Cabo Verde
| |||||
Lugha rasmi | Kireno | ||||
Mji Mkuu | Praia | ||||
Mji Mkubwa | Praia | ||||
Serikali | Jamhuri | ||||
Rais | Jorge Carlos Fonseca | ||||
Waziri Mkuu | Ulisses Correia e Silva | ||||
Eneo | km² 4,033 | ||||
Idadi ya wakazi | 543,767 (2018) | ||||
Wakazi kwa km² | 123.7 | ||||
Uchumi nominal | Bilioni $2.042 | ||||
Pesa | Eskudo ya Cabo Verde | ||||
Kaulimbiu | "Umoja, Kazi, Maendeleo" | ||||
Wimbo wa Taifa | Chimbo ya Uhuru | ||||
![]() |
Cabo Verde (ing. Cape Verde) ni nchi ya visiwa katika bahari ya Atlantiki mbele ya pwani ya Afrika ya Magharibi.
JiografiaEdit
Eneo la visiwa vyake kwa jumla ni km² 4,033.
Funguvisiwa vyake ina visiwa 15 katika vikundi viwili:
- Visiwa "juu ya upepo" (Barlavento): Santo Antão, São Vicente, São Nicolau, Sal, Boa Vista na visiwa bila watu vya Santa Luzia, Branco na Razo.
- Visiwa "chini ya upepo" (Sotavento): Maio, Santiago, Fogo, Brava na visiwa bila watu vya Ilheus Secos ou do Rombo.
MijiEdit
Mji mkuu ni Praia katika kisiwa cha Santiago.
Miji mikubwa zaidi ni (takwimu za mwaka 2005): Praia (wakazi 113.364), Mindelo (wakazi 70.611), Santa Maria (wakazi 17.231), Pedra Badejo (wakazi 9.488) na São Filipe (wakazi 8.189).
HistoriaEdit
Hadi kufika kwa Wareno katika karne ya 15 visiwa vya Cabo Verde havikuwa na watu.
Wareno walianzisha mashamba ya miwa na kuleta watumwa kutoka bara la Afrika.
Cabo Verde ilikuwa pia kituo muhimu cha biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika.
Wahamiaji kutoka Ulaya walikuwa pia Wahispania, Waitalia pamoja na Wayahudi na Waislamu waliokataliwa kukaa kwao Ureno.
WatuEdit
Kutokana na historia hiyo, leo idadi kubwa ya wakazi ni machotara waliozaliwa na Waafrika (waliochangia 56% ya DNA) na Wazungu (waliochangia 44%).
Lugha rasmi ni Kireno, lakini wakazi wanazungumza aina mbalimbali za Krioli iliyotokana na lugha hiyo.
Upande wa dini, walau 89.1% ya wakazi ni Wakristo, hasa wa Kanisa Katoliki (78.7%), lakini pia wa madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (10.4%).
Kutokana na hali ngumu ya uchumi, wananchi wanaoishi nje ya Cabo Verde ni wengi kuliko wale wanaoishi nchini. Kati ya waliohama baada ya uhuru (1975), 500,000 wanaishi Marekani na 150,000 Ureno.
Tazama piaEdit
MarejeoEdit
- J.Pim, C. Pierce, A.B.Watts, I. Grevemeyer, A. Krabbenhoeft (5 May 2008). Crustal structure and origin of the Cape Verde Rise. 272. Elesiever. pp. 422–428.
. http://www.earth.ox.ac.uk/~tony/watts/downloads/Pim_etal_2008.pdf. Retrieved 2015-07-18.
- Carling, Jorgen (2004). "Emigration, Return and Development in Cape Verde: The Impact of Closing Borders". Population, Space and Place (John Wiley & Sons, Ltd.) 55 (10): 113–132.
. . http://www.researchgate.net/publication/227504366_Emigration_return_and_development_in_Cape_Verde_the_impact_of_closing_borders.
- Ramalho, R.; Helffrich, G.; Schmidt, D.; Vance, D. (2010). "Tracers of Uplift and Subsidence in the Cape Verde Archipelago". Journal of the Geological Society (London: Geological Society of London) 167 (3): 519–538.
. https://www.geolsoc.org.uk/en/Publications/Supplementary%20Publications/2010/~/media/Files/GSL/shared/Sup_pubs/2010/18390SupPub.ashx.
Viungo vya njeEdit
- Official website of the Government of Cape Verde
- Cabo Verde katika Open Directory Project
- Cape Verde entry at The World Factbook
- Cape Verde from State.gov
- Country Profile from BBC News
- Cape Verde entry on Encyclopædia Britannica
- Cape Verde Archived Oktoba 7, 2008 at the Wayback Machine. from UCB Libraries GovPubs
- Key Development Forecasts for Cape Verde from International Futures
- Cape Verde 2012
- Amateur Radio Cabo Verde
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Cabo Verde kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |