Pennsylvania ni jimbo la kujitawala la Muungano wa Madola ya Amerika au Marekani. Iko kaskazini-mashariki ya nchi ikipakana na majimbo ya Ohio, West Virginia, Maryland, Delaware, New Jersey na jimbo la New York. Kona ya kaskazini-magharibi yagusa Ziwa Erie na Kanada iko ng'ambo ya ziwa hili.

Sehemu ya Jimbo la Pennsylvania








Pennsylvania
Keystone State, Quaker State

Bendera

Nembo
Nchi Bendera ya Marekani Marekani
Mji mkuu Harrisburg
Eneo
 - Jumla 119,283 km²
 - Kavu 116,074 km² 
 - Maji 3,208 km² 
Tovuti:  http://www.pa.gov/
Ramani ya Pennsylvania

Mji mkuu ni Harrisburg lakini mji mkubwa ni Philadelphia. Kwa miji mingine, angalia Orodha ya miji ya Pennsylvania.

Jina la jimbo latokana na jina la William Penn aliyepewa ardhi ya kuanzisha makazi kwa ajili ya kundi la kidini la Maquaker. Jina la jimbo latafsiriwa kama "misitu ya Penn". Pennsylvania ilikuwa moja ya makoloni 13 asilia ya Uingereza yaliyoasi dhidi ya nchi mama baada ya mwaka 1776 na kuanzisha Muungano wa Madola ya Amerika .

Pennsylvania ina wakazi 12,281,054 kwenye eneo la 119,283 km². Zaidi ya nusu huishi katika maeneo ya miji mikubwa Pittsburgh na Philadelphia. Kaskazini ya jimbo ina watu wachache.

Sehemu kubwa ya eneo la jimbo ni milima ya Appalachi. Mito mikubwa ni Monongahela, Allegheny na Ohio.

Miji Mikubwa hariri

  1. Philadelphia 1,447,395 (2008)
  2. Pittsburgh 316,718 (2006)
  3. Allentown 106,632
  4. Erie 103,817 (2008)
  5. Reading 81,207
  6. Scranton 72,485


 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Majimbo ya Marekani

AlabamaAlaskaArizonaArkansasCaliforniaColoradoConnecticutDelawareFloridaGeorgiaHawaiiIdahoIllinoisIndianaIowaKansasKentuckyLouisianaMaineMarylandMassachusettsMichiganMinnesotaMississippiMissouriMontanaNebraskaNevadaNew HampshireNew JerseyNew MexicoNew YorkNorth CarolinaNorth DakotaOhioOklahomaOregonPennsylvaniaRhode IslandSouth CarolinaSouth DakotaTennesseeTexasUtahVermontVirginiaWashingtonWest VirginiaWisconsinWyoming

  Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Pennsylvania kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.