Indonesia ni nchi ya visiwa katika Asia ya Kusini-Mashariki. Iko upande wa Kusini-Mashariki kati ya Bahari ya Uhindi na Pasifiki.

Indonesia


Visiwa vyake ni sehemu ya Funguvisiwa la Malay, ingawa Guinea Mpya kwa kawaida haihesabiwi katika fungu hilo.

Indonesia imepakana na Papua Guinea Mpya kwenye kisiwa cha Guinea Mpya, pia na Timor ya Mashariki kwenye kisiwa cha Timor, halafu na Malaysia kwenye kisiwa cha Borneo.

Nchi nyingine zilizo karibu ni Australia, Singapur na Ufilipino.

Jiografia hariri

Indonesia ni nchi ya visiwa 18,000 ilhali zaidi ya 6,000 kati ya hivyo vinakaliwa na watu.

Visiwa vikubwa vyenye wakazi wengi ni hasa vitano:

Historia hariri

Visiwa vya Indonesia viliathiriwa na utamaduni wa Uhindi. Kisiasa kulikuwa na falme nyingi.

Tangu karne ya 17 Waholanzi walianza kujenga vituo na kueneza utawala wao. Waliita koloni lao "Uhindi wa Kiholanzi" ("Nederlands-Indië").

Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia Japani ikatwaa visiwa na kuwafukuza Waholanzi.

Mwisho wa vita kiongozi Sukarno akatangaza Indonesia kama nchi huru. Waholanzi walijaribu kurudisha utawala wao lakini walilazimishwa na Marekani kukubali uhuru wa nchi.

Wakazi, lugha, utamaduni, dini hariri

Nchi ina wakazi 270,203,917 (2020) hivyo ina nafasi ya nne kati ya mataifa makubwa duniani. Ni nchi yenye Waislamu wengi kuliko nyingine zote duniani. Makabila asili ni 300 hivi; kubwa zaidi ni Wajava (42 %).

Lugha rasmi ni Bahasa Indonesia (Kiindonesia) iliyoundwa katika karne ya 20 kama lugha ya taifa kutokana na lahaja ya Kimalay. Nchini kote kuna lugha za asili zaidi ya 700 (angalia orodha ya lugha za Indonesia). Jawa pia ina sanaa ya mwandiko wa kipekee maarufu kama mwandiko wa Batiki (Batik Tulus) unaochorwa kwa jora za nguo.[1]

Idadi kubwa ya wakazi (87.2 %) wanahesabiwa kuwa Waislamu (karibu wote Wasuni), 9.8 % kama Wakristo (Waprotestanti 6.9 %, Wakatoliki 2.9 %), 1.6 % kama Wahindu na 0.7 % kama Wabuddha. Wahindu wako hasa kwenye kisiwa cha Bali. Hizo zote ni dini zilizotambulika rasmi pamoja na ile ya Konfusio (0.05 %).

Picha hariri

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Batik S128. Handwriting Batik (Batik Tulis) and Cities In Indonesia That Produce It. Toko Batik Online 2019. Iliwekwa mnamo 2019-05-11.

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


  Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Indonesia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.