Uislamu nchini Afrika Kusini

Uislamu kwa nchi


Uislamu nchini Afrika Kusini ni dini ndogo sana, inakadiriwa kuna asilimia chini ya 1.5 ya jumla ya wakazi wote, kulingana na hesabu yao. Uislamu nchini humo umekua katika hatua tatu. Hatua ya kwanza ni ile ya uletaji wa Waislamu wakiwa kama sehemu ya wahamaiaji watumwa waliokuja pasipo-hiari, wafungwa wa kisiasa na wale waliouhamishoni kisiasa kutoka Afrika na Asia (hasa Funguvisiwa vya Indonesia) ambao uliisha tangu katikati mwa miaka ya 652 hadi 1800. Hatua ya pili ulikuwa ujio wa Wahindi kama wafanyakazi wa mikataba waliokuwa wakifanya kazi katika mashamba ya miwa kwa ajili ya sukari huko mjini Natal kati ya 1860 na 1868, na tena kuanzia 1874 hadi 1911. Inakadiriwa Wahindi 176,000 ambao wote walikuwa wa imani moja ya Uislamu walisafirishwa kwenda jimboni Natal, karibia asilimia 7-10 ya meli ya awali wote walikuwa Waislamu.

Hatua ya tatu imeonekana wakati wa baada ya apartheid – wimbi kubwa la Waafrika Waislamu waliwasili katika pwani na mipaka ya Afrika Kusini. Idadi ya sasa inakadiriwa kuwa kati ya 75-100 000. Ongezeko hili huhesabiwa kama idadi ya Waislamu waliowasili kama wageni kutoka Uhindi kwa minajili ya kukuza uchumi.[1]Ingawa sehemu kubwa ya Waislamu wa nchini humo ni wa dhehebu la Sunni, idadi kidogo sana ambao ni Ahmadi, hasa katika mji wa Cape Town.[2]

Tazama pia hariri

  • Msikiti wa Nurul Islam, msikiti uliopo mjini Cape ambao ulianzishwa mnamo 1844.
  • Nizamiye Masjid msikiti kubwa katika Kizio cha Kusini; upo mjini Midrand, Gauteng, umemalizika mnamo 2012.

Marejeo hariri

  1. Faizal Dawjee. "Muslims in the Struggle.". Iliwekwa mnamo 24 May 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Abdulkader Tayob. Islamic Resurgence in South Africa: The Muslim Youth Movement. uk. 104. Iliwekwa mnamo May 31, 2014.  Check date values in: |accessdate= (help)

Jisomee hariri

  • [1] Islam in South Africa