Tajikistan ni nchi ndogo ya Asia ya Kati ambayo haina pwani kwenye bahari yoyote.

Tajikistan
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
38°33′ N 68°48′ E
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY
Ramani ya Tajikistan

Imepakana na Uchina, Afghanistan, Uzbekistan na Kyrgyzstan.

Eneo lake ni km² 143,100.

Idadi ya wakazi ni milioni 9.3.

Jiografia hariri

Sehemu kubwa ya nchi ni milima ya Pamir yenye kimo kati ya mita 3600 na 4400.

Historia hariri

Kihistoria maeneo ya Tajikistan yalitawaliwa na madola mbalimbali, hasa na Uajemi.

Uislamu ulifika huko mnamo mwaka 800 BK.

Mwaka 1868 Tajikistan ilivamiwa na Urusi na kuwa sehemu ya Dola la Urusi, halafu sehemu ya Umoja wa Kisovyet baada ya mapinduzi ya 1917. Tangu mwaka 1929 iliitwa Jamhuri ya Kisovyet ya Kisoshalisti ya Tajikistan.

 
Dushanbeː kituo cha reli.

Baada ya kuporomoka kwa Umoja wa Kisoviet, Tajikistan ilipata uhuru wake mwaka 1991.

Kati ya mwaka 1992 hadi 1997 kulikuwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo ilisababisha Warusi wengi kuondoka na ilikwisha kwa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Baada ya mashambulio ya kigaidi ya tarehe 11 Septemba 2001 jeshi la Marekani lilipata nafasi ya kutumia vituo vya kijeshi kwa ajili ya vita katika Afghanistan.

Watu hariri

Wakazi wengi ni Watajiki na kuongea Kitajiki (84.2%), lugha ambayo inahusiana na Kiajemi. Ndiyo lugha rasmi na ya kawaida. Kabila linalofuata kwa ukubwa ni Wauzbeki (13.9%). Angalia pia orodha ya lugha za Tajikistan.

Wananchi wengi ni Waislamu (96.7%), hasa Wasuni, na ndiyo dini rasmi tangu mwaka 2009; Washia ni 3%. Wakristo ni 1.6%, hasa Waorthodoksi na Waprotestanti.

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


  Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tajikistan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.