini wa kwanza aliyekubali ufunuo huo.

Herufi za uhai hariri

Baada ya Mulla Husain kumkubali, Bab alimwambia asubiri kabla ya kuhubiri hadi wafuasi 17 wengine watakapokuwa wamefika kwake. Katika muda mfupi, waumini wengine 17 walimkuta "kwa utafutaji wao wenyewe". Kati ya wanafunzi hao 18 alikuwepo pia mwanamke mmoja, Zarrin Tāj Baraghāni, aliyekuwa mashuhuri kama mshairi kwa jina la Qurrat al-ʿAyn (kwa Kiarabu: "faraja ya macho") au kama Ṭāhira (kwa Kiarabu: "safi"), na baadaye aliitwa mwanaharakati wa kwanza wa haki za wanawake huko Mashariki ya Kati.

Bab aliwaita wanafunzi hao 18 "Herufi Hai" akawatuma kwenda sehemu mbalimbali za Uajemi na Turkestan ili kueneza habari ya kuwasili kwake.

Hija ya kwenda Makka na Madina hariri

Bab mwenyewe alikwenda Hija huko Makka na Madina mnamo Novemba 1844 na "Herufi Hai" Quddus, ambapo alitangaza utume wake wazi. Alitunga barua kwa Sharifu wa Makka akajitangaza kuwa Imamu wa 12.

Kukamatwa na Kufukuza hariri

 
Bab alifungwa katika Ngome ya Maku kabla ya kunyongwa kwake.

Baada ya kurudi Iran, viongozi wa Uislamu walianza kumstaki na kuhubiri dhidi yake. Bab alikamatwa mara ya kwanza Shiraz, baadaye Isfahan. Kutoka kule alitumwa kama mfungwa Teheran na baadaye Tabriz.

Gereza na mauti hariri

 
Tarehe 9 Julai 1850 Bab alitekelezwa hadharani hapa huko Tabriz.

Katika msimu wa joto wa 1847, Bab alihamishwa kwenye ngome ya mlima wa Maku, magharibi mwa Azerbaijan alipofungwa siku 40. Mnamo Julai 1848 alipelekwa huko Tabriz, ambapo alihojiwa na mahakama ya wataalamu wa Uislamu. Walipendekeza kumpa adhabu ya kifo, lakini serikali, ilipendelea alikuwa na wafuasi wengi waliompenda, ilijaribu kumtangaza kichaa. Bab alipigwa vibaya akafungwa tena katika ngome.

Mwaka 1850 waziri mkuu mpya Amir Kabir aliamua kumaliza kesi hiyo akaamuru kumwua. Tarehe 9 Julai 1850 Bab alirudishwa Tabriz akawekwa mbele ya kikosi cha wanajeshi ambao walimpiga risasi. Maiti yake ilitupwa katika shimo. Lakini wafuasi wake wanadai maiti ilichukuliwa kwa siri usiku na kufichwa baadaye katika sehemu mbalimbali hadi alipoletwa Haifa mnamo 1899 na alilazwa na ʿ Abdul-Baha ' katika jengo la kaburi kwenye Mlima Karmeli mnamo 1909.

 
Baada ya kunyongwa kwa Bab, mifupa yake ilihifadhiwa hapa.

Wafuasi wake hariri

Baada ya kifodini chake jumuiya aliyoanzisha iliendelea. Wafuasi wengi walijiunga na Baha Ullah aliyejitangaza kuwa yule aliyetangazwa na Bab na kuanzisha dini ya Baha'i. Wengine walikaa peke yao na ibada za pekee lakini si wengi. Leo hii wako mnamo wafuasi 1,000 wanaoendelea katika mafundisho wa Bab ilhali hawakujiunga na Ubahai.

Upeo wa kufichua hariri

Bab ameandika mengi. Yeye mwenyewe alisema mnamo 1848 kwamba alikuwa ameandika vifungu 500,000. Katika jamii ya Bahai kuna mkusanyo wa dondoo kutoka maandishi ya Bab katika lugha za Ulaya chini ya kichwa "Uteuzi kutoka kwa maandishi yake". Louis Alphonse Daniel Nicolas Karne ya alama saba na Bayan ya Kiarabu na Kiajemi iliyotafsiriwa kwa Kifaransa.

Kazi zake muhimu zaidi ni:

  • Qayyūm al-Asmā (takriban Kijerumani: "Milele wa majina", pia hujulikana kama "Maoni juu ya Surah Joseph")
  • al- Bayan al-'Arabi ("Azimio la Kiarabu")
  • Bayan-i-Farsi ("Azimio la Uajemi")
  • Dala'il-i-Sab'ih (" Ushuhuda Saba ")
  • Kitab-i-Asma (" Kitabu cha Majina ")
  • Kitab-i-panj sha'n (Kijerumani takriban: "Kitabu cha sifa tano")

Ushuhuda wa mtu binafsi hariri

Kutoka kwa Bab hariri

  • [h-net.org Le Livre de Sept Preuves („Sieben Beweise“)]. 1902. 
  • [h-net.org Le Beyan Arabe („arabische Erklärung“)]. 1905. 
  • [h-net.org Le Beyan Persan („persische Erklärung“)]. 4 Bände (1911, 1913, 1914). 
  • [holy-writings.com Eine Auswahl aus seinen Schriften]. Bahá’í-Verlag. 1991. ISBN 3-87037-247-8. 
  • [h-net.org Reading Itself. The Bab’s “Sura of the Bees”. A Commentary on Qur’an 12:93 from the Sura of Joseph (Surat al-nahl, „Sure der Bienen“ [Sure 93 des Qayyum al-Asma’ ‹Ewiger der Namen›])] 5. 1997. 
  • [h-net.org The Persian Bayan. Ongoing Translation (Bayan-i-Farsi, „persische Erklärung“)]. 1,4 ab 1997. 
  • [h-net.org The Bab’s “Journey towards God” (Risalah fi’s-Suluk, „Reise zu Gott“)] 2,1. 1998. 
  • [h-net.org The Primal Point’s Will and Testament („Wille und Testament des Ersten Punktes [der Bab]“)] 7,2. 2004. 

Juu ya Bab hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bab kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.