Indonesia
Indonesia ni nchi za visiwa katika Asia ya Kusini-Mashariki. Iko upande wa Kusini-Mashariki kati ya Bahari ya Hindi na Pasifiki. Visiwa vyake ni sehemu ya Funguvisiwa la Malay, ingawa Guinea Mpya kwa kawaida haihesabiwi katika fungu hilo. Indonesia imepakana na Papua Guinea Mpya kwenye kisiwa cha Guinea Mpya, pia na Timor ya Mashariki kwenye kisiwa cha Timor, halafu na Malaysia kwenye kisiwa cha Borneo. Nchi nyingine zilizo karibu ni Australia, Singapuri na Ufilipino.
Jamhuri ya Indonesia Republik Indonesia (Kiindonesia) | |
---|---|
Kaulimbiu: Bhinneka Tunggal Ika (Kijava cha Kale) "Umoja katika Tofauti" | |
Wimbo wa taifa: "Indonesia Raya" | |
Mji mkuu na mkubwa | Jakarta |
Lugha rasmi | Kiindonesia |
• Rais | Prabowo Subianto |
• Makamu wa Rais | Gibran Rakabuming Raka |
• Uhuru kutangazwa | 17 Agosti 1945 |
• Kutambuliwa rasmi | 27 Desemba 1949 |
Eneo | |
• Jumla | km2 1,904,569 (ya ya 14) |
• Maji (asilimia) | 4.85% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2024 | ▲ 284,973,643 |
• Msongamano | 143/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ▲ $4.98 trilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $17,520 |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ▲ $1.49 trilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $5,248 |
HDI (2023) | 0.728 juu |
Gini (2024) | 37.9 |
Sarafu | Rupia ya Indonesia (Rp) |
Majira ya saa | UTCUTC+7, +8, +9 (WIB, WITA, WIT) |
Upande wa magari | Kushoto |
Msimbo wa simu | ++62 |
Jina la kikoa | .id |
Indonesia ni taifa lenye wakazi wengi wa Kiislamu duniani, likiwa na idadi ya watu inayozidi milioni 270, na hivyo kuifanya kuwa nchi ya nne kwa idadi ya watu duniani. Mji mkuu wake ni Jakarta, jiji kubwa lenye shughuli nyingi za kisiasa, kiuchumi na kitamaduni. Lugha rasmi ni Kiindonesia (Bahasa Indonesia): ingawa kuna zaidi ya lugha 700 zinazozungumzwa nchini humo, lugha hiyo inatumika kama chombo cha kuunganisha wananchi wa makabila mbalimbali.
Historia ya Indonesia imeathiriwa na mchanganyiko wa dini, biashara na ukoloni. Kabla ya ukoloni, Indonesia ilikuwa nyumbani kwa falme mbalimbali zenye ushawishi mkubwa kama vile Srivijaya na Majapahit. Katika karne ya 16, Wareno na baadaye Waholanzi walifika na kudhibiti maeneo mengi, hasa kupitia Kampuni ya Kiholanzi ya India ya Mashariki. Indonesia ilijipatia uhuru kutoka kwa Uholanzi mwaka 1945 chini ya uongozi wa Sukarno. Tangu wakati huo, nchi imepitia vipindi mbalimbali vya kisiasa, ikiwa ni pamoja na utawala wa kijeshi, hadi kuanzishwa kwa demokrasia ya kisasa mwishoni mwa karne ya 20.
Jiografia
haririIndonesia ni nchi ya visiwa 18,000 ilhali zaidi ya 6,000 kati ya hivyo vinakaliwa na watu.
Visiwa vikubwa vyenye wakazi wengi ni hasa vitano:
- Guinea Mpya (pamoja na nchi ya Papua Guinea Mpya)
- Java
- Kalimantan (Borneo ya Kiindonesia)
- Sulawesi
- Sumatra
Historia
haririVisiwa vya Indonesia viliathiriwa na utamaduni wa Uhindi. Kisiasa kulikuwa na falme nyingi.
Tangu karne ya 17 Waholanzi walianza kujenga vituo na kueneza utawala wao. Waliita koloni lao "Uhindi wa Kiholanzi" ("Nederlands-Indie").
Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia Japani ikatwaa visiwa na kuwafukuza Waholanzi.
Mwisho wa vita kiongozi Sukarno akatangaza Indonesia kama nchi huru. Waholanzi walijaribu kurudisha utawala wao lakini walilazimishwa na Marekani kukubali uhuru wa nchi.
Demografia
haririNchi ina wakazi 270,203,917 (2020) hivyo ina nafasi ya nne kati ya mataifa makubwa duniani. Ni nchi yenye Waislamu wengi kuliko nyingine zote duniani. Makabila asili ni 300 hivi; kubwa zaidi ni Wajava (42 %).
Lugha rasmi ni Bahasa Indonesia (Kiindonesia) iliyoundwa katika karne ya 20 kama lugha ya taifa kutokana na lahaja ya Kimalay. Nchini kote kuna lugha za asili zaidi ya 700 (angalia orodha ya lugha za Indonesia). Jawa pia ina sanaa ya mwandiko wa kipekee maarufu kama mwandiko wa Batiki (Batik Tulus) unaochorwa kwa jora za nguo.[1]
Idadi kubwa ya wakazi (87.2 %) wanahesabiwa kuwa Waislamu (karibu wote Wasuni), 9.8 % kama Wakristo (Waprotestanti 6.9 %, Wakatoliki 2.9 %), 1.6 % kama Wahindu (hasa kwenye kisiwa cha Bali) na 0.7 % kama Wabuddha. Hizo zote ni dini zilizotambulika rasmi pamoja na ile ya Konfusio (0.05 %).
Mandhari
hariri-
National Museum of Indonesia, Central Jakarta
-
Wisma 46, jengo refu kuliko yote ya Indonesia, likiwa Jakarta
-
Jalan Thamrin, barabara muhimu zaidi ya Central Jakarta
-
Treni katika stesheni ya Gambir, Central Jakarta
-
Bung Karno Stadium inaweza kupokea watazamaji 100,000
-
Ramani ya Indonesia
-
Wilaya za Indonesia
-
Malioboro, barabara muhimu zaidi huko Yogyakarta
-
Trans Jogja Bus, mwendokasi wa Yogyakarta
-
Mapishi ya Kiindonesia: Soto Ayam (chicken soup), sate kerang (shellfish kebabs), telor pindang (preserved eggs), perkedel (fritter) na es teh manis (sweet iced tea)
-
An Indonesian Army infantryman participating in the U.N.'s Global Peacekeeping Operation Initiative
-
Pindad Panser "Anoa" shown during Indo Defense and Aerospace Expo 2008
-
B-25 Mitchell bombers of the AURI in the 1950s
-
GE U20C in Indonesia, #CC201-05
-
GE U20C "Full-Width Cabin" in Indonesia, #CC203-22
-
GE U20C full computer control locomotive in Indonesia, #CC204-06
Tazama pia
haririTanbihi
hariri- ↑ Batik S128. "Handwriting Batik (Batik Tulis) and Cities In Indonesia That Produce It". Toko Batik Online 2019. Iliwekwa mnamo 2019-05-11.
{{cite web}}
: CS1 maint: numeric names: authors list (link)
Viungo vya nje
hariri- Serikali
- Tovuti rasmi Ilihifadhiwa 17 Februari 2012 kwenye Wayback Machine. (Kiindonesia) (Kiingereza)
- Government of Indonesia Ilihifadhiwa 17 Februari 2012 kwenye Wayback Machine.
- Minister of The State Secretary (Kiindonesia)
- Statistics Center
- Chief of State and Cabinet Members Ilihifadhiwa 12 Oktoba 2014 kwenye Wayback Machine.
- Taarifa za jumla
- Indonesia entry at The World Factbook
- Indonesia Ilihifadhiwa 26 Aprili 2009 kwenye Wayback Machine. from UCB Libraries GovPubs
- Indonesia katika Open Directory Project
- Indonesia profile from the BBC News
- Indonesia at Encyclopædia Britannica
- Wikimedia Atlas of Indonesia
- Official Site of Indonesian Tourism
- Key Development Forecasts for Indonesia from International Futures
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |