Mkoa wa Unguja Kaskazini

Mkoa wa Unguja Kaskazini ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 73000. Uko Unguja ambayo ni kisiwa kikubwa cha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mahali pa Unguja Kaskazini katika Tanzania
Mkoa wa Kaskazini Unguja, Tanzania

Makao makuu ya mkoa yako Mkokotoni.

Kuna wilaya mbili ambazo ni Kaskazini Unguja 'A' (105,780 mwaka 2012 na 157,369 mwaka 2022) na Kaskazini Unguja 'B' (81,675 mwaka 2012 na 99,921 mwaka 2022)[1][2].

Eneo la mkoa ni km² 470 ambako kuna jumla ya wakazi 257,290 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022[3].

Wengi wanajishughulisha na uvuvi na kilimo. Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna kilimo cha karafuu.

Upande wa magharibi utalii umeanza kuwa muhimu. Eneo la Ras Nungwi ni sehemu moja yenye mahoteli ya watalii wa nje.

Kisiwa cha Tumbatu ni sehemu ya mkoa huu.

Miji ya mkoa ndiyo Mkokotoni, Mahonda na Gamba.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri


  Makala hii kuhusu maeneo ya Unguja bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Unguja Kaskazini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.